Viongozi wa dini waumini wakishindwa toa sadaka na zaka msiwalaumu

wankuru nyankuru

JF-Expert Member
Feb 11, 2019
491
763
Mimi ni muumini wa hili kanisa usharika wa Mbezi Louis, tokea nianze kusali nikiwa sunday school pale ni mwaka wa 18 sasa, katika vitu nlivyogundua ni kwamba haya makanisa hasa Kkkt yanaendeshwa kupitia sadaka za waumini yaani waumini wakisema wasitoe sadaka ndani ya miezi 3 tu hali ya viongozi ipo taabani

Usiposhiriki misa au kutoa Sadaka unaonekana mkosaji, ibada nzima ni michango tu kikapu kuanzia mwanzo hadi mwisho watu wanakamuliwa ni pesa kwenda mbele ila sijui kama wanajua hizo pesa zinapotokea ni wapi

Linapokuja swala la uchumi tunatakiwa tuwe kitu kimoja, kesho kama taifa tukiingia mikataba mibovu alafu kesho tukaja kuivunja nchi ikiingia kwenye madeni mazito haumii mtu mwingine tunaumia wote ndio haya matozo na kodi kubwa walizoweka huu ni mwanzo tu picha linakuja Viongozi wetu wa KKKT ikifika mahali mkaambiwa kuwa hatuna pesa sababu uchumi umeharibika muwe wasikivu maana ibada zenu ni kuomba pesa mwanzo mwisho, hajawajenga wachungaji na wainjilisti kujitegemea kiuchumi mmewajenga kuwakamua waumini kwenye kapu la sadaka.

Askofu Shoo unasema unabariki uwekezaji ni uwekezaji gani huo wa kijinga namna hii, unampa mtu Bandari kwa mkataba wa kudumu huo ni uwekezaji au uuzaji wa Bandari? Kesho akiingia kiongozi type ya Magufuli akauvunja mwishowe DP world wataenda mahakamani halafu tukidaiwa mabilioni ya pesa wanatuwekea Tozo na kodi kubwa tulipe wananchi, wananchi tukishapigika tukija makanisani mikono mitupu muwe waelewa maana kodi kubwa ni chanzo cha kufanya watu wafilisike.

Niwapongeze Roman kwa kuwa wakweli maana mmeona mbali, waumini wenu mnajua kabisa uchumi wao ukiyumba utaleta shida hadi kwenu ila uchumi ukinyooka hata kwa kanisa ni faida kubwa.
 
Ni kujipendekeza kwa viongozi wetu wa kiimani kwa mfano hata hao Masheikh walioamua kuwa ndiyo mawaziri na makatibu wa serikali kwa kuwajibu wale wanaoenda against Samia utagundua ni kusukumwa na njaa tu

Japo huyo amejifanya kuweka mabano kwa kusema tunakubali uwekezaji huku hajafafanua uwekezaji wa namna gani ilibidi hapo hapo agonge msumari kwamba ”lakini uwekezaji wenye tija kwa nchi yetu” hapo hata huyo ushungi angetoka hapo jasho likimvuja.
 
Nani kakwambia sadaka yako muhimu?

Mimi nimejiunga kkkt na nitatoa sadaka nyingi mara 100 ya hizo unazotoa wewe
 
Mimi ni muumini wa hili kanisa usharika wa Mbezi Louis, tokea nianze kusali nikiwa sunday school pale ni mwaka wa 18 sasa, katika vitu nlivyogundua ni kwamba haya makanisa hasa Kkkt yanaendeshwa kupitia sadaka za waumini yaani waumini wakisema wasitoe sadaka ndani ya miezi 3 tu hali ya viongozi ipo taabani

Usiposhiriki misa au kutoa Sadaka unaonekana mkosaji, ibada nzima ni michango tu kikapu kuanzia mwanzo hadi mwisho watu wanakamuliwa ni pesa kwenda mbele ila sijui kama wanajua hizo pesa zinapotokea ni wapi

Linapokuja swala la uchumi tunatakiwa tuwe kitu kimoja, kesho kama taifa tukiingia mikataba mibovu alafu kesho tukaja kuivunja nchi ikiingia kwenye madeni mazito haumii mtu mwingine tunaumia wote ndio haya matozo na kodi kubwa walizoweka huu ni mwanzo tu picha linakuja Viongozi wetu wa KKKT ikifika mahali mkaambiwa kuwa hatuna pesa sababu uchumi umeharibika muwe wasikivu maana ibada zenu ni kuomba pesa mwanzo mwisho, hajawajenga wachungaji na wainjilisti kujitegemea kiuchumi mmewajenga kuwakamua waumini kwenye kapu la sadaka.

Askofu Shoo unasema unabariki uwekezaji ni uwekezaji gani huo wa kijinga namna hii, unampa mtu Bandari kwa mkataba wa kudumu huo ni uwekezaji au uuzaji wa Bandari? Kesho akiingia kiongozi type ya Magufuli akauvunja mwishowe DP world wataenda mahakamani halafu tukidaiwa mabilioni ya pesa wanatuwekea Tozo na kodi kubwa tulipe wananchi, wananchi tukishapigika tukija makanisani mikono mitupu muwe waelewa maana kodi kubwa ni chanzo cha kufanya watu wafilisike.

Niwapongeze Roman kwa kuwa wakweli maana mmeona mbali, waumini wenu mnajua kabisa uchumi wao ukiyumba utaleta shida hadi kwenu ila uchumi ukinyooka hata kwa kanisa ni faida kubwa.
Namsubiri mstaafu ampinge Shao kuwa viongozi wa dini wasichanganye siasa na dini, Shao anarudishwa fadhila za kijana wake kufutiwa kesi ya ugaidi.
 
Tatizo kubwa kwa nchi yetu ni pale tulipoacha kumtegemea zaidi Mungu katika kutupatia akili nzuri ya kuendesha miradi yetu na kuanza kuwategemea zaidi wawekezaji!
As if hao wawekezaji wao ni miungu!
 
Tatizo kubwa kwa nchi yetu ni pale tulipoacha kumtegemea zaidi Mungu katika kutupatia akili nzuri ya kuendesha miradi yetu na kuanza kuwategemea zaidi wawekezaji!
As if hao wawekezaji wao ni miungu!
Shida ni uwezo wa kifikra na utendaji mkuu, maana muda mwengine unakuta wafanya kufuru ndo wawekezaji sasa alafu wapo nondo vibaya mno
 
Viongozi wa KKKT wametumia busara kubwa sana kumwambia SSH kuwa LI mkataba lake halifaii!
Ila wasiokuwa na akili hawaelewi!
Hongera sana Askofu Dr. Shoo
 
Shida ni uwezo wa kifikra na utendaji mkuu, maana muda mwengine unakuta wafanya kufuru ndo wawekezaji sasa alafu wapo nondo vibaya mno
Shida ni ccm. Tulivyoingia mfumo wa vyama vingi ilitakiwa ccm yenyewe ife. Vije vyama vipya vyenye ushindani sawa na katiba mpya isiyopendelea mfumo wa chama kimoja.
 
Back
Top Bottom