Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Kuna mzozo mkubwa umeibuka katika ndoa fulani baada ya mdada mmoja kuwa na mazoea ya kupiga simu redioni kumtakia njozi njema mpenzi wake xxx (akimtaja kwa majina matatu)...
Jamaa anayetajwa ni mume wa mtu, ambaye ameenda chuo kuongeza ilmu, na kumuacha mkewe akilea familia. katika hali ya kushangaza, kuna dada amejitokeza (na inahisiwa ni wmanachuo mwenzake), anapiga simu kwenye vipindi vya redio kadhaa hasa usiku, kumsalimu na kumtakia njozi njema jamaa huyo ambapo huyo dada ili kuwa specific amekuwa akitaja majina matatu, chuo anachosoma, na wakati mwingine koz anayosoma. Tena anaenda mbali zaidi na kutaja eneo jamaa anakoishi (namnukuu, ..."namtakia likizo njema na njozi njema huko .... aliko mapumzikoni nyumbani kwa sasa) wakati wa likizo.
jamaa alishamwelewesha mkewe kuwa hajui kinachoendelea, lakini siku zinavyozidi kwenda, mgogoro unazidi kuongezeka, maana almost kila siku huyo dada lazime apige simu kwenye hata zaidi ya kituo kimoja cha redio, vipindi vya usiku.
Imekuwa kero kwani sasa inajulikana kwa ndugu, jamaa na rafiki wa pande zote, ambao wamekuwa wakisikia salamu hizo au kuahdithiana. Jamaa kwa sasa anafanya taratibu za kupata namba za huyo dada kwenye vituo vya redio kadhaa, japo namba aliyopewa na kituo kimoja ilikuwa haipatikani kila alipopiga na amepeleka malalamiko tume ya mawasiliano, japo hajapata majibu...
Kuna haja ya vituo vya redio na TV kuwa makini na haya mambo maana wasio na nia njema wanaweza kutumia hzi fursa vibaya...
Jamaa anayetajwa ni mume wa mtu, ambaye ameenda chuo kuongeza ilmu, na kumuacha mkewe akilea familia. katika hali ya kushangaza, kuna dada amejitokeza (na inahisiwa ni wmanachuo mwenzake), anapiga simu kwenye vipindi vya redio kadhaa hasa usiku, kumsalimu na kumtakia njozi njema jamaa huyo ambapo huyo dada ili kuwa specific amekuwa akitaja majina matatu, chuo anachosoma, na wakati mwingine koz anayosoma. Tena anaenda mbali zaidi na kutaja eneo jamaa anakoishi (namnukuu, ..."namtakia likizo njema na njozi njema huko .... aliko mapumzikoni nyumbani kwa sasa) wakati wa likizo.
jamaa alishamwelewesha mkewe kuwa hajui kinachoendelea, lakini siku zinavyozidi kwenda, mgogoro unazidi kuongezeka, maana almost kila siku huyo dada lazime apige simu kwenye hata zaidi ya kituo kimoja cha redio, vipindi vya usiku.
Imekuwa kero kwani sasa inajulikana kwa ndugu, jamaa na rafiki wa pande zote, ambao wamekuwa wakisikia salamu hizo au kuahdithiana. Jamaa kwa sasa anafanya taratibu za kupata namba za huyo dada kwenye vituo vya redio kadhaa, japo namba aliyopewa na kituo kimoja ilikuwa haipatikani kila alipopiga na amepeleka malalamiko tume ya mawasiliano, japo hajapata majibu...
Kuna haja ya vituo vya redio na TV kuwa makini na haya mambo maana wasio na nia njema wanaweza kutumia hzi fursa vibaya...