YEHODAYA
JF-Expert Member
- Aug 9, 2015
- 36,908
- 51,904
Baadhi ya viongozi wa dini wameanza kujitumbukiza kwenye kusikiliza makutano wanasema nini yaani watu wengi wanasema nini ili kutafuta sifa kwa makutano.Hii kitu imepelekea wao kutelekeza wito wa Mungu walioitiwa kwenye kazi zao za kichungaji na kiaskofu nk
Ponsio Pilato alikuwa msomi na mwanasaheria na mwenye vitabu vya sheria lakini Yesu alipoletwa na makutano akajaa mihemko akatelekeza vitabu vyake vya sheria akawauliza makutano mnataka nimfanyie nini huyu Yesu makutano wakapiga kelele asulubishwe asulubishwe! Akaamua asublubishwe bila hata ku quote kifungu chochote cha kitabu chake cha sheria.
Sasa kuna ma Ponsio Pilato wengi ambao wamegeuka kazi yao kuongelea makutano wanataka nini na kuacha kuongelea Mungu anataka nini.
Wachungaji na maaskofu Yesu aliwatuma akisema enendeni ulimwenguni kote mkaihubiri injili.Baadhi yao wamegeuka wasikiliza makutano wanataka nini wamegeuka wahubiri katiba mpya na tume huru za uchaguzi ili kutafuta sifa za makutano na kuitelekeza Injili waliyotumwa na Yesu. Wanasulubisha Yesu.
Niseme wazi Yesu alikuwa yuko sahihi kusema ufalme wangu si wa ulimwengu huu! Hii trend ya wachungaji na maaskofu kutafuta ufalme wa ulimwengu huu iwe kutaka kukubalika kwa makutano, kugombea vyeo vya kisiasa na kuwa upande wa vyama fulani kiwe tawala au upinzani ni kumsulubisha Yesu.
Viongozi wa kidini wana waumini wa vyama vyote na wasio na vyama ni vyema wakabaki kwenye wito wao tu na nashauri hata wasiwe na kadi ya chama chochote cha siasa na mwegemeo wa chama chochote.
Wabaki tu watangaza injili ya Kristo ya tubuni na kuiamini injili .Ulaya viongozi wa dini walijitia wapenda sifa za makutano kwa kushabikia siasa makanisa Ulaya yamekufa.
Ponsio Pilato alikuwa msomi na mwanasaheria na mwenye vitabu vya sheria lakini Yesu alipoletwa na makutano akajaa mihemko akatelekeza vitabu vyake vya sheria akawauliza makutano mnataka nimfanyie nini huyu Yesu makutano wakapiga kelele asulubishwe asulubishwe! Akaamua asublubishwe bila hata ku quote kifungu chochote cha kitabu chake cha sheria.
Sasa kuna ma Ponsio Pilato wengi ambao wamegeuka kazi yao kuongelea makutano wanataka nini na kuacha kuongelea Mungu anataka nini.
Wachungaji na maaskofu Yesu aliwatuma akisema enendeni ulimwenguni kote mkaihubiri injili.Baadhi yao wamegeuka wasikiliza makutano wanataka nini wamegeuka wahubiri katiba mpya na tume huru za uchaguzi ili kutafuta sifa za makutano na kuitelekeza Injili waliyotumwa na Yesu. Wanasulubisha Yesu.
Niseme wazi Yesu alikuwa yuko sahihi kusema ufalme wangu si wa ulimwengu huu! Hii trend ya wachungaji na maaskofu kutafuta ufalme wa ulimwengu huu iwe kutaka kukubalika kwa makutano, kugombea vyeo vya kisiasa na kuwa upande wa vyama fulani kiwe tawala au upinzani ni kumsulubisha Yesu.
Viongozi wa kidini wana waumini wa vyama vyote na wasio na vyama ni vyema wakabaki kwenye wito wao tu na nashauri hata wasiwe na kadi ya chama chochote cha siasa na mwegemeo wa chama chochote.
Wabaki tu watangaza injili ya Kristo ya tubuni na kuiamini injili .Ulaya viongozi wa dini walijitia wapenda sifa za makutano kwa kushabikia siasa makanisa Ulaya yamekufa.