Vifungo vya Kichawi Baada ya Talaka

Sniper

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2008
Posts
2,008
Reaction score
950
Ndoa ni taasisi yenye nguvu kubwa kijamii na kiroho. Lakini pale panapojitokeza kutokuelewana, mara nyingi matokeo yake huwa ni migawanyiko na hatimaye talaka. Katika mazingira mengi, talaka haimalizii tatizo pekee, bali huibua hali mpya ya maumivu, visasi na mara nyingine mashambulizi ya kiroho.

Baadhi ya wake, baada ya kutalakana, huchukua hatua za kichawi kumfunga mume wao kimaendeleo. Vifungo hivi huonekana katika sura mbalimbali: mume kushindwa kupata mafanikio ya kifedha, kuzuiwa kupata kazi nzuri, biashara kufa ghafla, au hata kukosa amani ya kimaisha. Hii inatafsirika kama “kifungo cha talaka” ambacho hutokana na hasira, wivu au hamu ya kulipiza kisasi.

Wakati ndoa na talaka zinapaswa kuwa mchakato wa kuamua njia bora za maisha ya baadaye, uchawi unaotumika kama kifungo unageuza talaka kikwazo kwa maendeleo.

Ni bahati mbaya sana baadhi ya wanaume wengi hawajalijua hili. Nawasanua, unapoona sintofahamu baada ya talaka, jikague, chukueni hatua.

Hii sio ramri chonganishi. Yapo kwenye jamii zetu na tunaishi nayo. Na vibinti vya sikuizi vimekuwa vichawi kuliko bibi zao!
 
Ndoa nadhani ilikuwa na nguvu kubwa kiroho na kijamii kama unavyodai kwa miaka ya nyuma huko!
Kwa miaka na siku za hivi karibuni Ndoa hazina Tena Nguvu na zinaendelea kupoteza Nguvu na umuhimu wake.
Familia za sasa nyingi ni za kihuni,unategemea zitatengeneza wanajamii bora?
 
Kwani mnalzamishwa kuoa(ga) jamani mpaka mpeane talaka?si bora uishi peke yako tu kuliko kuoa na kuachana kuolewa na kuachana, vunja hata uchumba kulikoni
 

Ukiwa na sababu ya kuacha mke ya usaliti we muache tu, ya huko mbele yatajijua mwenyewe, mwanaume ni kusonga tu mbele bila woga na kumtanguliza Mungu, usitutishe!
 
Kwani mnalzamishwa kuoa(ga) jamani mpaka mpeane talaka?si bora uishi peke yako tu kuliko kuoa na kuachana kuolewa na kuachana, vunja hata uchumba kulikoni
Watu hujuana vizuri baada ya kufunga Ndoa.
 
Uchawi kwa wenye Yesu unadunda!. Utapawata wanyonge wasio na mtetezi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…