Vigogo CHADEMA wadaiwa kukiuka amri ya mahakama, wafunguliwa kesi

Vigogo CHADEMA wadaiwa kukiuka amri ya mahakama, wafunguliwa kesi

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
780
Reaction score
1,831
:
Katika hali isiyotarajiwa, viongozi waandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wanaweza kujikuta kwenye wakati mgumu baada ya uwepo wa taarifa zinazodai kuwa wamefunguliwa kesi nyingine ya jinai kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam wakidaiwa kukiuka amri ya Mahakama iliyotolewa Juni 10.2025

Inatajwa kuwa amri inayodaiwa kukiukwa inatokana na maamuzi ya Mahakama ya maombi Na. 8960/2025 ambayo msingi wake ni wa kesi ya madai Na. 8323/2025 iliyofunguliwa Mahakamani hapo na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar Said Issa Mohamed, Maulidah Anna Komu na Ahmed Rashid Khamis dhidi ya Bodi ya Wadhamini na Katibu Mkuu wa CHADEMA, kesi iliyopo mbele ya Jaji Hamidu Mwanga

Taarifa ilizozipata Jambo TV kutoka kwenye vyanzo vyake vya kuaminika imeonesha kuwa maombi hayo yamefunguliwa na waleta maombi kwenye kesi ya msingi ambao ni Said Issa Mohamed na wenzake wawili (2), ambapo vigogo wa CHADEMA wanaodaiwa kukiuka amri hiyo ni pamoja na John Wegesa Heche (Makamu M/Kiti Tanzania Bara), Amani Golugwa (Naibu K/Mkuu Tanzania Bara), Godbless Lema (Mjumbe wa K/Kuu), John Pambalu (Mkurugenzi wa Organization) na Boniface Jacob (M/Kiti Kanda ya Pwani na Mjumbe K/Kuu),

Wengine ni Pamela Maassay (K/Mkuu BAWACHA), Hamad Mussa Yussuf (Mkuu wa Idara ya Habari na Uenezi Z'bar), Gervas Lyenda (Mkuu wa Idara ya Habari), John John Mnyika (Katibu Mkuu), Bodi ya Wadhamini na Katibu Mkuu wa CHADEMA,

Kesi hiyo itakuwa ni ya pili kufunguliwa kwa vigogo wa CHADEMA, kesi ya kwanza kama hiyo ilitupiliwa mbali baada ya Mahakama kupitia Jaji Awamu Mbagwa aliyekuwa anasikiliza kukubaliana na hoja za upande wa utetezi kuwa waleta maombi walifungua kesi nje ya muda uliowekwa kwa mujibu wa sheria...
 
Chadema tunafeli wapi? Kwani said issa hana mke na watoto? It's about time tuwe aggressive kama enzi za Dr slaa na mabere marando!! Tulidhibiti sana element za namna hii otherwise chama kingekufa tokea 2013
Mke na watoto wanahusika vipi na CHADEMA?
 
Kwan hii kesi si aliwahii kuileta mahakaman na ikatolewa hukumu imekuwaje ikarudi tena kwenye mahakama Ile Ile na sio kwamba imekatiwa rufaa?
 
CCM ingejua kuwa jinsi wanavyoisumbua CHADEMA wanaipa matangazo ya bure wangeachana na huu ujinga.
Kama matangazo yanainufaisha chadema, kwa nini tena wasiendelee kutangazwa bure ili chadema iwe juu? Au hamtaki chadema iwe juu?

Huu upendo wa ghafla kwa ccm umetoka wapi?

Halafu chadema inashtakiwa na makada wake, tena siyo makada tu bali waliwahi kuwa viongozi wa ngazi za juu. Au wameisha hamia ccm au yeyote anaye dai haki ndani ya chadema ni ccm?
 
Kama matangazo yanainufaisha chadema, kwa nini tena wasiendelee kutangazwa bure ili chadema iwe juu? Au hamtaki chadema iwe juu?

Huu upendo wa ghafla kwa ccm umetoka wapi?

Halafu chadema inashtakiwa na makada wake, tena siyo makada tu bali waliwahi kuwa viongozi wa ngazi za juu. Au wameisha hamia ccm au yeyote anaye dai haki ndani ya chadema ni ccm?
Kwanza dont assume mtu anayeongea dhidi ya ujinga wa CCM ni CHADEMA.

Haya ni matumizi mabaya ya rasilimali za nchi, na pia hata hao CCM haiwasaidii. Wapambane kukubalika na wananchi sio kuhangaika na CHADEMA
 
Kwanza dont assume mtu anayeongea dhidi ya ujinga wa CCM ni CHADEMA.

Haya ni matumizi mabaya ya rasilimali za nchi, na pia hata hao CCM haiwasaidii. Wapambane kukubalika na wananchi sio kuhangaika na CHADEMA
Kwenye hyo kesi ya ugawanyaji wa mali, nani ccm hapo?
 
Kwenye hyo kesi ya ugawanyaji wa mali, nani ccm hapo?
Huoni upumbavu unaoendelea, Polisi nchi nzima wanakazana kutumia rasilimali zetu kukamata wanawake wa CHADEMA, mahakama ilishaondoa zuio, kwanini wanaendelea kutumia kodi zetu kupambana na kina mama?

Kukosekana kwa uwazi nayo ni shida, ningependa kujua ni pesa kiasi gani zinatumika kufanya huu ujinga
 
Sio katika hali isiyotarajiwa, bali ni hali iliyotarajiwa mahakamaccm zinapokea maagizo kutoka kwa mwenyekiti wa CCM

Hakuna namna itawaponya CCM, mahakamaccm, policcm kwa ujinga wanaoufanya hata wakimtumia msajiliccm kukifuta hiki chama kwa hila na kuwafunga wanachama, viongozi, na wafuasi haitosaidia .

Wametengeneza upinzani feki kwa mabilioni ukaitwa CHAUMMA ila umeishia kufeli vibaya sana.
 
Marehemu Ndugai alipowaapisha wakina Halima gereji kama wabunge wa Chadema ilikuwa wazi kuwa amekiuka Katiba ya nchi na utaratibu wa Bunge. Hata hivyo ilikuwa wazi kuwa watamaliza muhula pamoja na Mahakama kuangalia suala lao.

Kwenye hili ni wazi Chadema hawatapewa nafasi ya kujihusisha na siasa mpaka 2030. Inawezekana hizi kesi hazina mashiko lakini zitavutwa mpaka 2030. Na hamna Mahakama au nchi ya nje itakayolazimisha haki itendeke kwa Chadema.

Mbowe alilijua hili.

Amandla...
 
Mke na watoto wanahusika vipi na CHADEMA?
Yes CCM wanatumia Said issa kama leverage ya kudai maridhiano sasa chadema tunaweza mtumie mke wake na watoto wake kama bait aondoe kesi.

Tukiwachekea nyie mtakuja kukifuta chadema kimatani matani tu. Yaani tungeanza na huyu, alafu Mchome tunge solve 70% ya changamoto za ndani ya chadema
 
Kama matangazo yanainufaisha chadema, kwa nini tena wasiendelee kutangazwa bure ili chadema iwe juu? Au hamtaki chadema iwe juu?

Huu upendo wa ghafla kwa ccm umetoka wapi?

Halafu chadema inashtakiwa na makada wake, tena siyo makada tu bali waliwahi kuwa viongozi wa ngazi za juu. Au wameisha hamia ccm au yeyote anaye dai haki ndani ya chadema ni ccm?
Kwani we huoni ikiwa juu
 
Back
Top Bottom