Viongozi wa CHADEMA kutokumtambua Rais ni Kosa?

- Mkuu heshima sana, lakini huu ni mtizamo wako tu na sio kwamba ni standard ya elimu ya uraia Tanzania kama ulivyobainisha mwanzoni, umeandika maneno mengi mazuri ya kimapinduzi lakini tatizo ni ushahidi kwamba Dr. slaa ndiye aliyeshinda urais tungependa kuuona upo wapi? Kama watu kama wewe mnao tuwekeeni hapa tuuchambue tuone ukweli ulipo maana hapa si unajua ni uwanja wa werevu. Halafu umeharibu sana kumuingiza Mwalimu on this kwa sababu at the ehart hapa ni sheria za chama kimoja kutumuika kwenye system ya vyama vingi, na pia Rais wa sasa hakuhusika na kuiba kura unless unao ushahidi kwamba aliiba na kuwaamuru NEC pia kuiba, au aliiba nao!

- Wagiriki hawakusema Demokrasia ni lazima kushinda Wapinzani tu, wakishindwa basi sio Demokrasia na sidhani kama walisema kwamba Wapinzani wakitoka kwenye kikao cha bunge basi chama chenye majority kinakuwa hakina mandate ya wananchi kuongoza taifa. Cha muhimu ni kwamba CCM kama chama cha siasa wana kila sababu ya kusikiliza kilio cha Chadema na kutafakari wanacholilia ni nini hasa, maana huwezi kuwa-ignore wananchi Millioni 2.2 waliompigia kura za U-Rais Dr. Slaa as of official matokeo yaliyopo tayari, otherwise ni muhimu sana tukaonyeshwa ushaidi mzito kwamba Dr. Slaa ndiye aliyeshinda huu uchaguzi. Hiii protest ni simply political protest na ni kawaida katika very Demokraisa ya Wagirki unayoisema, kwa sababu hata CCM pia inaweza kutoka nje wabunge wa Chadema wanapochangia hoja inaweza kufanyika both ways, lakini muhimu ni isitugawe taifa kwamba kwa sababu chadema wanasusia Rais, basi wana haki sana na hili taifa kuliko wasiosusia yatakwua ni mawazo mufilisi sana!

William.


Ninachosema ni kuwa kukiuka utashi wa Watanzania ni kukiuka maadili ya Kitanzania kwani tunaamini katika na kujenga utamaduni wenye maadili ya kuheshimu matakwa ya watu. Sasa Kikwete na CCM wanataka tuamini katika utamaduni wa Stalin kuwa mtu wa maana si mpiga kura bali muhesabu kura. Na kwa kweli wamekwenda mbele zaidi na kuamini ule wa Kibaki na Kivuitu kuwa mtu wa maana katika uchaguzi si mpiga kura, msimamizi wala muhesabu kura bali mtangaza matokeo. Hii ni hatari. Ushahidi ni wazi kwamba matokeo yaliyotangazwa na Tume ni tofauti na yale yaliyopatkana katika vituo.

Nimemtumia Mwalimu kwani msemo ule wa mwaka 1962 ni wa muhimu kuwa katika nchi yetu wananchi wana haki ya kumpinga kiongozi yoyote yule anayekiuka maadili na sheria za nchi. Upingaji huu hautaishia kwa Kikwete bali kwa kiongozi yeyote yule awe wa Chadema, CUF, TLP, UDP na wengine wote. Ni kwamba katika kulinda maslahi, heshima ya nchi wananchi wana haki na jukumu la kuwapinga na kuwakosoa viongozi wao. Nasimama katika maelezo yangu nadhani yanahitaji kutiliwa maanani na wote wenye kuitakia nchi yetu mema. Ni lazima tuhakikishe kwamba chaguzi zetu si tu zinakuwa ni huru na haki bali pia zinaonekana kuwa ni huru na haki kwani taswira hushinda uhalisia (perception trumps reality). Na kwa bahati mbaya katika hili ukweli ni kuwa muonekano na ukweli vilifanana kwamba uchaguzi umechakachuliwa.
 
vipaombele vya JK

1.umoja amani na usalama
2.uchumi kukuza,
3.kuongeza jitihada za kuwezesha kiuchumi.
4.sekta binafsi nchini
5. kufanya nchi kuwa lango kwa kuboresha miundo mbuni
6. mariasili
7.kuboresha ukusanyaji kodi
8.elimu
9. huduma za kijamiii
10. kuimalisha utawala bora
11.kuimalisha uhusiano wa kimataifa
12. kuhifadhi mazingira
13. kulinda mafanikio

Ni too General kiasi kwamba kumbana itakuwa ngumu , kwani haujui ni nini hasa anazungumzia kwenye kila kipengere. Ni ujanja ujanja tuu unatumika.
 
Hao CHADEMA hovyo sana! Kama kweli hawamtambui basi sharti wasiingie bungeni na wasichukue ile hela ya posho wala pesaingine manake itakuwa kama wanachukua kutoka serikali wasioitambua!! Yule kiongozi wa upinzani bunge lililopita aliwaambia hivyo kwani wao CUF hawaku ingia baraza la wakilishi mpaka muafaka ulivyofikiwandipo wakarudi barazani na kuanza kuchukua fweza.

Namna gani hii!!!!????
Bunge ni nguzo tofauti na taasisi ya Uraisi ndio maana chaguzi za nguzo hizi 2 zinafuata vipengele tofauti vya katiba yetu.likewise kuna watu wanaomtambua Rais bila kutambua wabunge kadha wa kadha(mifano hai tazama kura za kupinga matokeo ya ubunge)

Just because YOU haven't been to Antarctica it does not mean the place does not exist
 
Yaani mara nyingine tunataka kusikia tunachotaka kusikia tu. Mtu anakwambia "karibu" wewe unasema kakwambia "toka hapa"

Alichosema Kikwete, kwa mujibu wako hapo juu, na tafsiri yako, ni vitu viwili tofauti.

Kikwete anawaambia tu kwamba yeye ndiye de facto na de jure president, na watahitaji ushirikiano wa serikali yake. Hizi protests zao haziwezi kumu unseat legally. Sijaona tishio hapo, ana knock some common sense into their quixotic zeal tu.

Hata kama wameibiwa kura kweli, wanachofanya ni utoto, wana half step. Kama wameibiwa waitishe maandamano nchi nzima ya wanachama na supporters wao, hata kama hawana legal means. Waitishe muswada wa dharura bungeni kubadilisha sheria za uchaguzi kabla ya kitu kingine chochote, waitishe mkutano wa katiba kwa mgomo wa nchi nzima, hapo nitawaona wako serious.

Hizi habari za kutoka bungeni nusunusu, mara wanapigia kura chaguo la Kikwete PM, mara wanasusia kusikiliza hotuba yake, nawaona wanacheza.
Nani kampigia kura chaguo la Kikwete? Labda CUF..
Halafu unataka Chadema waandamane ili mseme wanaanzisha fujo sio?
Chadema ni chama chenye watu makini sana kwa taarifa yako , walichofanya pale ni zaidi ya maandamano ya watu milioni nne, tena mbele ya wahisani na nchi nzima imeona. Wakiandamana mnaweza wahonga hata waandishi wasindike maandamano yao.
Wamepiga Pentagon penyewe na hile ndio ilitakiwa.
Kuchakachua lazima kuwanyime raha hata kama wakijifariji vipi kuwa hawajali.
 
- Mkuu heshima sana, lakini huu ni mtizamo wako tu na sio kwamba ni standard ya elimu ya uraia Tanzania kama ulivyobainisha mwanzoni, umeandika maneno mengi mazuri ya kimapinduzi lakini tatizo ni ushahidi kwamba Dr. slaa ndiye aliyeshinda urais tungependa kuuona upo wapi? Kama watu kama wewe mnao tuwekeeni hapa tuuchambue tuone ukweli ulipo maana hapa si unajua ni uwanja wa werevu. Halafu umeharibu sana kumuingiza Mwalimu on this kwa sababu at the ehart hapa ni sheria za chama kimoja kutumuika kwenye system ya vyama vingi, na pia Rais wa sasa hakuhusika na kuiba kura unless unao ushahidi kwamba aliiba na kuwaamuru NEC pia kuiba, au aliiba nao!

- Wagiriki hawakusema Demokrasia ni lazima kushinda Wapinzani tu, wakishindwa basi sio Demokrasia na sidhani kama walisema kwamba Wapinzani wakitoka kwenye kikao cha bunge basi chama chenye majority kinakuwa hakina mandate ya wananchi kuongoza taifa. Cha muhimu ni kwamba CCM kama chama cha siasa wana kila sababu ya kusikiliza kilio cha Chadema na kutafakari wanacholilia ni nini hasa, maana huwezi kuwa-ignore wananchi Millioni 2.2 waliompigia kura za U-Rais Dr. Slaa as of official matokeo yaliyopo tayari, otherwise ni muhimu sana tukaonyeshwa ushaidi mzito kwamba Dr. Slaa ndiye aliyeshinda huu uchaguzi. Hiii protest ni simply political protest na ni kawaida katika very Demokraisa ya Wagirki unayoisema, kwa sababu hata CCM pia inaweza kutoka nje wabunge wa Chadema wanapochangia hoja inaweza kufanyika both ways, lakini muhimu ni isitugawe taifa kwamba kwa sababu chadema wanasusia Rais, basi wana haki sana na hili taifa kuliko wasiosusia yatakwua ni mawazo mufilisi sana!

William.

Slaa hakudai kuwa yeye ndio angeshinda uraisi..,alidai kuwa KURA alizopata kikwete zimechakachuliwa...,na wao kama chadema wako tayari kukubali ushindi wa kikwete uwe wa asilimia 40 au asilimia 90,as long as hakuna mapungufu makubwa(naamini uliyaona hayo mapungufu,hamna haja ya kuyarudia).

wabunge wa CCM hawana uhusiano wa moja kwa moja na kikwete,wao walichaguliwa kwa kura tofauti,wale ambao walichakachua,kesi zao ziko mahakamani..,kikwete hawezi pelekwa huko kwa sababu ya katoba yetu kutoruhusu.

sitegemei kuona wabunge wakiprotest wabunge wenzao maana hayawahusu..,na kuna platform ya malalamiko ya kibunge(mahakama)
 
Ninachosema ni kuwa kukiuka utashi wa Watanzania ni kukiuka maadili ya Kitanzania kwani tunaamini katika na kujenga utamaduni wenye maadili ya kuheshimu matakwa ya watu. Sasa Kikwete na CCM wanataka tuamini katika utamaduni wa Stalin kuwa mtu wa maana si mpiga kura bali muhesabu kura. Na kwa kweli wamekwenda mbele zaidi na kuamini ule wa Kibaki na Kivuitu kuwa mtu wa maana katika uchaguzi si mpiga kura, msimamizi wala muhesabu kura bali mtangaza matokeo. Hii ni hatari. Ushahidi ni wazi kwamba matokeo yaliyotangazwa na Tume ni tofauti na yale yaliyopatkana katika vituo.

Nimemtumia Mwalimu kwani msemo ule wa mwaka 1962 ni wa muhimu kuwa katika nchi yetu wananchi wana haki ya kumpinga kiongozi yoyote yule anayekiuka maadili na sheria za nchi. Upingaji huu hautaishia kwa Kikwete bali kwa kiongozi yeyote yule awe wa Chadema, CUF, TLP, UDP na wengine wote. Ni kwamba katika kulinda maslahi, heshima ya nchi wananchi wana haki na jukumu la kuwapinga na kuwakosoa viongozi wao. Nasimama katika maelezo yangu nadhani yanahitaji kutiliwa maanani na wote wenye kuitakia nchi yetu mema. Ni lazima tuhakikishe kwamba chaguzi zetu si tu zinakuwa ni huru na haki bali pia zinaonekana kuwa ni huru na haki kwani taswira hushinda uhalisia (perception trumps reality). Na kwa bahati mbaya katika hili ukweli ni kuwa muonekano na ukweli vilifanana kwamba uchaguzi umechakachuliwa.


- Mkuu heshima sana, haya again ni maoni yako binafsi ambayo ni haki yako kuwa nayo kama mwananchi tatizo pale unapojaribu kudai kuwakilisha wananchi wote wa Tanzania kwa sababu ya kitendo cha wabunge 46 tu wa Chadema, ili uweze kufanikiwa kwenye uwanja wa werevu kama hapa, ni lazima uwe na more hard evidence zaidi ya "Muonekano", unasema "Ushahidi ni wazi" wengine tunauliza huo ushahidi uko wapi kwamba Dr. Slaa, ndiye aliyeshinda U-Rais akaibiwa?

- Moja ya hasara kubwa sana za hiki kitendo ni kushawishi vikundi katika jamii kuanza kudai haki zao nje ya sheria za jamhuri, ndio maana CCM wanatakiwa kuwa waangalifu sana on how they respond to this, maana one mistake wataingiza hili taifa kwenye matatizo makubwa sana na hasa wakionyesha kuogopa, hawatakiwi kuonyesha kuogopa maana haya ni mambo ya kawaida kwenye siasa za Demokrasia na vyama vingi, behind the scene ni lazima kufanyike juhudi za kusikiliza kilio cha Chadema on NEC ambayo kama kuna ushahidi wa kutosha kwamba yapo matatizo huko basi yatatuliwe kikatiba sio kupindisha pindisha mambo ili wabunge wa Chadema waache, I mean huenda ikawa vyema kwa CCM kuwaacha wabunge wa Chadema waendelee na hii protest and then wananchi wataamua kwenye kura zijazo kama vile Clinton alivyowafanyia Republicans under Gingrich, waliishia kuisimamisha Federal government lakini kwenye uchaguzi uliofuatia wananchi wakawafundisha adabu Republicans kwa lile kosa,

- Again mkuu wabunge 46 wa Chadema hawatuwakilishi wananchi wote wa Tanzania katika hiyo imani kwamba, Dr. Slaa ndiye aliyeshinda huu uchaguzi na kwamba ameibiwa na NEC na Rais aliyeshinda, tunahitaji kuona strong evidence hasa hapa kwenye uwanja wa werevu!


William.
 
Slaa hakudai kuwa yeye ndio angeshinda uraisi..,alidai kuwa KURA alizopata kikwete zimechakachuliwa...,na wao kama chadema wako tayari kukubali ushindi wa kikwete uwe wa asilimia 40 au asilimia 90,as long as hakuna mapungufu makubwa(naamini uliyaona hayo mapungufu,hamna haja ya kuyarudia).

wabunge wa CCM hawana uhusiano wa moja kwa moja na kikwete,wao walichaguliwa kwa kura tofauti,wale ambao walichakachua,kesi zao ziko mahakamani..,kikwete hawezi pelekwa huko kwa sababu ya katoba yetu kutoruhusu.

sitegemei kuona wabunge wakiprotest wabunge wenzao maana hayawahusu..,na kuna platform ya malalamiko ya kibunge(mahakama)

- Mkuu maelezo yako ni sawa, lakini hapo ni tatizo la sheria sio la Rais aliyechaguliwa na kuthibitishwa na NEC kwa mujibu wa katiba, naomba kukuuliza hapa kosa la Rais ni lipi la kuwafanya Chadema, kumsusia? Wangemsusia Mkuu wa NEC ningeelewa!


William.
 

- Mkuu maelezo yako ni sawa, lakini hapo ni tatizo la sheria sio la Rais aliyechaguliwa na kuthibitishwa na NEC kwa mujibu wa katiba, naomba kukuuliza hapa kosa la Rais ni lipi la kuwafanya Chadema, kumsusia? Wangemsusia Mkuu wa NEC ningeelewa!


William.
Unajua its funny,but true..,kikwete kama Rais hana Kosa,lakini Taasisi anayoiongoza ya Urais ina makosa...,na hiki ndicho chadema wanachokisimamia...,
Kama kikwete hakuchakachua kura si angeruhusu tu recount?kwa nini aogope?

KUHUSU KUMSUSIA MKUU WA NEC RUDIA MFANO WANGU HAPO JUU...,ukiletewa chakula chenye nzi/hakijaiva mgahawani na waiter...,asipokubali kubadilisha..,huwa unagombana na waiter au unaenda kwa mpishi/manager?mchukulie mhudumu kama messenger..m
 
Unajua its funny,but true..,kikwete kama Rais hana Kosa,lakini Taasisi anayoiongoza ya Urais ina makosa...,na hiki ndicho chadema wanachokisimamia...,
Kama kikwete hakuchakachua kura si angeruhusu tu recount?kwa nini aogope?

- Hapa umeleta neno jipya na muhimu sana, RECOUNT kwani katiba yetu inasema nini on that?

William
 

- Mkuu heshima sana, haya again ni maoni yako binafsi ambayo ni haki yako kuwa nayo kama mwananchi tatizo pale unapojaribu kudai kuwakilisha wananchi wote wa Tanzania kwa sababu ya kitendo cha wabunge 46 tu wa Chadema, ili uweze kufanikiwa kwenye uwanja wa werevu kama hapa, ni lazima uwe na more hard evidence zaidi ya "Muonekano", unasema "Ushahidi ni wazi" wengine tunauliza huo ushahidi uko wapi kwamba Dr. Slaa, ndiye aliyeshinda U-Rais akaibiwa?

- Moja ya hasara kubwa sana za hiki kitendo ni kushawishi vikundi katika jamii kuanza kudai haki zao nje ya sheria za jamhuri, ndio maana CCM wanatakiwa kuwa waangalifu sana on how they respond to this, maana one mistake wataingiza hili taifa kwenye matatizo makubwa sana na hasa wakionyesha kuogopa, hawatakiwi kuonyesha kuogopa maana haya ni mambo ya kawaida kwenye siasa za Demokrasia na vyama vingi, behind the scene ni lazima kufanyike juhudi za kusikiliza kilio cha Chadema on NEC ambayo kama kuna ushahidi wa kutosha kwamba yapo matatizo huko basi yatatuliwe kikatiba sio kupindisha pindisha mambo ili wabunge wa Chadema waache, I mean huenda ikawa vyema kwa CCM kuwaacha wabunge wa Chadema waendelee na hii protest and then wananchi wataamua kwenye kura zijazo kama vile Clinton alivyowafanyia Republicans under Gingrich, waliishia kuisimamisha Federal government lakini kwenye uchaguzi uliofuatia wananchi wakawafundisha adabu Republicans kwa lile kosa,

- Again mkuu wabunge 46 wa Chadema hawatuwakilishi wananchi wote wa Tanzania katika hiyo imani kwamba, Dr. Slaa ndiye aliyeshinda huu uchaguzi na kwamba ameibiwa na NEC na Rais aliyeshinda, tunahitaji kuona strong evidence hasa hapa kwenye uwanja wa werevu!


William.

Hapo ndugu unausahau msingi mkuu zaidi wa demokrasia,MINORITY RIGHTS..,kwa mantiki yako kikwete hafai kuwa raisi wa watanzania kwani amechaguliwa na asilimia 42 tu ya watu wanaostahili kupiga kura,na hao pia ni asilimia 12 tu ya wananchi wote ya jamhuri yetu.

wanafalsafa waliwahi sema hauwezi tatua tatizo kwa kutumia njia/ufikiri/ujuzi sawasawa na wakati tatizo lile lilipotengeneza,unatakiwa ufiirie zaidi..,ndicho wanachofanya hawa mabwana.

back in 1950's nyerere et al waliitwa wahaini etc..,sioni tatizo chadema wakipewa majina yasiyopendeza kutoka kwa wanaokula nchi..,sitegemei viongozi wa CCM watasema wanachokifanya CHADEMA ni mfano wa kuigwa
 
- Hapa umeleta neno jipya na muhimu sana, RECOUNT kwani katiba yetu inasema nini on that?

William

The possibility of a recount was there before the announcing of winners.a Loophole CCM exploited fully...,hence the repay from chadema
 
Hapo ndugu unausahau msingi mkuu zaidi wa demokrasia,MINORITY RIGHTS..,kwa mantiki yako kikwete hafai kuwa raisi wa watanzania kwani amechaguliwa na asilimia 42 tu ya watu wanaostahili kupiga kura,na hao pia ni asilimia 12 tu ya wananchi wote ya jamhuri yetu.

wanafalsafa waliwahi sema hauwezi tatua tatizo kwa kutumia njia/ufikiri/ujuzi sawasawa na wakati tatizo lile lilipotengeneza,unatakiwa ufiirie zaidi..,ndicho wanachofanya hawa mabwana.

back in 1950's nyerere et al waliitwa wahaini etc..,sioni tatizo chadema wakipewa majina yasiyopendeza kutoka kwa wanaokula nchi..,sitegemei viongozi wa CCM watasema wanachokifanya CHADEMA ni mfano wa kuigwa

- Mkuu msingi wa MINORITY RIGHTS unapatikana Supreme Court, Mzee Madison wa USA the author wa Mihimili mitatu ya serikali, alisema kwamba Judicial System katika Demokrasia ni muhimu sana kwa ajili ya simply kusimamia haki za Minority kwa hiyo ni lazima iwe huru, kwa hiyo mahakamani ndiko hasa hili tatizo la Chadema minority kama ulivyosema linatakiwa kupelekwa huko.

- Asilimia za kuwa Rais wa jamhuri zinathibitishwa na katiba kwa hiyo kama ni 42% tu waliopiga kura, inategemea katiba inasema nini, unless kama unasema katiba inasema wabunge 46 wanaweza kubadili katiba kwa kugomea kumtambua Rais!

- Kufikiria zaidi ndicho exactly tunachokifanya hapa kama sikosei, tunajaribu kujadili kwenye level tofauti na mtaani, yaani kujaribu kuelewa nini kesi ya Chadema kwa taifa!
, maana wengine tunashindwa kuiona so far!

William.
 
"Mh Zitto kabwe, Mh Shibuda, Mh Lucy owenya, Mh ndesamburo pamoja na kafulila hawa wote leo hawakwenda bungeni kwa kuwa hawakutaka (kutoka wakati Rais anahutubia), walipingana na tendo hilo,Je kama Rais aliapa kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri na wabunge pia unawezaje kusema humtambui?????hivi ndivyo adabu ya mtoto kwa baba yake???ama kweli MTOTO UMLEAVYO NDIVYO AKUAVYO,ila sisi wananchi tutawafunda" - Violet Mzindakaya.
 
Mimi mambo ya nidhamu ya mtoto kwa baba siyafagilii. If anything tunahitaji kukosa nidhamu zaidi.

Ila kama nilivyosema mwanzo, hii habari ya kutomtambua rais inaonekana kutoka kwa Slaa sana, wabunge wanaonekana kushinikizwa tu.
 
Mimi mambo ya nidhamu ya mtoto kwa baba siyafagilii.

Ila kama nilivyosema mwanzo, hii habari ya kutomtambua rais inaonekana kutoka kwa Slaa sana, wabunge wanaonekana kushinikizwa tu.

Kiongozi,
hiyo nimeweka quotation kwa sababu nimeichukua kama ilivyo toka kwa Violet mzindakaya.
Nimeshtuka kuona kuwa hata hapa JF hatupewi taarifa muhimu kama hizi. Kwa nini hatuambiani ukweli kuwa uamuzi huo kuna wasiouunga mkono?
 
@ZE... thanks sana tu, kumbe umeitoa kwa Vai, hahahaaaa!!! yuko chama gani?
 
Kiongozi,
hiyo nimeweka quotation kwa sababu nimeichukua kama ilivyo toka kwa Violet mzindakaya.
Nimeshtuka kuona kuwa hata hapa JF hatupewi taarifa muhimu kama hizi. Kwa nini hatuambiani ukweli kuwa uamuzi huo kuna wasiouunga mkono?

Kiongozi huwezi kutegemea kupata ukweli kuhusu Slaa kutoka kwa Kikwete now, au unaweza?

Vipi kama hizi ni propaganda za kipinzani tu?
 
Back
Top Bottom