Vipimo vinaonesha sitoweza kuzaa, kama kuna msaada tafadhali

Vipimo vinaonesha sitoweza kuzaa, kama kuna msaada tafadhali

GLOOMY

Member
Joined
Jul 24, 2019
Posts
38
Reaction score
102
Awali ya yote, nawasalimu.

Nimeleta hii maada kwenu ni baada ya maumivu makali moyo wangu umeyabeba,na thamani ya maisha siioni tena na sioni haja ya kupalangana na maisha kabisa.

Nimeoa miaka 2 iliyopita,sijabahatika kupata mtoto,mwaka Jana nilifunga safari kwenda Bugando kufanya SPERMS ANALYSIS, majibu yakaja kwamba nilikuwa na low sperm count.

Juzi nimerudi tena Bugando kupima kipimo kile kile jibu nimeambiwa no sperm count (0)

Niliporudi kwa Dr akashauri nikubaliane na hali kwani sitoweza kupata mtoto kabisa.
Najaribu kuupokea ushauri lakini naumia na sijui nini nifanye.

Ombi langu kwenu wa jamii hii
1. Kama juna Dr mtaalamu naomba mawasiliano au connection naye tafadhali

2. Kama kuna njia mbadala ya kutatua hili tatizo,na bi uhakika niko tayari kuifuata

N.b. nimelileta kwenu kupunguza maumivu hasa kwa kunifariji, kunishauri na ikiwezekana kunisaidia.
 
...pole sana mkuu chakufanya tafuta pesa kwa bidii na uwe na mademu wengi kila mtaa lazima atokee mmoja wao kukwambia anayo mimba yako wee usioji mambo mengi lea mimba badae mtoto...si unajua ata yusuph alipiga kimya baada yakujua mariamu mchumbake yuko mimba..nakushauli ndg bora kuishi kwa furaha ya kubumba kuliko kuishi na donda
 
Pole sana kaka. Kwanza kabisa nakushauri.
1. Mkabidhi yesu kristo maisha yako na utubu dhambi zote katika maisha yako.
2. Ishi katika kumtegemea yeye na jinyenyekeze kwake.
3. Uwe ni mtu wa toba na maombi na jenga imani kubwa kwake.

N.B
Usijenge imani yako kwa wachungaji wala makanisa ukawa unasubili wakuombee na kuwa mtumwa wa makanisa Hao nao wanashida zao. Mchungaji ni mmoja tu [emoji117]JESUS CHRIST.


Ushauri wangu ndio huo. Msikilize huyo jamaa wa kihindi. Aliambiwa na madaktali atakufa lakini Jesus akampa maisha na sasa ni mzima wa afya kabisa. Trust in Jesus Christ. Huu ni ushauri wangu kaka. Pole sana
 
Awali ya yote,nawasalimu.
Nimeleta hii maada kwenu Ni baada ya maumivu makali Moyo wangu umeyabeba,na thamani ya maisha siioni Tena na sioni haja ya kupalangana na maisha kabisa...
Pole sana mkuu.Ila kwa ushauri wangu naomba uzingatie "WATER THERAPY" kwa miezi walau mitatu.Ni very very very important.Tumia kwa wingi vyakula vya protini (mfano, karanga,maziwa,mayai nk).Pia epuka kula processed products.Zingatia balanced diet.Ndani ya hiyo miezi nahakika utakuja kutoa ushuhuda hapa.
NB1:EPUKA POMBE +SIGARA + STRESS
NB2:Heri usahau vyote hapo juu ila sio hiyo WATER THERAPY.NI MKOMBOZI WA WENGI,Kama huielewi i-google.[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Matthew 9:27-31 Yesu alipokuwa anapita Yeriko ombaomba kipofu alimuita Yesu mtoto wa Daudi usinipite nisamehe.

Yesu alimwambia kwakuwa umeniamini imani yako imekuponya.

Madaktari watasema lakini Yesu ndiye Daktari mkuu.

Sali na kuomba kwa Yesu hakuna kinachoshindikana.
 
Pole sana mkuu jaribu kuchek na hospital nyingne Tena na majibu yakiwa yaleyale omba kibali Kuna watoto yatima wako weng sana wenye umri chini ya mmoja chukua Lea japo haipunguz maumivu lakin itarejesha Aman kidogo

Ila mkeo ukijua ana mimba ndio utata utaanzia hapo

Kama vip kubali tu mkeo afanye yake iwe sir ya ndani tu ya wawili no way out
 
Pole sana mkuu haya mambo yakukosa kizazi uwezi kuamini kama ujakumbwa nalo au kama huna mtu wakaribu mwenye hili tatizo.

Kiukweli tatizo lipo pole sanaaa ndugu yangu ila kwa Mungu ni swala dogo sana nawala usikate tamaa fanya juhudi kama hizi nahatimae Mungu atakusaidia kutokana najuhudi utazomuonesha kwadhati yamoyo wako.

Mungu ajawahi kumuacha mja wake mwenye kumuomba kilicho chema sanasana kitachelewa2. Mungu akubariki.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom