Adamu Alphonce
Senior Member
- May 2, 2012
- 146
- 226
Mtu anaeuliza bei ya vitu kila siku na kununua hanunui..!.kila unahonunua anataka ajue umenunua bei gani..!
Kwa lengo la kuwekana sawa, unaweza ukawa unatabia mbaya, ila hujui kama ni mbaya mbele za watu.
Mimi katika kuishi na watu mbalimbali, nimeshuhudia watu wenye tabia tofauti tofauti ila tunavumiliana tu, wakati mwingine tunarekebishana..!
Hizi hapa ni zile chache miongoni mwa nyingi ninazozikumbuka toka kwa watu niliwahi kuishi nao..
- Kutumia simu wakati wa kula. Hii nimeiweka ya kwanza kabisa kwa sababu ilikuwa tabia yangu, mama yangu kila alipokuwa akinikemea niliona kama anazingua tu! ila siku nilipokemewa ugenini ndio nikaamini kweli hii ni tabia mbaya, na nikaacha mara moja.
- Kutawala mazungumzo. Huyu alikuwa rafiki yangu, classmate, alikuwa anapenda aongee yeye muda wote, hata kama mada haijui vizuri hakupenda kuwa msikilizaji kabisa.
- Kutotambua muda wa utani. Hii niliiona kwa watu wengi sana, ila tamzungumzia jamaa yangu mmoja hivi, Rashid (R.I.P), huyu mshikaji alikuwa hawezi kuwa serious, alikuwa hajali mood ya mtu, hajali watu waliokuzunguka muda huo, yeye atakachoona kinafaa kukutania anakisema tu popote wakati wowote.
- Kutumia viwakilishi badala ya jina la mtu. Hii nayo niliiona kwa wengi, unakuta mtu analijua jina lako kabisa, lakini anakuita, wewe, huyu, yule.
- Kukosoa ovyo ovyo. Sikatai mtu kukosolewa anapokosea, ila unapokosoa hakikisha una lengo la kumuelimisha mkosolewa na sio kumuaibisha au kwa lengo la kujikweza mbele za watu, jambo la kuzingatia zaidi, lugha ya ukarimu itumike.
- Kucheka hadi kwenye serious moments. Wengine sijui huwa ni makusudi au sijui ndo hawezi kuzuia kicheko, yaani mtu hatambui nyakati za kuwa serious, kicheko kikija, yeye anacheka tu! ni kweli kuna jambo linaweza kukufurahisha peke yako na ukajikuta umeshindwa kuzuia kicheko, basi ukacheka. Huenda watu wakakuvumilia wakajua ni bahati mbaya tu! ajabu inakujua pale inapoonekana kuwa wewe sasa umekuwa ni mtu wa kuchekacheka kila muda ni wewe tu!
Dah! mi nilidhani ile harufu inayotoka wakati wa kupiga chafya huwa ni mimi tu inanikera.Tabia ya kutema mate ovyo.
Kupiga chafya tena inayonuka na huombi msamaha.
Puuu.
Kuongea huku unatafuna chakula.
Hahahahamkuu umepanga?wananikera sana hawa ndugu
Punguza uchoyoDah kuna watu wanapenda sana kupiga mizinga (kuomba hela), yaani hata kama ni mshkaji au ndugu unaogopa hata kumpigia umsalimie maana lazima tu atakupiga mzinga. Ukiona simu yake roho inakwenda mbio hata kupokea unaogopa.
Mkuu umesahau kale katabia kako ka kunuka sox vepee umesahau kukaodhesha au labda hujakasanukia!Kwa lengo la kuwekana sawa, unaweza ukawa unatabia mbaya, ila hujui kama ni mbaya mbele za watu.
Mimi katika kuishi na watu mbalimbali, nimeshuhudia watu wenye tabia tofauti tofauti ila tunavumiliana tu, wakati mwingine tunarekebishana..!
Hizi hapa ni zile chache miongoni mwa nyingi ninazozikumbuka toka kwa watu niliwahi kuishi nao..
- Kutumia simu wakati wa kula. Hii nimeiweka ya kwanza kabisa kwa sababu ilikuwa tabia yangu, mama yangu kila alipokuwa akinikemea niliona kama anazingua tu! ila siku nilipokemewa ugenini ndio nikaamini kweli hii ni tabia mbaya, na nikaacha mara moja.
- Kutawala mazungumzo. Huyu alikuwa rafiki yangu, classmate, alikuwa anapenda aongee yeye muda wote, hata kama mada haijui vizuri hakupenda kuwa msikilizaji kabisa.
- Kutotambua muda wa utani. Hii niliiona kwa watu wengi sana, ila tamzungumzia jamaa yangu mmoja hivi, Rashid (R.I.P), huyu mshikaji alikuwa hawezi kuwa serious, alikuwa hajali mood ya mtu, hajali watu waliokuzunguka muda huo, yeye atakachoona kinafaa kukutania anakisema tu popote wakati wowote.
- Kutumia viwakilishi badala ya jina la mtu. Hii nayo niliiona kwa wengi, unakuta mtu analijua jina lako kabisa, lakini anakuita, wewe, huyu, yule.
- Kukosoa ovyo ovyo. Sikatai mtu kukosolewa anapokosea, ila unapokosoa hakikisha una lengo la kumuelimisha mkosolewa na sio kumuaibisha au kwa lengo la kujikweza mbele za watu, jambo la kuzingatia zaidi, lugha ya ukarimu itumike.
- Kucheka hadi kwenye serious moments. Wengine sijui huwa ni makusudi au sijui ndo hawezi kuzuia kicheko, yaani mtu hatambui nyakati za kuwa serious, kicheko kikija, yeye anacheka tu! ni kweli kuna jambo linaweza kukufurahisha peke yako na ukajikuta umeshindwa kuzuia kicheko, basi ukacheka. Huenda watu wakakuvumilia wakajua ni bahati mbaya tu! ajabu inakujua pale inapoonekana kuwa wewe sasa umekuwa ni mtu wa kuchekacheka kila muda ni wewe tu!
Kutema tema vitu hovyo tena huangalii ni wapi.Mfano mnakula samaki,basi mtu miba anatemea hata chipi ya sakafu au hata kwenye kapeti....Tabia ya kutema mate ovyo.
Kupiga chafya tena inayonuka na huombi msamaha.
Puuu.
Kuongea huku unatafuna chakula.
Haha ahsante kwa kunishtua aiseeHeaven Sent njoo huku ucheke comments za hawa wakuu!
Hata hii nayo inakera. Nani alichagua maumbile ya jinsi alivyo? Wengine warefu, wengine wafupi, wengine wembamba, kuna weusi na weupe wewe ni nani hata uwacheke watu kwa maumbile yao?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]una kibamia mkuu??