kwa wale wajasiriaardhi inatakiwa kujua hii mamboi ili kuepuka kuibiwa.
ekari moja ni sawa na eneo lenye ukubwa wa mita za mraba elfu nne (4000m[SUP]2[/SUP]) mfano.viwanja vingi vya mpira huwa na urefu wa mita tisini 90m na upana wa mita arobaini na tano 45m. ukichukua 45x90 unapata mita za mraba 4050m[SUP]2. [/SUP]kwa hiyo tunaweza sema ekari moja ni sawa na uwanja wa mpira wenye vipimo standard. kama shamba unalonunua haliko na pembe nne unaweza omba msaada kwa mtaalamu akusaidie kupima eneo. kumbuka hapa hatuongelei vipimo kuwa 45x90 bali eneo lazima liwe 4000m[SUP]2[/SUP] kwa hiyo kama shamba lako lina urefu na upana wa 50x40m basi ni eka sababu litakuwa na eneo la 4000m[SUP]2
[/SUP]hekta moja ni sawa na ekari mbili na nusu. ni eneo lenye ukubwa wa 10,000m[SUP]2 [/SUP]au sawa na eneo la 100mx100m au 250mx40m au 500mx20m
wenu katika ujasiriamali,
Red Giant.
Samahani mkuu, na hii ya 70m x 70m ambayo ndio maarufu sana imetoka wapi? Mara nyingi sana hii ya 4900sq meters inatumika kama unit ya acre moja.
Punje, hapo umemaliza na hasa ulivyoeleza source ya huu mchanganyo wa 70 x 70!!..70 X 70 imetokana na vipimo vya YADI; katika vipimo hivyo eka ilihesabika ni yadi 70 kwa yadi 70; na hatua moja ya mtu mzima ililinganishwa na yadi moja. Yadi moja ni sawa na futi tatu kama ninakumbuka vizuri. hivyo eka moja nisawa na yadi 4,900 za mraba; 4,900 yd[SUP]2[/SUP]. kwa ufahamu zaidi YADI 1 NI SAWA NA MITA 0.9144; AU MITA 1 NI SAWA NA YADI 1.093613298337708. NIDHANIITAWASIDIA WENGI.
acre ni saw na ekari? kwnye vipimo katika square metre inakuaje au ina ukubwa gani wakuu kwa units hzo?
Samahani mada ni ya muda mrefu sana hii ila naomba kujua, nikitaka kupata kipimo halisi nitumie kifaa gani hasa kama nataka kupima eka kumi za pamoja. AsantePunje, hapo umemaliza na hasa ulivyoeleza source ya huu mchanganyo wa 70 x 70!!
Amini amini nawaambia taarifa nyingi hapa Tz hasa kutoka kwa wataalam wasiokuwa makini ni zenye ubora wa chini sana na hazina usahihi kabisa! Taarifa hizo zinaweza kukupoteza ukadhani mambo ni mazuri au mabaya kumbe ni kinyume chake! Mkulima anaulizwa unashamba lenye ukubwa wa ekari ngapi, umevuna kiasi gani, kijiji kizima kinajumla ya eka ngapi! Mara nyingi takwimu zitolewazo toka kwa wakulima walio wengi juu ya maeneo yao ya uzalishaji huwa ni haya mashamba yaliyopimwa kwa kutembea tena kwa kuhesabu hatua 70 x 70 !
Hebu fikiria kama mpimaji wa shamba hatua yake ni sawa na cm 75 akipima hatua 70 atapata urefu wa sm 75 x 70 = sm 5,250 ukibadili kipimo cha sm kuwa mita sm 5,250 ni sawa na urefu wa mita 52.5. Kwa hiyo kupima hatua 70 x 70 ni sawa na kupima mita 52.5 x mita 52.5 = mita mraba 2756.25.
Hebu sasa linganisha eneo halali la ekari moja (mita mraba 4000) na eneo la ekari Feki 2756.25 tunazopimiwa kienyeji !!! Eneo la Ekari Feki ni asilimia 69 ya ekari halisi! Yaani katika kila ekari 100 unazopimiwa eka halisi ni 69 tu!!
Naomba nisisitize kuwa upana wa hatua ya sm 75 niliotumia ndiyo hali halisi maana wapimaji wengi hupima kwa kutembea kawaida, wachache sana hufikia hatua ya kukaribia mita moja (sm 100)!
Kwa hiyo ndugu zangu mavuno mengi tunayoambiwa hutokana na eneo feki hilo, unaweza kusema mkulima kapata kipato kidogo lakini ukikokotoa kwa ekari moja halisi unakuta amejitahidi sana! Pia eneo feki lina hasara moja mkulima anatumia madawa, mbolea na kiasi cha mbegu iliyoshauriwa kwa eneo la ekari moja yeye huweka kwenye eka moja feki, kwa hiyo au anazidisha dozi au anapata gharama kubwa isivyostahili.
Changamoto kwenu wajasiria mali wa kilimo, ACHANENI KABISA na upimaji wa maeneo ya mashamba kwa kutembea! Mtu mrefu na mfupi hatua zao tofauti, mtu aliyeshiba na mwenye njaa hatua zao tofauti, mtu anaeuza na anaenunua shamba hatua zao tofauti, mlimani na mabondeni hatua ni tofauti, shamba safi na chafu hatua zake tofauti! Kama unanunua shamba, au unakodi ukakuta mwenye mali hataki kupima kwa kipimo halisi basi wewe kubali yaishe ukishamiliki shamba pima mwenyewe ili ujihakikishie pasi na shaka eneo halisi la shamba lako! Poleni kuwachosha wandugu maana nami sinaga dogo mweee!! Mheshimiwa Malila nakusalimia sana popote ulipo, umenitia chachu kwa ushauri na ukarimu wako wa kumegeana maarifa nimeamua nifuate nyayo zako!
Mkuu vipi, Kuna jamaa anataka kuniuzia kiwanja ila anasema robo eka ni 22mx17.5m...70 X 70 imetokana na vipimo vya YADI; katika vipimo hivyo eka ilihesabika ni yadi 70 kwa yadi 70; na hatua moja ya mtu mzima ililinganishwa na yadi moja. Yadi moja ni sawa na futi tatu kama ninakumbuka vizuri. hivyo eka moja nisawa na yadi 4,900 za mraba; 4,900 yd[SUP]2[/SUP]. kwa ufahamu zaidi YADI 1 NI SAWA NA MITA 0.9144; AU MITA 1 NI SAWA NA YADI 1.093613298337708. NIDHANIITAWASIDIA WENGI.
In a nutshell:-
1 ACRE/EKARI = 4046.8566 SQM
1 HECTARE/HEKARI = 10000 SQM
ekari ni 4000m² hii 70*70 ni local way ya kuhesabu hatua za miguu tu.Ni kweli mkuu ekari1 ni 70mx70m kwahiyo eneo la ekari1 ni mita za eneo au square metres4900 hata kama hilo eneo ni mstatili,pembetatu,trapeza au msambamba au vinginevyo!
Hapa ujanja ni kumtafuta Mtu mrefu unaenda naye kupimaKWA KITAALAM HAKUNA EKARI YA MIGUU,UKUBWA WA EKARI MOJA NI MITA ZA
ENEO 4000 SAWA NA UREFU MITA 100 NA UPANA MITA 40 AU MITA 64 UREFU NA UPANA
MITA 63,KIPIMO CHA MIGUU SIYO SAHIHI INGAWA WATU WENGI HUTUMIA KWA
MAZOEA KWA KUPIMA MIGUU 70 UREFU NA MIGUU 70 UPANA,LAKINI KUMBUKA
WATU TUNATOFAUTIANA UREFU WENGINE NI WAFUPI