Viongozi 4 wa CHADEMA watinga Polisi, Heche na Mnyika washikiliwa, Mdee na Matiko wanasakwa. Waachiwa kwa dhamana

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,458
7,837
Dar es Salaam.Viongozi wanne wa CHADEMA wamewasili Kituo Kikuu cha Polisi wakiongozwa na Katibu Mkuu Dk. Vicenti Mashinji.

Viongozi hao ambao wamewasili Polisi kwa ajili ya kuitikia wito ni pamoja na manaibu katibu John Mnyika na Salum Mwalimu pamoja na Mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti John Heche.

Wakili wao Fredrick Khiwelo amesema wengine wako njiani akiwamo Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Aikaeli Mbowe.

Awali Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa Hai kwa Taifa Leo tarehe 22 Machi 2018, ametoa waraka wa kuitwa Polisi yeye na viongozi wenzake.

Katika waraka huo Mbowe amesema kwamba kuna taarifa pia ya kumuunganisha Peter Msigwa, Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa (Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa) na Mjumbe wa Kamati Kuu katika shauri hili.

====

UPDATES:

Baadhi ya viongozi waandamizi wa CHADEMA, wameachiwa na polisi katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar, wametakiwa kuripoti tena Machi 27 kwa mahojiano.

Wakati huo huo viongozi wa chama hicho John Heche na John Mnyika, wanaendelea kushikiliwa kituoni hapo kwa mahojiano.

Jeshi la Polisi limetoa amri kuwa Wabunge Halima Mdee na Ester Matiko wa CHADEMA wakamatwe popote walipo na kufikishwa Polisi kwa mahojiano.

Jeshi la polisi kanda ya maalumu ya Dar es Salaam limewaachia kwa dhamana viongozi waandamizi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo na kutakiwa kuripoti tena Machi 27 kwa ajili ya kuendelea na mahojiano zaidi.

Habari zaidi....

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika na Mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Serengeti, John Heche wameachiwa kwa dhamana baada ya kuhojiwa kwa zaidi ya saa mbili katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam.


Mara baada ya kuachiwa, Heche ambaye ni mbunge wa Tarime Vijijini amesema kitendo cha viongozi wa Chadema kuripoti polisi na kukaa kwa saa tano bila kuhojiwa chochote na kutakiwa kuripoti siku nyingine ni sawa na kifungo cha nje.


“Hii ni mara ya tano ninaripoti polisi. Polisi Tanzania ni kama wametuhukumu kifungo cha nje, kila baada ya siku mbili wanataka turipoti kituo kikuu cha Polisi Dar es Salaam bila kujali unaishi wapi, gharama unazotumia kuja na kurudi Dar es Salaam na majukumu yako mengine ya kikazi unayoshindwa kuyatekeleza. Kuna wakati inabidi kukataa uonevu huu,” amesema Heche

Leo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe; Katibu Mkuu, Dk Vicent Mashinji; naibu makatibu wakuu, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar) pamoja na Heche waliripoti kituoni hapo kwa ajili ya mahojiano.


Hata hivyo, mbunge huyo wa Tarime Vijijini na Mnyika waliendelea kuhojiwa huku wenzao wakiachiwa kwa dhamana, sababu ya wao kubaki kituoni hapo ikielezwa kuwa ni kitendo chao cha kutoripoti Machi 16, 2018.


Mara baada ya kuachiwa viongozi hao wametakiwa kuripoti tena kituoni hapo Machi 27, 2018.


Heche amesema kitendo wanachofanyiwa si sahihi kwa maelezo kuwa baadhi yao ni wabunge na kwa sasa wanapaswa kushiriki vikao vya kamati za chombo hicho.


“Mimi napaswa kuwa katika vikao vya kamati za Bunge Dodoma. Mbali na hilo nikiwa jimboni kwangu, kutoka huko mpaka Dar es Salaam natumia nauli zaidi ya Sh1milioni. Hivi kwa nini hawalioni hili,” amehoji Heche.


Amesema kwa hali ilivyo ni vyema wakaelezwa hatima yao kwa maelezo kuwa mbali na kupoteza fedha, pia wanashindwa kushiriki shughuli za kibunge.


“Mfano wanataka turejee tena Jumanne ijayo (Machi 27, 2018). Hapa ninaondoka nakwenda Dodoma kushiriki vikao vya kamati, nitalazimika kuondoka jumatatu ili kuwahi. Sasa huu ni usumbufu kwa kweli. Katika hili sitakubali nitafanya kitu,” amesema Heche.


Wakili wa viongozi hao, Frederick kihwelo amesema Mnyika na Heche walizuiwa kuondoka na kutakiwa kuandika maelezo.


"Baada ya kufika, polisi waliwataka Heche na Mnyika ambao hawakufika Machi 16 . Walitaka wabaki baada ya wenzao kuondoka na kuwaagiza kuandika ahadi ya maandishi kuwa Jumanne ijayo watakuwepo,”amesema.
 
Hata wangewasweka kamati kuu nzima, hawawezi zuia mafuriko kwa mikono. Hali imeshabadilika na kila mtu sasa yupo prepared kwa lolote.

Wanatakiwa kujua kwamba mindset yetu ni kwamba sisi tumeshakubali yote, tumetekwa nyara, tunateswa, tunakamatwa na hata baadhi yetu kuuwawa na hao "malimbukeni wa madaraka" na waliosalama mpaka sasa siyo sisi bali ni vizazi vijavyo.

Hivyo basi mapambano haya hatujipiganii sisi, tunapigania vizazi vyetu na taifa la baadae! Hivyo sisi watufanye watakavyo tu, tumejikatia tamaa lakini tunao morale wa kuwa tumejitoa muhanga sasa kukomboa taifa letu kwa faida ya wanetu!
 
Baadhi ya viongozi waandamizi wa Chadema, wameachiwa na polisi katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar, wametakiwa kuripoti tena Machi 27 kwa mahojiano.

Wakati huo huo viongozi wa chama hicho John Heche na John Mnyika, wanaendelea kushikiliwa kituoni hapo kwa mahojiano [HASHTAG]#MwananchiUpdates[/HASHTAG]
 
Hii sasa sifa. Huu mchuano wa kukomoana unatuharibia amani na mshikamano wetu kama Taifa. Hivi ni lazima Magufuli ajibu kila "tusi" kwa kuwakamata waliomtukana na kuwaharrass? Strong men never waste time on petty issues. Hii ni ishara ya udhaifu mkubwa. Ni aina flani ya ugonjwa. Mental instability.
 
Leo tena viongozi wa Chama kikuu cha Upinzani wameripoti Polisi na kuambiwa warudi tens 27/3. Huu ni mfululizo wa nenda rudi zisizo na ukomo huku Mwenyekiti Mbowe akitoa tamko kuwa kuna jambo linapikwa ili wawekwe ndani muda mrefu kwa kesi aitha ya Uhaini, uhujumu au yeyote itakayo watoa kwenye mstari kwa muda mrefu.
Uvumilivu wanao onyesha ni mkubwa dhidi ya maonevu ya dola lakini kwa vile dola ina kila kitu basi hawana cha kufanya.
Nchi wahisani zitoazo misaada na mikopo kwa Maendeleo ya nchi yetu jee mabalozi wao hawaoni hali hii ilivyo? Sasa sio wanasiasa tuu wanaokabiliwa na tishio la ukandamizaji wa demokrasia bali wapo wanafunzi, wafanyabiashara, waandishi na hata viongozi wa dini.
Nadhani ili kuokoa hawa wasio na nguvu ya kuadabisha dola ni eitha kupata msaada wa karipio kutoka kwa mabalozi wa nchi wahisani au wananchi wenyewe kuamua KUANDAMANA BILA UKOMO kuwasemea wenzao.
Ila hii option ya pili ni hatari sana kwa utawala wowote duniani kwani huwa inazua machafuko, inaondoa utawala madarakani, yaweza kuleta vifo na hatimae wachache wenye mamlaka kuishia The Hague.
Kwa nini wanaruhusu kulibomoa Taifa? Mzee Mwinyi, Mkapa na JK mko wapi kushauri? Au mnaona haya hayawahusu na mnakula pension zenu kwa raha?
Nakuhakikishieni kikiwaka hata nyie hamtakuwa salama aslani!
 
Hawa hawachoki kuvunja sheria.. nini tena wamefanya? maana wanapenda kwenda polisi na mahakamani.. hawaoni wenzao wengine wanaotii sheria!
 
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Jeshi la Polisi limetoa amri ya kukamatwa popote walipo kwa wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mbunge Kawe, Halima Mdee na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiku, kutokana na kutoripoti polisi wiki iliyopita.

Wakili wa Chadema, John Malya amesema hatua hiyo inatokana na wabunge hao kushindwa kuitikia wito uliowataka kuripoti polisi wiki iliyopita kwa sababu walikuwa wakihudhuria vikao vya kamati za bunge vinavyoendelea Mjini Dodoma.


Aidha Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na Mbunge wa Kibamba, John Mnyika wamewekwa chini ya ulinzi kusubiri maelekezo ya kwa nini hawakuhudhuria wiki iliyopita.

Nadhani kulikuwa na Mwongozo wa Spika kuhusiana na Shughuli ya Bunge dhidi vs Wito/Ukamataji wa Mbunge- wajuvi yawezekana sijalisikia vizuri au kumbukumbu haiko vizuri.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hata wangewasweka kamati kuu nzima, hawawezi zuia mafuriko kwa mikono. Hali imeshabadilika na kila mtu sasa yupo prepared kwa lolote.

Wanatakiwa kujua kwamba mindset yetu ni kwamba sisi tumeshakubali yote, tumetekwa nyara, tunateswa, tunakamatwa na hata baadhi yetu kuuwawa na hao "malimbukeni wa madaraka" na waliosalama mpaka sasa siyo sisi bali ni vizazi vijavyo.

Hivyo basi mapambano haya hatujipiganii sisi, tunapigania vizazi vyetu na taifa la baadae! Hivyo sisi watufanye watakavyo tu, tumejikatia tamaa lakini tunao morale wa kuwa tumejitoa muhanga sasa kukomboa taifa letu kwa faida ya wanetu!
Ungewasindikiza huko,na ukadeliver hii message mbele yao mkuu,
 
Back
Top Bottom