"HEKIMA" yako ipo upande upi?
Sijashawishika kuwaunga mkono hao "wapumbavu" kwa sababu baona mpango wao una asilimia kubwa ya kufa kibudu, ama hizo pesa kuishia kwenye chipsi kuku; Kuna "muvi" nyingi za kitanzania zinatoka kila wiki, lakini ni zinazofanikiwa kuuzika hazifiki hata asilimia mbili, watanzania wanataka kuona nani ameigiza, ray, kanumba, wolper na the like; sasa wao wanakuja na kipumbavu wajue kuna uwezekano mkubwa wa kupoteza, WAJIPANGE. Kwenye hii forum kuna nyuzii nyingi sana zinaongelea biashara za uzalishaji kwa mapana, lakini wewe na HEKIMA zako unaonesha huwa unaingia humu kwa bahati mbaya hasa unapoona heading za "kipumbavu" kama hii!....tumia muda kidogo kufanya research kwenye hizi kurasa utapata mambo mengi sana! TUMIA HEKIMA YAKO!