Viongozi wa shirikisho la soka Tanzania hivi mbona mnapenda kujiabisha waziwazi kila mmoja ajue mapungufu yenu?

vibertz

JF-Expert Member
Mar 15, 2022
1,468
2,668
Kuna matukio mawili yameongozana yamedhihirisha ni wazi TFF ina watu wasiokuwa na uadilifu, wasiokuwa na maono na hawana upeo wa kufikiria, kuchambua vitu kwa kina.

Tukio la kwanza ilikuwa ni kitendo cha kupeleka fainali ya kombe la CRDB federation cup Manyara. Tukio la pili ni kitendo cha kuhamishia Zanzibar badala ya Manyara.

Tukio la tatu ni kitendo cha Simba kuamisha uwanja dhidi ya KMC na nyie TFF na bodi ya ligi mkalibariki.

Hiyo sio haki, timu za mpira wa miguu ni taasisi ambazo zinakuwa na mipango na mikakati yake kulingana na ratiba iliyokuwepo. Kitendo KMC kujulishwa kuwa mechi atacheza mechi na Simba Dar kwenye uwanja wa Isamuhyo, inawafanya wapange bajeti zao na ratiba zao kulingana na taarifa waliyoipata.

Ghafla timu iliyoomba uwanja wa Isamuhyo inabadili kwenda Arusha, ni kutowatendea haki KMC. Kuna gharama za safari hapo inajitokeza kitu ambacho KMC hawakuliwaza wala kujiandaa nayo. Simba wao wamejiamulia kwavile inauwezo wa kupanda ndege na pia wamesha organize mambo yao, je vipi huyu mpinzani wake? Au kwavile ni timu ndogo?

KMC hutumia usafiri wa bus kwenda mkoani, kucheza mechi hapo kuna muda kwaajili ya kusafiri, kuna muda kwaajili ya kupumzika kutokana na uchovu wa safari, na kuna muda kwa ajili ya kujiandaa na mchezo je hilo limefikiriwa kwa KMC? Au ndio KMC wanafanyiwa hujuma ili apoteze mechi au ashindwe kusafiri ili Simba ipewe point tatu na magoli

3. Hii ni hujuma ya wazi kwa KMC ambao wanagombea nafasi ya 4 dhidi ya Coastal union na pia upendeleo wa wazi kwa Simba ili washinde mechi kiurahisi. Kinachofanyika kwa KMC sio haki ni uonevu huo.
 
kama walitoa sababu zenye mashiko kwanini wasiruhusiwe? Kama kmc hajaafiki si aseme..! wewe umekuwa wasemaji wao what if simba ka top up kmc what will you gonna say about it?

By the way Zanzibar ipo ndani ya Tanzania au nje ya Tanzania?

Uwanja wa manyara mbaya na mdogo,mechi hawataki kuichezesha Dar ili kutoa malalamiko ya fulani yupo nyumbani nyie pigeni kelele lakini ngoma itachezewa Zanzibar.
 
Kuna matukio mawili yameongozana yamedhihirisha ni wazi TFF ina watu wasiokuwa na uadilifu, wasiokuwa na maono na hawana upeo wa kufikiria, kuchambua vitu kwa kina...
Bila kutolewa Wales karia mambo haytaenda.Karia ni simba damu damu sasa unategemea nini hapo!
 
Ila uongozi wa TFF ni wa ovyo kabisa, zinapenda kuzikandamiza timu ndogo kama vile hazina haki
 
Kuna matukio mawili yameongozana yamedhihirisha ni wazi TFF ina watu wasiokuwa na uadilifu, wasiokuwa na maono na hawana upeo wa kufikiria, kuchambua vitu kwa kina.

Tukio la kwanza ilikuwa ni kitendo cha kupeleka fainali ya kombe la CRDB federation cup Manyara. Tukio la pili ni kitendo cha kuhamishia Zanzibar badala ya Manyara.

Tukio la tatu ni kitendo cha Simba kuamisha uwanja dhidi ya KMC na nyie TFF na bodi ya ligi mkalibariki.

Hiyo sio haki, timu za mpira wa miguu ni taasisi ambazo zinakuwa na mipango na mikakati yake kulingana na ratiba iliyokuwepo. Kitendo KMC kujulishwa kuwa mechi atacheza mechi na Simba Dar kwenye uwanja wa Isamuhyo, inawafanya wapange bajeti zao na ratiba zao kulingana na taarifa waliyoipata.

Ghafla timu iliyoomba uwanja wa Isamuhyo inabadili kwenda Arusha, ni kutowatendea haki KMC. Kuna gharama za safari hapo inajitokeza kitu ambacho KMC hawakuliwaza wala kujiandaa nayo. Simba wao wamejiamulia kwavile inauwezo wa kupanda ndege na pia wamesha organize mambo yao, je vipi huyu mpinzani wake? Au kwavile ni timu ndogo?

KMC hutumia usafiri wa bus kwenda mkoani, kucheza mechi hapo kuna muda kwaajili ya kusafiri, kuna muda kwaajili ya kupumzika kutokana na uchovu wa safari, na kuna muda kwa ajili ya kujiandaa na mchezo je hilo limefikiriwa kwa KMC? Au ndio KMC wanafanyiwa hujuma ili apoteze mechi au ashindwe kusafiri ili Simba ipewe point tatu na magoli

3. Hii ni hujuma ya wazi kwa KMC ambao wanagombea nafasi ya 4 dhidi ya Coastal union na pia upendeleo wa wazi kwa Simba ili washinde mechi kiurahisi. Kinachofanyika kwa KMC sio haki ni uonevu huo.
Hayo yote sio mapya, ni kawaida kabisa. Leta lingine tulipime
 
Tukio la tatu ni kitendo cha Simba kuamisha uwanja dhidi ya KMC na nyie TFF na bodi ya ligi mkalibariki. Hiyo sio haki, timu za mpira wa miguu ni taasisi ambazo zinakuwa na mipango na mikakati yake kulingana na ratiba iliyokuwepo. Kitendo KMC kujulishwa kuwa mechi atacheza mechi na Simba Dar kwenye uwanja wa Isamuhyo, inawafanya wapange bajeti zao na ratiba zao kulingana na taarifa waliyoipata. Ghafla timu iliyoomba uwanja wa Isamuhyo inabadili kwenda Arusha, ni kutowatendea haki KMC. Kuna gharama za safari hapo inajitokeza kitu ambacho KMC hawakuliwaza wala kujiandaa nayo. Simba wao wamejiamulia kwavile inauwezo wa kupanda ndege na pia wamesha organize mambo yao, je vipi huyu mpinzani wake? Au kwavile ni timu ndogo? KMC hutumia usafiri wa bus kwenda mkoani, kucheza mechi hapo kuna muda kwaajili ya kusafiri, kuna muda kwaajili ya kupumzika kutokana na uchovu wa safari, na kuna muda kwa ajili ya kujiandaa na mchezo je hilo limefikiriwa kwa KMC? Au ndio KMC wanafanyiwa hujuma ili apoteze mechi au ashindwe kusafiri ili Simba ipewe point tatu na magoli. Hii ni hujuma ya wazi kwa KMC ambao wanagombea nafasi ya 4 dhidi ya Coastal union na pia upendeleo wa wazi kwa Simba ili washinde mechi kiurahisi. Kinachofanyika kwa KMC sio haki ni uonevu huo.
Umesema kuna matukio matatu. lakini hili la KMC umeliandikia gazeti. Lakini kuna swali moja, kwani KMC wenyewe wenye kutakiwa kucheza mechi, wamelalamika wapi? Hebu tuonyeshe document ambayo KMC imelalamikia kuhamishwa uwanja.


 
Umesema kuna matukio matatu. lakini hili la KMC umeliandikia gazeti. Lakini kuna swali moja, kwani KMC wenyewe wenye kutakiwa kucheza mechi, wamelalamika wapi? Hebu tuonyeshe document ambayo KMC imelalamikia kuhamishwa uwanja.


View attachment 2997891
Nimejaribu kusikiliza haya mahojiano ila kuna kitu kimeshindwa kuwekwa wazi kwa wasikilizaji. Na mwandishi wa habari hajui jinsi ya kuuliza maswali. Anasema kuwa Simba haikuchelewa kuleta taarifa. Na wao bodi wakawasiliana na wadhamini, KMC, na mashabiki je kwanini ameshindwa kutaja specific time kuwa tarehe fulani ilitolewa hiyo taarifa?

La pili sijui kanuni inazungumzia habari ya masaa 72 au ni swala la siku 7 maana huyu msemaji wa bodi ya ligi yeye anasema kuwa taarifa ilitolewa zaidi ya masaa 72 inakuaje ni masaa 72 wakati nimeona humu wakisema kanuni ya ubadilishwaji wa uwanja inatakiwa kutolewa siku 7 kabla.
 
... inakuaje ni masaa 72 wakati nimeona humu wakisema kanuni ya ubadilishwaji wa uwanja inatakiwa kutolewa siku 7 kabla.
Nakunukuu: "Nimeona humu wakisema..." Mwisho wa kukunukuu.

Tatizo lako lilianzia hapo. Ulikurupuka kuanzisha uzi kwa kuona comments za watu wasiohusika wala kuzijua kanuni za uendeshaji wa ligi yetu. Ndio maana umebaki unalalamika peke yako, wakati KMC hawajawahi kulalamika na wameshasafiri kwenda kucheza mechi. Badala yake nilichoona unaanza kutafuta ufafanuzi na kujaribu kuwahamishia lawama 'waliomo humu'. Hujachelewa lakini, unaweza tu kumuomba Mod afute uzi huu kimya kimya maana mtu mzima unavuliwa nguo katikati ya soko. Endelea kuona humu. Mambo mengine yanachangiwa na uduni wa elimu
 
Back
Top Bottom