Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 915
- 4,270
Kwa mujibu wa vitabu vitakatifu hakuna ondoleo la dhambi linalotokana na kiongozi wa dini; vitabu vitakatifu vyote vimekabidhi mamlaka yakuondoa dhambi kwa Mungu siyo kwa wanadamu.
Kwanini watanzania tumekuwa wepesi kuamini maaskofu na masheikh wanaweza kutuondolea dhambi? Hawa ni viongozi wa taasisi wanapiga kampeni kuchukua madaraka kwenye taasisi zao; hawa ni binadamu kama sisi ila wao wamechagua ofisi zao ziwe nyumba za ibada lakini haina maana kwamba wao ni watakatifu.
Tukilitambua ilo tutarejea kwenye dini ya kweli ambayo ni kutenda yaliyo mema. Ukisimama na wema hata usipoenda nyumba ya ibada wanaokuzunguka watabarikiwa na maisha yako na hii ndiyo ibada ya kweli.
Kuna viongozi wa dini ambao wanawaabudu wanasiasa kuliko Mungu; wapo tayari kutamka adharani kwamba mwanasiasa anayekatili watu ni mtu mwema. Huyu kiongozi anawezaje kuondolea dhambi? Anawezaje kupeleka maombi yako kwa Mungu?
Viongozi wa dini ambao wanaona wanachofanyiwa Wamasai Arusha ni jambo wanalostahili si viongozi wa dini bali ni wachumia familia zao.
Kwanini watanzania tumekuwa wepesi kuamini maaskofu na masheikh wanaweza kutuondolea dhambi? Hawa ni viongozi wa taasisi wanapiga kampeni kuchukua madaraka kwenye taasisi zao; hawa ni binadamu kama sisi ila wao wamechagua ofisi zao ziwe nyumba za ibada lakini haina maana kwamba wao ni watakatifu.
Tukilitambua ilo tutarejea kwenye dini ya kweli ambayo ni kutenda yaliyo mema. Ukisimama na wema hata usipoenda nyumba ya ibada wanaokuzunguka watabarikiwa na maisha yako na hii ndiyo ibada ya kweli.
Kuna viongozi wa dini ambao wanawaabudu wanasiasa kuliko Mungu; wapo tayari kutamka adharani kwamba mwanasiasa anayekatili watu ni mtu mwema. Huyu kiongozi anawezaje kuondolea dhambi? Anawezaje kupeleka maombi yako kwa Mungu?
Viongozi wa dini ambao wanaona wanachofanyiwa Wamasai Arusha ni jambo wanalostahili si viongozi wa dini bali ni wachumia familia zao.