Viongozi wa Simba acheni hivyo vikao na wachezaji, zungumzeni na mameneja wao

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,152
7,926
Sijui huu ni utaratibu wa wapi unaotumiwa na Simba kufanya vikao vya kila siku na wachezaji. Hauwezi kujua shida za mchezaji kwa utaratibu huu. Tukisema siasa imezidi pale Simba kuna watu hawatuelewi.

Kila mchezaji wa Simba ana manager wake anayejua kila issue ya mteja wake. Mimi nadhani klabu hasa kwa upande wa management na bodi ianzishe utaratibu mpya wa kuwasiliana na mamanager wa wachezaji kwenye masuala yote yanayohusiana na mchezaji. Kama kuna ahadi za posho ambazo zimechelewa kutekelezwa, mazungumzo yasifanyike kwa mdomo bali kwa maandishi kwenda kwa manager. Kama kuna issue zozote za malimbikizo ya mishahara, taarifa zote zipitie kwa maandishi kwa management ya mchezaji. Kama mchezaji ana malalamiko yoyote ukiacha yale ambayo ameyafikisha kwa benchi la ufundi nae inabidi ayapitishe kwa manager wake atakayefikisha kwa vyombo husika ndani au nje ya klabu. Kama kuna mapungufu au malalamiko ya jumla ya wachezaji mfano hali ya kambi, vifaa duni vya gym, nk. ni jukumu la captain wa timu kufikisha kwa viongozi. Hilo halihitaji vikao.

Wachezaji wa mpira hawana tofauti sana na wasanii wa muziki, hawajui kujieleza hasa kwenye masuala ya fedha, biashara au kisheria. Ukimzingua au akiona mbabaishaji atakufanyia tu vitimbwi kwa jinsi anavyojua yeye.

Wachezaji wakiwa uwanjani wanaonekana wana mawazo na hawana morali ya kucheza kwa sababu wana visirani vyao na hawana jinsi ya kuvifikisha kwa uongozi. Kwanza inaonyesha mazingira ya pale ukijifanya kulalamika tena mbele ya viongozi wote wanaona Aha tumempata mchawi wetu, huyu ndiyo anaongoza mgomo baridi.

Cha mwisho nadhani kuna mgawanyiko kati ya wachezaji wazawa na wageni na pia kuna wachezaji wanaopewa vipaumbele zaidi ya wengine hata katika malipo.
 
Sijui huu ni utaratibu wa wapi unaotumiwa na Simba kufanya vikao vya kila siku na wachezaji. Hauwezi kujua shida za mchezaji kwa utaratibu huu. Tukisema siasa imezidi pale Simba kuna watu hawatuelewi.

Kila mchezaji wa Simba ana manager wake anayejua kila issue ya mteja wake. Mimi nadhani klabu hasa kwa upande wa management na bodi ianzishe utaratibu mpya wa kuwasiliana na mamanager wa wachezaji kwenye masuala yote yanayohusiana na mchezaji. Kama kuna ahadi za posho ambazo zimechelewa kutekelezwa, mazungumzo yasifanyike kwa mdomo bali kwa maandishi kwenda kwa manager. Kama kuna issue zozote za malimbikizo ya mishahara, taarifa zote zipitie kwa maandishi kwa management ya mchezaji. Kama mchezaji ana malalamiko yoyote ukiacha yale ambayo ameyafikisha kwa benchi la ufundi nae inabidi ayapitishe kwa manager wake atakayefikisha kwa vyombo husika ndani au nje ya klabu. Kama kuna mapungufu au malalamiko ya jumla ya wachezaji mfano hali ya kambi, vifaa duni vya gym, nk. ni jukumu la captain wa timu kufikisha kwa viongozi. Hilo halihitaji vikao.

Wachezaji wa mpira hawana tofauti sana na wasanii wa muziki, hawajui kujieleza hasa kwenye masuala ya fedha, biashara au kisheria. Ukimzingua au akiona mbabaishaji atakufanyia tu vitimbwi kwa jinsi anavyojua yeye.

Wachezaji wakiwa uwanjani wanaonekana wana mawazo na hawana morali ya kucheza kwa sababu wana visirani vyao na hawana jinsi ya kuvifikisha kwa uongozi. Kwanza inaonyesha mazingira ya pale ukijifanya kulalamika tena mbele ya viongozi wote wanaona Aha tumempata mchawi wetu, huyu ndiyo anaongoza mgomo baridi.

Cha mwisho nadhani kuna mgawanyiko kati ya wachezaji wazawa na wageni na pia kuna wachezaji wanaopewa vipaumbele zaidi ya wengine hata katika malipo.
Timu gani inaongeaGA na meneja wa mchezaji badala ya mchezaji? Kwenye Sakata la Mbappe na PSG, timu yake iliongea na meneja wake? Man U na Ronaldo, meneja wake alihusishwa?
 
Timu gani inaongeaGA na meneja wa mchezaji badala ya mchezaji? Kwenye Sakata la Mbappe na PSG, timu yake iliongea na meneja wake? Man U na Ronaldo, meneja wake alihusishwa?
Naongelea masuala ya madai ya malipo au changamoto zingine za kawaida ni vyema yakapitia channel za management ya mchezaji ili kumpa mchezaji utulivu wa akili siyo yuko uwanjani anawaza madeni au masuala madogo ya kambini. Kama ni masuala ya performance ya mchezaji, ni wazi hilo ni suala linalotakiwa kufanyiwa kazi na benchi la ufundi, likishindikana huko ndiyo linafika kwa management, sioni mchezaji au kundi la wachezaji wanaingiaje kuhojiwa kwenye vikao vya wakurugenzi wa bodi. Wale wachezaji siyo wanafunzi wa shule ya msingi.

Kwa mifano yako umesahau pia kuwa managers/makocha wa vilabu vya huko Ulaya wana mamlaka na nafasi kubwa kufanya maamuzi kuhusu wachezaji kuliko hawa wa kwetu. Mpaka issue inafika ngazi za juu tayari unakuwa umeona misuguano na maamuzi yamechukuliwa kuanzia ngazi ya mchezaji na kocha wake. Hili hatujaliona likifanyika Simba. Sanasana tunaona wachezaji wenye performance mbovu ndiyo wanapewa muda zaidi uwanjani.

Bila kupitia channel hizi nilizosema ndiyo unakutana na hali kama hiyo ya Rais wa PSG kumtishia Mbappe atasugua benchi, ndiyo yale yale watu wamekuwa wanajiuliza kuhusu Phiri. Pia kumbuka suala la Mbappe ni suala la kimkataba na nina uhakika wanasheria na managers wa Mbappe walikuwepo kwenye vikao.

Kuhusu Ronaldo ni hivyo hivyo pia, unaona issue yake ilikuwa ni ya kinidhamu na unaona channel za uongozi zilivyoohusika. Hivi uliona Ronaldo yuko kikaangoni mbele ya bodi ya Man U bila kuwa na mwanasheria wake au manager?
 
Naongelea masuala ya madai ya malipo au changamoto zingine za kawaida ni vyema yakapitia channel za management ya mchezaji ili kumpa mchezaji utulivu wa akili siyo yuko uwanjani anawaza madeni au masuala madogo ya kambini. Kama ni masuala ya performance ya mchezaji, ni wazi hilo ni suala linalotakiwa kufanyiwa kazi na benchi la ufundi, likishindikana huko ndiyo linafika kwa management, sioni mchezaji au kundi la wachezaji wanaingiaje kuhojiwa kwenye vikao vya wakurugenzi wa bodi. Wale wachezaji siyo wanafunzi wa shule ya msingi.

Kwa mifano yako umesahau pia kuwa managers/makocha wa vilabu vya huko Ulaya wana mamlaka na nafasi kubwa kufanya maamuzi kuhusu wachezaji kuliko hawa wa kwetu. Mpaka issue inafika ngazi za juu tayari unakuwa umeona misuguano na maamuzi yamechukuliwa kuanzia ngazi ya mchezaji na kocha wake. Hili hatujaliona likifanyika Simba.

Bila kupitia channel hizi nilizosema ndiyo unakutana na hali kama hiyo ya Rais wa PSG kumtishia Mbappe atasugua benchi, ndiyo yale yale watu wamekuwa wanajiuliza kuhusu Phiri. Pia kumbuka suala la Mbappe ni suala la kimkataba na nina uhakika wanasheria na managers wa Mbappe walikuwepo kwenye vikao.

Kuhusu Ronaldo ni hivyo hivyo pia, unaona issue yake ilikuwa ni ya kinidhamu na unaona channel za uongozi zilivyoohusika. Hivi uliona Ronaldo yuko kikaangoni mbele ya bodi ya Man U bila kuwa na mwanasheria wake au manager?
Dah! Maelezo yooooote hujatoa mfano hata mmoja. Hakika wewe ni Great Thinker!!!!
 
Dah! Maelezo yooooote hujatoa mfano hata mmoja. Hakika wewe ni Great Thinker!!!!
Umetumia mifano ambayo haiendani na kile kinachoendelea Simba. Kwa kuwa umeenda kutumia mifano ya Ulaya, tupe mifano inayoendana, mfano tuonyeshe picha ya wachezaji wamewekwa kikaanganoni na bodi ya wakurugenzi?
 
Wachezaji hawajalipwa Posho inavyoonekana ndio maana vikao haviishi na Wachezaji wanatishiwa atakaeongea tu anafukuzwa kazi ndio maana Mangungu kashika bomba hataki kuachia ngazi...
 
Back
Top Bottom