Vikosi na makambi JKT

Vikosi na makambi JKT

B Coy! Platoon one section one. Kibooko Enzi hizo platoon commander S/Sergeant Mwiba.
Du umenikumbusha mbali mkuu. Namkumbuka afande Mwiba. Huyu kama sikosei alikuwa ni Mhaya. Alikuwa ana mikwara flani lakini alikuwa safi sana. Katika B Coy hiyo kulikuwa na staf sajenti Warangi wa wili. Mmoja alikuwa anapenda sana sifa lakini ukimsifia tu mambo yanakuwa shwari. Mimi nilikuwa mwaka1987-1988,... Ninahamu ya kwenda tena huko
 
askari wa kileo ni Rais kutoa sir I za jeshi sana nahisi hata tukiwauliza idadi ya wanajeshi,silaha,ramani ya kambi na etc mtataja wote mulio komenti mjitafakari ni wepesi kununuliwa na age zenu ni 22-30
Hilo nimeliona hata Mimi...hawa ni wapenda sifa kabisa wajulikane tu walipita huko.Kwanza hata kuorodhesha tu hivyo vikosi vya jeshi na kuanza kuvielezea ni makosa kwa majibu wa taratibu za Jeshi.
 
Ilikuwa raha sana na misamiati yake:

Kujongo
Selule
Top layer
Dunia
Disco
Vest (green vest ya kijani)
Mestin

Wahenga wenzangu ongezeni hapo
 
Ilikuwa raha sana na misamiati yake:

Kujongo
Selule
Top layer
Dunia
Disco
Vest (green vest ya kijani)
Mestin

Wahenga wenzangu ongezeni hapo
pitishoti= PT shot(phsical training shot)
Hanga
order
=======imezuiliwa======
 
kwa aina hii ya maaskari tulionao, ni rahisi sana kwa majasusi wa nje kupata taarifa za kijeshi kuhusu nchi yetu, yanabwabwaja hadharani utadhani kuwa askari ni sifa, hii ni mitandao ya kijamii hebu kuweni na akiba aisee, mnataja kambi ( location), Op, na makamanda ( OCs, platoon commanders) n.k.
hamfai kabisa.

Ngw'ana Kabula
 
kwa aina hii ya maaskari tulionao, ni rahisi sana kwa majasusi wa nje kupata taarifa za kijeshi kuhusu nchi yetu, yanabwabwaja hadharani utadhani kuwa askari ni sifa, hii ni mitandao ya kijamii hebu kuweni na akiba aisee, mnataja kambi ( location), Op, na makamanda ( OCs, platoon commanders) n.k.
hamfai kabisa.

Ngw'ana Kabula
siku hizi hamuna siri hizo, great deal ni namna ya ku perform BATTLE DRILLS
mfano hai: mreno akidhamiria kushambulia 842 kj au farm 17 mamba wa mto ruvuma wanamshughulikia mpaka anaishiwa viazi vyote. Mkongo akidhamiria kushambulia burombora , sokwe wa hifadhi ya Gombe wanamshughulikia mpaka anasahau nja aliyopitia.

Kama umeelewa nilichoandika basi unajua maana ya siri ya ulinzi wa taifa letu.

Ndo maana tunapokea kila sura kujiunga na JKT compulsory, kisha mnaondoka na uraia wenu mnatuachia jeshi letu na ulinzi wetu imara
 
Ahha kumbe uzi huu unatufundisha siri ya jeshi kuwa JKT namba yao ya kikosi zinaanza na 8.
Haya twende,komando,mizinga,mp,kifaru,anga,afya,ardhini ,majini?
 
siku hizi hamuna siri hizo, great deal ni namna ya ku perform BATTLE DRILLS
mfano hai: mreno akidhamiria kushambulia 842 kj au farm 17 mamba wa mto ruvuma wanamshughulikia mpaka anaishiwa viazi vyote. Mkongo akidhamiria kushambulia burombora , sokwe wa hifadhi ya Gombe wanamshughulikia mpaka anasahau nja aliyopitia.

Kama umeelewa nilichoandika basi unajua maana ya siri ya ulinzi wa taifa letu.

Ndo maana tunapokea kila sura kujiunga na JKT compulsory, kisha mnaondoka na uraia wenu mnatuachia jeshi letu na ulinzi wetu imara
Hahahaaaaa,,,,,,,,,,,,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna afande mmoja wa kike alikuwa mzuri hataree, sasa ukikutanisha naye macho tu, unasikia anawaita maafande wenzake.......afande lukangaa kuruta ananitongoza..... sasa kaka lazima umkumbuke bi mkubwa home kwa doso utakalokula.
 
Back
Top Bottom