Mung Chris
JF-Expert Member
- Sep 12, 2017
- 3,438
- 3,951
Wadau kaeni sawa imenitokea. Matapeli wapo kazini.
Hawa vijana wanao tangaza kuwa ni wataalam wa kutengeneza Website (tovuti) sawa na bure wengi wao ni matapeli hawafai. Nimekutana nao kama 4. Wamo wakenya na watanzania. Majina wanayo yatumia ni Mediapix, Datazone technology... na tovuti wanazo uki google utawaona. Wao wanataka kila kitu online hawana ofisi wala nn.
Hawa vijana wanakwambia lipia Hosting na registration tu bei inaanzia 100,000-250,000. Kwanza hawana ofisi wanakwambia location ya ofisi ambapo haipo. Wanakwambia atakutengenezea utalipia akimaliza. Anakuwekea demo kwa usiyejua utajua ni yenyewe. Anaanza kuomba pesa umpe zote ili amalizie. Kinachotokea anajiandikisha yeye kuwa admin. Kuna vitu anafuta anakwambia umeharibu umlipe arekebishe. Kama tovuti ni ya malipo ya bidhaa anakwambia kuna plugin za kununua na akufungulie acount ya benki ulaya irahisishe malipo umlipe... Hapo unampa hela ya kufungua acount, hela ya plugins za malipo namba ya sim ya ulaya atakupa ili ikusaidie kuweka kwenye acount ya benki inapo funguliwa.
Wana introduce vitu vingi halafu ukishamlipa haifanyi hiyo kazi anasepa. Ukimwambia unayo domain na hosting tayari anakwambia lipia pesa hiyo hiyo akutengenezee halafu anakwambia hiyo server iko slow sana akuhamishie kwenye server nyingine unamlipa tena. Ukimkimbia baada ya kulipia ukiangukia kwa mwingine anakwambia server haifai nakuhamishia kwingine ukalipie kwake...
Ninachotaka kuwaomba wadau msiingie kwenye hizo giza. Mmoja anaitwa Mediapix alitangaza hapa Jf na amefunga comments zote baada ya kutapeli watu kadhaa. Mjihadhari sana wako instagram, twitter, facebook na hapa jf ndio wana promote matangazo yao.
Ushauri wangu usimkubalie mtu asiye na ofisi physical ambayo utafika na umsainishe mkataba wa kazi yako mwanzo mwisho mpaka makabidhiano, vinginevyo ni hatari sana. Kwanza wanazo namba ambazo hawakuzisajili kwa majina yao wengine wamepata lipa namba za majina ya biashara na hawana ofisi wako mtandaoni hawaogopi
Wakija na ujinga kwenye huu uzi nitaweka namba zao na chats zao kuhusu kazi walizofanya hata kwa marsfiki 2 nime screenshot zote ili hata wakizifuta ninazo. Kaeni chonjo msidanganyike mkaliwa vichwa. Wengine hata hawajui kutengeneza website anakulia pesa zote hutakaa uione hiyo website.
Take care.
Hawa vijana wanao tangaza kuwa ni wataalam wa kutengeneza Website (tovuti) sawa na bure wengi wao ni matapeli hawafai. Nimekutana nao kama 4. Wamo wakenya na watanzania. Majina wanayo yatumia ni Mediapix, Datazone technology... na tovuti wanazo uki google utawaona. Wao wanataka kila kitu online hawana ofisi wala nn.
Hawa vijana wanakwambia lipia Hosting na registration tu bei inaanzia 100,000-250,000. Kwanza hawana ofisi wanakwambia location ya ofisi ambapo haipo. Wanakwambia atakutengenezea utalipia akimaliza. Anakuwekea demo kwa usiyejua utajua ni yenyewe. Anaanza kuomba pesa umpe zote ili amalizie. Kinachotokea anajiandikisha yeye kuwa admin. Kuna vitu anafuta anakwambia umeharibu umlipe arekebishe. Kama tovuti ni ya malipo ya bidhaa anakwambia kuna plugin za kununua na akufungulie acount ya benki ulaya irahisishe malipo umlipe... Hapo unampa hela ya kufungua acount, hela ya plugins za malipo namba ya sim ya ulaya atakupa ili ikusaidie kuweka kwenye acount ya benki inapo funguliwa.
Wana introduce vitu vingi halafu ukishamlipa haifanyi hiyo kazi anasepa. Ukimwambia unayo domain na hosting tayari anakwambia lipia pesa hiyo hiyo akutengenezee halafu anakwambia hiyo server iko slow sana akuhamishie kwenye server nyingine unamlipa tena. Ukimkimbia baada ya kulipia ukiangukia kwa mwingine anakwambia server haifai nakuhamishia kwingine ukalipie kwake...
Ninachotaka kuwaomba wadau msiingie kwenye hizo giza. Mmoja anaitwa Mediapix alitangaza hapa Jf na amefunga comments zote baada ya kutapeli watu kadhaa. Mjihadhari sana wako instagram, twitter, facebook na hapa jf ndio wana promote matangazo yao.
Ushauri wangu usimkubalie mtu asiye na ofisi physical ambayo utafika na umsainishe mkataba wa kazi yako mwanzo mwisho mpaka makabidhiano, vinginevyo ni hatari sana. Kwanza wanazo namba ambazo hawakuzisajili kwa majina yao wengine wamepata lipa namba za majina ya biashara na hawana ofisi wako mtandaoni hawaogopi
Wakija na ujinga kwenye huu uzi nitaweka namba zao na chats zao kuhusu kazi walizofanya hata kwa marsfiki 2 nime screenshot zote ili hata wakizifuta ninazo. Kaeni chonjo msidanganyike mkaliwa vichwa. Wengine hata hawajui kutengeneza website anakulia pesa zote hutakaa uione hiyo website.
Take care.