DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Watanzania wamekumbushwa kuendelea kuilinda na kudumisha Amani iliyopo hapa Nchini hasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba mwaka 2025.
Hayo yameelezwa kati Dua Maalumu iliyoandaliwa na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Mtaa wa Mtepwezi kata ya Likonde Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani Mkoani Mtwara kwa lengo la kuwaombea Dua Ndugu jamaa na marafiki waliofariki dunia sambamba na kuliombea Taifa la Tanzania kufanya uchaguzi mkuu kwa njia ya Amani,
ndipo Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Jamaldin Chamwi akatoa neno kwa Watanzania, huku kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara SSP Osward Ntelanya akisisitiza kuilinda amani hiyo.
Nao Baadhi ya Waumini Wa Dini hiyo akiwemo Halima Salumu, Saidi Mpwago pamoja na Hashimu Salumu wametaka Watanzania kushiriki Uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu na kuwachagua viongozi Bora watakaowaletea maendeleo.
Chanzo: Mtwara Digital
Hayo yameelezwa kati Dua Maalumu iliyoandaliwa na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Mtaa wa Mtepwezi kata ya Likonde Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani Mkoani Mtwara kwa lengo la kuwaombea Dua Ndugu jamaa na marafiki waliofariki dunia sambamba na kuliombea Taifa la Tanzania kufanya uchaguzi mkuu kwa njia ya Amani,
ndipo Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Jamaldin Chamwi akatoa neno kwa Watanzania, huku kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara SSP Osward Ntelanya akisisitiza kuilinda amani hiyo.
Nao Baadhi ya Waumini Wa Dini hiyo akiwemo Halima Salumu, Saidi Mpwago pamoja na Hashimu Salumu wametaka Watanzania kushiriki Uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu na kuwachagua viongozi Bora watakaowaletea maendeleo.
Chanzo: Mtwara Digital