Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,016
- 9,885
BAADA ya Serikali kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki, sasa imechukua hatua zaidi kwa kutoa muda hadi Aprili 8, 2021 kuwa mwisho wa matumizi wa vifungashio vya plastiki vinavyotumika kufungashia bidhaa ndogo ndogo yakiwemo maji, karanga na ubuyu.
Akizungumza katikaa ziara ya Makamu wa Rais kwenye Uwanja wa Tangamano mkoani Tanga, Mbunge wa Tanga Mjini ambaye pia ni Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Ummy Mwalimu alisema mwisho wa matumizi ya vifungashio hivyo ni Aprili 8 ambapo baada ya hapo atakayebainika anatumia vifungashio vya plastiki atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kulipa faini Shilingi laki tano.
Kauli hiyo imekuja baada ya hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mhandisi Samuel Gwamaka alipokaiririwa akisema kuwa wamebaini vifungashio hivyo vinazalishwa kwa wingi kwa ukubwa na vimekuwa vikitumika kama mifuko ya kubebea bidhaa sokoni.
Alisema katika kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la wazalishaji wa vifungashio vya plastiki aina ya “tubings” vinavyotumika kufungashia bidhaa kama karanga, ubuyu na barafu, vikiwa havina kibali kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na lakiri (seal) wala alama (label) kama kanuni namba tatu inavyoelekeza.
Akizungumza katikaa ziara ya Makamu wa Rais kwenye Uwanja wa Tangamano mkoani Tanga, Mbunge wa Tanga Mjini ambaye pia ni Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Ummy Mwalimu alisema mwisho wa matumizi ya vifungashio hivyo ni Aprili 8 ambapo baada ya hapo atakayebainika anatumia vifungashio vya plastiki atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kulipa faini Shilingi laki tano.
Kauli hiyo imekuja baada ya hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mhandisi Samuel Gwamaka alipokaiririwa akisema kuwa wamebaini vifungashio hivyo vinazalishwa kwa wingi kwa ukubwa na vimekuwa vikitumika kama mifuko ya kubebea bidhaa sokoni.
Alisema katika kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la wazalishaji wa vifungashio vya plastiki aina ya “tubings” vinavyotumika kufungashia bidhaa kama karanga, ubuyu na barafu, vikiwa havina kibali kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na lakiri (seal) wala alama (label) kama kanuni namba tatu inavyoelekeza.