Nenda kwanza shule unachelewa,kisha fuatilia kwa muda wako,machafuko ya Libya yalifadhiliwa na nani? msafara wa Gaddafi ulikua unashambuliwa toka juu na ndege za nchi gani kabla ya Gaddafi kukamatwa na kuuawa.Nikumbushe vizuri, Gadafi aliuliwa na wazungu gani?
Gaddafi aliogopewa hata baada ya kufa,walijua kua,kama watu wangekua wanaliona kaburi lake basi wangehamasika zaidi hata kulipa kisasi,waliogopa kizazi kijacho kuja kuona kaburi la shujaa wao,alizikwa Jangwani tena usiku ili watu wasijue kaburi lake lilipo!
Hata Osama Bin Laden waliitupa maiti yake baharini badala ya kuizika! kwa sababu hizo hizo ambazo ni uoga wa wazungu,
Halafu kutwa wao hao hao wanapiga kelele eti haki za binadamu! Mzungu ataendelea kutuchezea akili mpaka siku tutakapo amua sisi wenyewe kutoka usingizini.
Waafrika tunasahau haraka:Ilikuwa mwaka 2011 ndipo alipoonekana kwa Mara mwisho kiongozi wa zamani wa Libya colonel GADAFI.
Ni katika hotuba zake na pia akiuawa na vikosi vya waasi wakisimamiwa na NATO air Force.
Lakini haikuonekana tena maiti ya Gadafi ikizikwa popote katika ardhi ya Libya ama popote duniani.
Baada ya maelezo haya nawasilisha kwa kuomba kuuliza Tena kwa wanajamii forums
"" VIKO WAPI KABURI NA MWILI WA COLONEL GADAFI?”
Petroleum and coalKuna siku wataonekana tu ..itakapofika kipindi wanataka kuweka historia wazi watamuonyesha kwenye majumba yao ya historia ikiongozwa na maneno haya HUYU NDIYE ALIEKUWA KIONGOZI WA LIBYA ALIEFANYIA WANANCHI WAKE KILA KITU .. LAKINI KUTOKANA NA WA AFRICA HAWANA AKILI WAKAMUUWA WENYEWE KIONGOZI WAO ...Mi.i nakwambi badae hawa jamaa wa mataifa makubwa wanakuja kuturuka waafrica kwa kuona kila kitu tulikuwa tunataka wenyewe...Ngoja wavune wanavyovitaka vikiisha utaona kama kutakuwa na taifa linalokushobokea ...Hebu naomba kujuzwa pale Somalia kunapatikana nini katika Taifa lile