wakuu naombeni mnijuze tofauti kati ya haya maneno, hayati na marehemu.
shukrani mkuu kwa kudadavuaHAYATI, ni mtu alokufa lakini ambae akitajwa hutajwa kwa wema na anaekumbukwa kwa wema, wake na mara nyingi watu hawa wanaoitwa hayati uhai wao walikua na umaarufu fulani.
MAREHEMU, ni mtu yeyote alokwishakufa siku nyingi zilizopita.
wakuu naombeni mnijuze tofauti kati ya haya maneno, hayati na marehemu.
Hayati ni neno la Kiarabu, likiwa na maana aliye hai....!
Waswahili tunalitumia kwa namna mbili, kwa wale wasio hai, likitamkwa kabla ya jina lina maanisha huyo mtu hana uhai.
Mfano kuna huu msemo wa Kiswahili: Si hayati si mamati, (si mzima si mgonjwa)
Neno Marehemu ni neno la kiarabu likitamkwa marhum kwa maana mrehemewa, linatokana na neno Rehma, likimaanisha Huyo mfu amerehemewa.