Vijana wa Hong Kong ni balaa

Vijana wa Hong Kong ni balaa

Gushleviv

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2011
Posts
3,457
Reaction score
5,325
Kama kuna yeyote anaefuatilia habari za kimataifa nadhani anaona kinachotokea sasa Kisiwani HongKong kundi la Vijana Waandamanaji wamevamia Jengo la Bunge na kuweka Kambi baada ya kutokubaliana na maamuzi yanayokuwa yakitolewa na Bunge hilo! Sasa najiuliza hivi Tanzania na hawa vijana wetu wanaoshinda kutwa kucha kugombea Likes na Followers Instagramu na kupiga umbea usio na manufaa wana uwezo wa kufanya mtiti kama huo??
Hapa najifunza kuwa Mabadiliko yanaweza kuletwa na Vijana na sio Wazee tuliowazoea kutupelekesha.

Nawasilisha!
D4D19365-5D78-46F4-BFB6-25C6D0F2181D.jpeg
1AA015DE-A2F9-4AFC-A062-CA8BC8E73A7D.jpeg
56F81913-C6A4-4429-B9CF-EA2B2699AE1E.jpeg
 
Hong Kong wana Elimu bora sana ni ngumu kufananisha na Nchi ambayo Elimu sio kipaumbele chao wao kila mwaka wanajadili na kutunga sheria ngumu za kuwakopesha vijana wasisome Elimu ya juu wakati wao hawakukopeshwa walisomeshwa buree kabisa ila kukopesha kwa wengine ni ngumu na inatengezwa hivyo ili wajinga na masikini wawe wengi waendelee kuwachagua bila kujali kuboresha maisha yao...
 
Kwa hiyo ukiandamana unapata nini?

Hong Kong wana shida zao na serikali zao.

Sasa Tanzania tuna shida gani na serikali?

Ya Hong Kong hayafanani na ya Tanzania.

Tanzania tuna amani na utulivu, kikubwa tu ni kufanya kazi
 
Kwa hiyo ukiandamana unapata nini?

Hong Kong wana shida zao na serikali zao.

Sasa Tanzania tuna shida gani na serikali?

Ya Hong Kong hayafanani na ya Tanzania.

Tanzania tuna amani na utulivu, kikubwa tu ni kufanya kazi
Umekuwa zezeta akili zimekutoka hadi unaamini unaishi sehemu yenye amani na utulivu!
 
Acha kuwaponza nyumbu wetu

hicho ni kina kirefu na mamba wakali kibao wamejazana...wataangamizwa!

kule akina Musiba wao wako wanaozea magerezani ilhali wa kwetu...wanatukuzwa na kukalishwa viti vya mbele
 
Umekuwa zezeta akili zimekutoka hadi unaamini unaishi sehemu yenye amani na utulivu!
Kama unadhani amani hamna, mbona huondoki?
Mbona huandamani?
Amani na utulivu upo ndiyo maana huondoki na huandamani.
Wote wanaokimbia nchi zao wanakimbia vita na njaa..
Tz hamna vita wala njaa. Ndiyo maana upo hapo ulipo
 
Kauli kama mtapigwa tu
Kipigo cha mbwa koko
Tutawqshughulikia NA MATUKIO KAMA
kifo cha akwilina n.k Ni mambo ambayo yanafanya watanzania wajifikirie Mara mbilimbili kuandamana
Inawezekana yanayoongelewa nyuma ya keyboard ni hali tofauti na uhalisia na ndiyo maana watu wkipigwa mikwara kama hiyo hujifikiria na kuogopa.
 
Hapa bongo kila MTU mpigaji anaweza akawambia mchangie pesa ya maandamano

Pesa za M4CA walikula kina John mrema na genge lake
 
Na ukiona wameingia kwenye maandamo basi hapo kuna masilahi ya wanasiasa yameguswa ndio wanaingizwa road kuyatetea.
 
Wenzetu hao wapo wakiona jambo hawalielewi wana take action ila sie kama tumeathiriwa na kulalamika tu yani huku kulalamika sio kwamba tunachukizwa bali ni kitu ambacho tunapenda kufanya na ndio maana huoni vitendo.
Hebu andamana kama haujauliwa? Hong Kong huwezi kuifananisha na Tanzania hata kesho kutwa. Vijana wanaandamana huku polisi wapo pamoja nao wanawalinda. Rudi Afrika andamana kama haujafa na kiongozi wa maandamano lazima atekwe.
Mtoa uzi umekosea sana kuifananisha Hong Kong na Tanzania
 
Hapa bongo kila MTU mpigaji anaweza akawambia mchangie pesa ya maandamano
Pesa za M4CA walikula kina John mrema na genge lake
Hata zile za Tetemeko la Kagera walilamba CCM. Yaani pesa za kuwasaidia wahanga wa tetemeko zinawekwa kwenye mfuko wa chama cha CCM. Bongo ni shida sana. Wapigaji wapo kila sehemu.
 
Unaweza ukaaanza wewe na mkeo tutakuja
Hata zile za Tetemeko la Kagera walilamba CCM. Yaani pesa za kuwasaidia wahanga wa tetemeko zinawekwa kwenye mfuko wa chama cha CCM. Bongo ni shida sana. Wapigaji wapo kila sehemu.
 
Back
Top Bottom