Paspii0
JF-Expert Member
- Apr 10, 2020
- 638
- 1,038
Katika jamii ya sasa, vijana wengi wanakosa mwelekeo na thamani, na hili linaweza kuathiri jamii nzima. Kama kizazi hiki hakitapewa uangalizi na mwongozo, tunaweza kujikuta na kizazi kilichopoteza mwelekeo, hata kabla ya kufika kaburini.
Vijana wanavua ndoto kwa kubeti, wakitegemea bahati badala ya juhudi na uvumilivu.Wafanyabiashara wanajua mbinu za kuhamasisha, wanajua vijana wanapenda mafanikio ya haraka, na hivyo wanakuza biashara ya kubeti kwa njia ambazo haziweki wazi hatari zinazohusiana nazo.
Vijana hawajali chochote, na kama kizazi hiki kisiposimamiwa vizuri, tutajikuta na kizazi bora zaidi kaburini kuliko kizazi cha sasa kinachoishi.
Vijana wanavua ndoto kwa kubeti, wakitegemea bahati badala ya juhudi na uvumilivu.Wafanyabiashara wanajua mbinu za kuhamasisha, wanajua vijana wanapenda mafanikio ya haraka, na hivyo wanakuza biashara ya kubeti kwa njia ambazo haziweki wazi hatari zinazohusiana nazo.
- Vijana wanabugia visungura baada ya kubeti, wakitafuta faraja kwa pombe, lakini wanajua fika kuwa wanajenga majeraha kwa afya zao.
- Vijana wanavuta shisha wakifikiri wanajifurahisha, lakini wanashindwa kuona athari zinazozidi kutengeneza vidonda kwenye mapafu yao.
- Mademu wanajikuta kwenye mtindo wa umalaya, wakiona njia rahisi ya kujipatia mali au upendo, lakini wanajenga vidonda vya kiroho na kimwili kwa kila hatua wanayochukua.
Vijana hawajali chochote, na kama kizazi hiki kisiposimamiwa vizuri, tutajikuta na kizazi bora zaidi kaburini kuliko kizazi cha sasa kinachoishi.