Kikojozi
JF-Expert Member
- Mar 24, 2009
- 331
- 1
Nilikua najiuliza kama vikomo vya nauli vinavyopangwa na serikali vinawafanya wamiliki wa magari kushindwa kumudu gharama za uendeshaji na hivyo kupendelea kuajiri madereva wasio na sifa bila mikataba kwa ujira duni, kutumia magari mabovu na yaliyochoka na kuwakatisha tamaa wajasiriamali/wawekezaji wanaotaka kununua na kuendesha magari/mabasi mapya na ya kisasa.
Kama kwa mabasi yaendayo mikoani mfano Arusha kikomo cha nauli ni shs 50,000/- kwa full luxury. Ina maana serikali inanikataza mimi kama mwekezaji kununua full luxury mpya ya mwaka 2010 yenye "airbags" kwa kila abiria na kila aina ya kifaa kuhakikisha usalama kwa abiria ambayo gharama yake ya uendeshaji kwa kila abiria huenda ikawa 80,000/-? Kama kuna watu wako radhi kulipa shs100,000/- nauli ya Arusha kusafiri na basi jipya na la kisasa kabisa kuna tatizo?
Kwa kifupi, vikomo vya nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani vinatulazimu kusafiri kwa kutumia mikweche/vimeo vinavyoendeshwa na vihiyo na hivyo kusababisha ajali nyingi?
Is cheap expensive?
Kama kwa mabasi yaendayo mikoani mfano Arusha kikomo cha nauli ni shs 50,000/- kwa full luxury. Ina maana serikali inanikataza mimi kama mwekezaji kununua full luxury mpya ya mwaka 2010 yenye "airbags" kwa kila abiria na kila aina ya kifaa kuhakikisha usalama kwa abiria ambayo gharama yake ya uendeshaji kwa kila abiria huenda ikawa 80,000/-? Kama kuna watu wako radhi kulipa shs100,000/- nauli ya Arusha kusafiri na basi jipya na la kisasa kabisa kuna tatizo?
Kwa kifupi, vikomo vya nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani vinatulazimu kusafiri kwa kutumia mikweche/vimeo vinavyoendeshwa na vihiyo na hivyo kusababisha ajali nyingi?
Is cheap expensive?