Viongozi wastaafu walishtukizwa kuongea na wameongea ukweli

fazili

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
13,810
18,543
Nilikuwa nafuatilia mazishi ya hayati BW Mkapa tangu mwanzo hadi mwisho. Niliona jinsi ambavyo rais wetu alivyo mtaka rais wa Zanzibar kuzungumza na wananchi wa Masasi na Shein alionesha kushtuka kwa hilo kwani hakuwa amearifiwa lakini alikwenda.

Pia akafuata Kikwete na baadaye Mwinyi. Wote walionesha kutofurahishwa na kitendo cha kukurupushwa kuongea bila kutaafiwa.

Anyway, kilichonifurahisha ni kitendo cha mh. Kikwete kuweka mambo sawa kuhusu ukuaji wa uchumi na mambo mengine mengi kama ninavyoyaweka hapa chini kwa kifupi:

1. Mpango wa kufikia uchumi wa kati uliasisiwa na Mkapa na lengo ni kufikia $3000 mwaka 2025 na kusema mpango huo serikali zote zimeufanyia kazi kwa hatua na sio jambo la serikali hii tu

2. Kikwete alionesha ujasiri mkubwa kwa kusema Mkapa alifanya mengi sana lakini hakuwa anapenda kusifiwa. Alitumia neno la kiingereza "populist" na kusema wazi kuwa Mkapa hakuwa populist ila wengi hawakumwelewa alimaanisha nini. Ukiwa kiongozi halafu ukawa populist ni mbaya sana na populist wanachukiwa sana popote kwani huvuruga siasa kwa kujipendekeza kwa namna sisizo nzuri kwa wananchi.

3. Kiwete aliweka wazi wazi kuwa mwaka 1995 kwenye round ya kwanza ya kura za maoni alimshinda Mkapa ila maamuzi ya chama yalimwelekea Mkapa. Na kwamba hata baada ya mchuano huo mkali Mkapa baadaye alifanya kazi kwa karibu na Kikwete na hapakuwepo na uadui. Rejea hatima ya Membe mwaka huu ndani ya CCM kwa kujaribu kumshindanisha JPM.

4. Kikwete aliweka wazi kuwa bado serikali hii ina kazi kubwa kufikia lengo la $3000 mwaka 2025 na kwamba sasa wamefikia $1080 tu bado $1920.

Kikwete alimaliza hatuba yake kwa kusema kuwa hiyo ndio gharama ya kukurupushwa kuongea. Ama kweli Kikwete aliuweka wazi ukweli bila kuogopa, sikutegemea hayo pale msibani.
 
“Mkapa ndiye amefanya kazi kubwa sana kukuza uchumi baada ya kuchukua nchi kutoka kwa Rais Mwinyi ikiwa na uchumi goigoi sana. Alipambana,” -J.M.Kikwete
___________________________

"MAGUFULI Ni wa kipekee Sana, aliikuta nchi iko vibaya Sana kiuchumi yeye ndio katufikisha kwenye uchumi huu mzuri wa Kati"
Rais A.H.Mwinyi.


*Hii inaitwa ukimwaga mboga......🤣*
 
Kwanza mimi nilishangaa serikali hii ilishindwa hata kumpa nafasi Rasmi kwenye ratiba aliyekuwa waziri wake Mkuu yaani Ndugu Sumaye nafasi ya kuongea machache juu ya Marehemu raisi Mkapa, naona kama ni uchoyo fulani wa baadhi ya watu kuhodhi msiba wa marehemu.

Hata wastaafu nao hawakuwekwa rasmi kwenye ratiba ili kumzungumzia mwenzao, uchoyo wa namna gani huu. Eti ni mpaka Magufuli alipojisikia ndo akawastukiza!

Nakumbuka mwaka 1999 kwenye kifo cha Mwalimu, pale uwanja wa Taifa mzee Mwinyi aliwekwa kwenye ratiba ya kumzungumzia mwalimu, mstaafu mwenzie. Lakini cha ajabu safari hii Ratiba yote ilikuwa centred juu ya Magufuli tu!
 
Mkwere sio mnafiki. Anaongea ukweli. Nakumbuka miaka yake walikuwa wakipingana kwa hoja bungeni baadae anawaita ikulu anasikiliza hoja za kila upande then wanamaliza. Hakukuwepo kupigana risasi, kutekana au kupotea kwa watu kwa miaka yote 10. Hongeraaa rais Kikwete.
Acha unafiki. Ni kweli kipindi cha Kikwete hapakuwa na matatizo hayo? Tuwe wakweli, Kikwete alivurunda kwa namna yake na huyu naye anavurunda kwa namna yake. Lakini tangu enzi ya JKN hadi leo kila mmoja ana dosari zake.

Ni Kikwete aliyesema wafanyakazi waandamane wakione. Kuna watu wamepotea kimyakimya.
 
Nilikuwa nafuatilia mazishi ya hayati BW Mkapa tangu mwanzo hadi mwisho. Niliona jinsi ambavyo rais wetu alivyo mtaka rais wa Zanzibar kuzungumza na wananchi wa Masasi na Sheina alionesha kushtuka kwa hilo kwani hakuwa amearifiwa lakini alikwenda. Pia akafuata Kikwete na baadaye Mwinyi. Wote walionesha kutofurahishwa na kitendo cha kukurupushwa kuongea bila kutaafiwa.

Anyway, kilichonifurahisha ni kitendo cha mh. Kikwete kuweka mambo sawa kuhusu ukuaji wa uchumi na mambo mengine mengi kama ninavyoyaweka hapa chini kwa kifupi:
1. Mpango wa kufikia uchumi wa kati uliasisiwa na Mkapa na lengo ni kufikia $3000 mwaka 2025 na kusema mpango huo serikali zote zimeufanyia kazi kwa hatua na sio jambo la serikali hii tu
2. Kikwete alionesha ujasiri mkubwa kwa kusema Mkapa alifanya mengi sana lakini hakuwa anapenda kusifiwa. Alitumia neno la kiingereza "populist" na kusema wazi kuwa Mkapa hakuwa populist ila wengi hawakumwelewa alimaanisha nini. Ukiwa kiongozi halafu ukawa populist ni mbaya sana na populist wanaochukiwa sana popote.
3. Kiwete aliweka wazi wazi kuwa mwaka 1995 kwenye round ya kwanza ya kura za maoni alimshinda Mkapa ila maamuzi ya chama yalimwelekea Mkapa. Na kwamba hata baada ya mchuano huo mkali Mkapa baadaye alifanya kazi kwa karibu na Kikwete na hapakuwepo na uadui. Rejea hatima ya Membe mwaka huu ndani ya CCM.
4. Kikwete aliweka wazi kuwa bado serikali hii ina kazi kubwa kufikia lengo la $3000 mwaka 2025 na kwamba sasa wamefikia $1080 tu

Kikwete alimaliza hatuba yake kwa kusema kuwa hiyo ndio gharama ya kukurupushwa kuongea. Ama kweli Kikwete aliuweka wazi ukweli bila kuogopa, sikutegemea hayo tena mahali pale.
 
Kuna kundi la watu wachache wako busy sana, wanataka kutengeneza chuki kati ya JPM na JMK, au JPM na WADAU

Wanatafutiza mazingira ya kuchomekea chuki/ mgongano/ mabishano / misuguano.

Ni vema wakakatambua kuwa mipango yao yote hata kabla hawajawaza ilishajulikana na mwisho wa siku wataangukia pua.

Summary: Zaburi 57: 6
 
“Mkapa ndiye amefanya kazi kubwa sana kukuza uchumi baada ya kuchukua nchi kutoka kwa Rais Mwinyi ikiwa na uchumi goigoi sana. Alipambana,” -J.M.Kikwete
___________________________

"MAGUFULI Ni wa kipekee Sana, aliikuta nchi iko vibaya Sana kiuchumi yeye ndio katufikisha kwenye uchumi huu mzuri wa Kati"
Rais A.H.Mwinyi.


*Hii inaitwa ukimwaga mboga......*
Umenikumbusha
Siku hiyo nilijikuta nacheka tu
Mkapa alikuta uchumi mbovu na magu kakuta mbovu
 
Mkwere sio mnafiki. Anaongea ukweli. Nakumbuka miaka yake walikuwa wakipingana kwa hoja bungeni baadae anawaita ikulu anasikiliza hoja za kila upande then wanamaliza. Hakukuwepo kupigana risasi, kutekana au kupotea kwa watu kwa miaka yote 10. Hongeraaa rais Kikwete.

Wewe wa ajabu kweli kulikuwa na kupingana kwa hoja zipi wakati ule bageti zilikuwa zinapitishwa kijairo jairo.
 
Acha unafiki. Ni kweli kipindi cha Kikwete hapakuwa na matatizo hayo? Tuwe wakweli, Kikwete alivurunda kwa namna yake na huyu naye anavurunda kwa namna yake. Lakini tangu enzi ya JKN hadi leo kila mmoja ana dosari zake.

Ni Kikwete aliyesema wafanyakazi waandamane wakione. Kuna watu wamepotea kimyakimya.
Akina nani wamepotea?
 
Mkwere sio mnafiki. Anaongea ukweli. Nakumbuka miaka yake walikuwa wakipingana kwa hoja bungeni baadae anawaita ikulu anasikiliza hoja za kila upande then wanamaliza. Hakukuwepo kupigana risasi, kutekana au kupotea kwa watu kwa miaka yote 10. Hongeraaa rais Kikwete.
Ulimboka ni wakati gani na yule wa Chanel ten vile?
 
Mkwere sio mnafiki. Anaongea ukweli. Nakumbuka miaka yake walikuwa wakipingana kwa hoja bungeni baadae anawaita ikulu anasikiliza hoja za kila upande then wanamaliza. Hakukuwepo kupigana risasi, kutekana au kupotea kwa watu kwa miaka yote 10. Hongeraaa rais Kikwete.
Kisha baada ya kuwapa chai na mikate wanaondoka nayeye anaendelea na ratiba zake.
 
Hapo ndipo ninapoichukia siasa. Mkwele kwa sababu amesema kile unachokipenda ameshakuwa mtu safi.
Mimi nakikumbuka kipindi hicho sana, wakati ambao Ridhiwani alitamba nchi nzima kama mwana wa mfalme. Kila duka jenereta iliunguruma mbele yake, yaliundwa makampuni ya kuiuzia umeme TANESCO. TANESCO ilikuwa sehemu ya kuchuma pesa watu walitajirika, walinunua malori, madawa ya kulevya yaliuzwa kama njugu, walitengeneza pesa kwa njia haramu, hospitali kubwa zote zinatibu vijana waathirika was madawa, hawa watu walikuwa peponi, leo ndio wanaosifiwa. Kama tumefika mahali tunalinganisha na haya anayofanya Magufuli na hao wengine, basi hakutatokea kiongozi atakayetufaa.
Hata Lisu akabahatika kuwa rais, naye sio malaika nina uhakika naye hatachukuwa muda atatukanwa matusi mengi. Ninachokiona ni kwamba wakosoaji wakubwa hawakosoi kwa lengo jema, Bali kutafuta zamu ya kutawala basi. Watanzania tunahitaji kuwa macho na Huyu kiumbe anayeitwa mwanadamu.
 
Mkwere sio mnafiki. Anaongea ukweli. Nakumbuka miaka yake walikuwa wakipingana kwa hoja bungeni baadae anawaita ikulu anasikiliza hoja za kila upande then wanamaliza. Hakukuwepo kupigana risasi, kutekana au kupotea kwa watu kwa miaka yote 10. Hongeraaa rais Kikwete.
Ulimboka je?
 
Back
Top Bottom