Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Angali yuko mtini,
Vipi huyo awe wako?
Waninunia mtani.
Nakuuliza kwanini,
Huyo ndege awe wako,
Alama yako nini?
Vipi nisimtamani,
Asiye mkononi mwako?
Wakati yuko mtini.
Ulimtia machoni,
Mara kawa ni wa kwako,
Kwa ubavu gani?
Watuzuia kwa nini,
Wengine na wangaliko,
Sikubali asilani!
Manati i mkononi,
Nikitungua si wako,
Ugomvi wa nini!?
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Vipi huyo awe wako?
Waninunia mtani.
Nakuuliza kwanini,
Huyo ndege awe wako,
Alama yako nini?
Vipi nisimtamani,
Asiye mkononi mwako?
Wakati yuko mtini.
Ulimtia machoni,
Mara kawa ni wa kwako,
Kwa ubavu gani?
Watuzuia kwa nini,
Wengine na wangaliko,
Sikubali asilani!
Manati i mkononi,
Nikitungua si wako,
Ugomvi wa nini!?
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)