Wingawinga
JF-Expert Member
- Oct 31, 2021
- 621
- 1,524
- Thread starter
- #381
Heheheehehehehe na Last name yangu umeitaja hapo ila ndio hivyo mambo ya kimya kimya .Kweli hao bakirane ni kina Benjamin na hao Bakilana nadhani mmoja aliita PhilipWaliokaa pembeni ya Oysterbay Primary ni akina Bakirane, sio bakilana. Akina Bakilana walikaa kule karibu na lilipoanzia daraja la Tanzanite.
Kwa kina Bakirane walikua wanafuga Ng'ombe pale kwao na ile Isuzu KB double cabin tulienda nayo sana kuchukua majani shamba.
Enzi hizo huwezi ishi au pita pita mitaa ile usiwajie akina Kafipa, Apson, Kejo, Kitomari, Mtui, Cathless, Faraji, Kamuzora, Warioba, Mengi, Kihampa, Ngamilo, Ngalawa, Malecela, Bakilana, Bakirane, Ligate, Usungu, Mtui, Kotta, Mpembe, Maliti, Ntukamazina, Mahiga, na wengineo, akina Malocho na Mang'enya waliishi Chole road huko na Akina Typhon Maji. Majina ni mengi sana ngoja niachie hapo.