Mrejesho: Vipimo vinaonesha sitoweza kuzaa, kama kuna msaada tafadhali

GLOOMY

Member
Jul 24, 2019
38
88
Nawasalimu ndugu zangu.

Miezi kadhaa nilileta mada hapa nikashauriwa na kufarijiwa nanyi, ushauri wenu kwa 75% niliufanyia kazi na wengi walishauri kurudia vipimo hospital nyingine hasa Kamanga Hospital na nilifanya kwa mwongozo wa Dr. bingwa.

Majibu yalikuwa yale yale 0 sperm count.
Dr. hadi leo anasema hajui hii hali imesababishwa na nini.

Ukweli sikutaka kurukia hatua nyingine bali nikajitafakali:

1.Mwaka 2008 nilikuwa na mahusiano na mdada, tulifanikiwa kupata mtoto, Ila sikumuoa kwa sababu nilikuwa bado nasoma na nilivyomaliza alikuwa tayari ameshaolewa.

2. Mtoto nilimchukuwa na naishi naye. Lakini kwa matatizo haya ya uzazi nikalazimika kupima DNA huyu mtoto, vipimo vinaonesha ni mtoto wangu.

3. Nina 0 sperms count na siwezi kuzalisha. Nikamrudia mzazi mwenzangu kwa swali la mtego tu (nimepima nimeonekana siwezi kuzalisha, hivyo basi hata mtoto huyu bila shaka sio wangu).

Jibu nililopewa ni kwamba mtoto ni wangu, ila hata yeye hajui kwa nini sizai, mama yake mzazi pia alikiri kuwa ni mtoto wangu Ila mwenzangu alichukia nilivyoenda chuoni na kutomuoa, hivyo nimtumie hela ya nauli aende mkoani akaongee naye kama kuna kitu alikifanya.

Kaka mtu pia alionesha mashaka na aliniahidi kuongea nao, mwisho wa siku alisema yeye kaongea nao lakini mengine nijiongeze mwenyewe.

Lakini ukweli inaonekana nimeumizwa na mzazi mwenzangu, kwa sababu alichukua picha zangu na kuna nguo zangu za ndani zilipotea katika mazingira ya kutatanisha.

Lakini sikutilia shaka kwa sababu ya uchanga wangu kwenye mahusiano na malezi niliyokulia.

Kwenu wadau, jitihada zangu zimeishia kwa kutafuta chanzo lakini suluhisho ndilo liko juu ya uwezo wangu, na sikuwa na imani na masuala haya na sasa yamenipata.

Changamoto ni kujua wataalamu wa kweli maana hapa Mjini wengi wafanyabiashara.

Naomba tena ushauri na connection ya kulitatua hili suala.
 
Kwa Yesu tu ndiyo jibu pekee ndugu yangu, nenda kaombewe ,mng'ang'anie Yesu haswa kikweli kweli, hajawahi kushindwa jambo hata siku moja.

Kama kweli ni huyo mwanamke ndiye amekufanyia ivyo basi amini utapata mtoto tu kwa jina la Yesu Kristu wa Nazareth.

Shetani hana mamlaka juu ya binadamu, mambo ya giza ni muongozo wa shetani huo. Kama nina ushuhuda watu wamepona Ukimwi kwa Yesu, watu wamezaa na mtu alikuwa ameondolewa kizazi kabisa, akaambiwa huwezi kuzaa tena, ni ndugu yangu kabisa katolewa mfuko wa uzazi akaambiwa hawez kuzaa tena lakini kwa jina la Yesu aliweza kuzaa na sasa ana mtoto na ameolewa.

Yesu yupo fanya maamuzi hakuna linaloshindikana kwake.

Pole sana, amini utapona usiwe na shaka.
 
Me naona suala lako ni jepesi sana, funga safari hadi huko kwa mama mkwe wako, mwambie tatizo lako na muombe yeye ndie akusaidie.

Lakini kwann unaridhika na hospital moja tu? Hakuna wataalam wa afya hata mikoa mingine ikibidi vuka boda nchi zingine kwann unajikatia tamaa.
Mama mkwe hawezi nisaidia kwa majibu niliyopewa na shemeji (mtoto wake mkubwa) na akashauri baada ya kuongea nae nami nijiongeze kwa namna nyingie.

Kwa kifupi alinijibu vile kwa sababu nilitishia kumrudisha mtoto akamtafute baba halali.
 
Huyo mtoto mmoja anatosha sana mkuu. Usisikitike kuna wengine hawana hata mtoto wa kusingiziwa. Kama unasimamisha oa mama mwenye watoto hata wawili,mwambie ukweli kama ulivyoeleza hapa. Ishi nae. Ila hiyo familia ya mzazi mwenzio kaa mbali sana nayo,hata mawasiriano kata kabisa. Halafu huwezi amini baada yote,baada ya muda utakuja kuzaa
 
Huyo mtoto mmoja anatosha sana mkuu. Usisikitike kuna wengine hawana hata mtoto wa kusingiziwa. Kama unasimamisha oa mama mwenye watoto hata wawili,mwambie ukweli kama ulivyoeleza hapa. Ishi nae. Ila hiyo familia ya mzazi mwenzio kaa mbali sana nayo,hata mawasiriano kata kabisa. Halafu huwezi amini baada yote,baada ya muda utakuja kuzaa
Nimeoa na Nina miaka 5 kwenye ndoa, Niko imara kwa kila kitu isipokuwa tu kuzalisha. Huyu mke wangu ndicho tatizo, naye anataka Mtoto ili awe na amani na pia fàmilia iwe na amani.
 
Back
Top Bottom