Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,239
- 44,477
Na. M. M. Mwanakijiji
Askari wanapokuja kukukamata wanajitambulishaje? Unajuaje watu waliokusimamisha au wanaodai kuwa ni "maafisa usalama au askari" kweli ni maafisa usalama? Je, ukiwa na mashaka nao unaweza kupiga simu namba gani au umpigie nani kuuliza?
Watanzania katika mazingira ya utekaji tumekubali kuwapa uhalali kwa bunduki. Yaani, mtu akikusimamisha huku amebeba bundling au wakiwa kwenye gari wanamchukua mwenzenu kisa tu Wana bundling inabidi mkubali kwa kudhania wanaofanya hivyo ni maafisa wa usalama. Matokeo yake tunawapa uhalali kwa bunduki (the gun mandate).
Imefikia mahali kuwa hata kama hakuna uchaguzi halali umefanyika tumekubali kuwapa uhalali kwa sababu kuna vimulimuli, ving'ora na saluti!! Na was wanajua hili. Hawaitaji kutushawishi tena kwa maneno wala kwa hoja. Ushawishi siyo tena wa nguvu za hoja Bali hoja za nguvu. Wanasema mwenye nguvu mpishe!!
Tukumbuke kuwa Muammar Gadaffi alikuwa na vimulimuli, ving'ora. Na saluti;
Mladic Generali wa Kiserbia aliyekuwa anatumikia kifungo cha maisha ICC alikuwa na vimulimuli, ving'ora na saluti!;
Hosni Mubarak alikuwa na vimulimuli, ving'ora na saluti;
Utawala wa Samia hauwezi kutegemea hofu, woga, wasiwasi, nabkutokuaminiana. Hauwezi kushinda nguvu za hoja kwa kutegemea hoja za nguvu za risasi! Watampigia saluti, wataapishana na misafara yao itaongezwa vimulimuli na ving'ora!
Lakini maswali yatabakia...na hayatojibiwa mpaka yatakapojibiwa kwa hoja!!! Na mengine yataendelea kuja! Hayaishi mpaka yaishe!!
Haya pigeni saluti!!!