Vifo vya vijana hawa miaka 80 na early 90 huko ushuani, Oysterbay

Makatta nilikuwaga nasoma tangazo la familia gazeti la Uhuru wkt wa kuadhimisha siku ya kifo chake. Walikuwa wanaweka hadi picha enzi hizo. Sasa wivu wa kuishi Oysterbay ndiyo visababishe kijana kurushwa kutoka ghorofani? Hizo siyo sababu zenye ushawishi au nguvu za kutosha za kufanya mauaji ya kinyama kama hayo.
Ebana ume nikumbusa kitu, ngoja nikupe hii sad story halafu ndio nije ni kuchane kwa wivu wako ka watoto wa kishua .
Baada ya Makatta kuwawa, tulikuwa na famili friends zetu hao walikua wanakaa mtaa wa Ethiopian cresent and Winding , kwenye hiyo familia Baba yao alisha fariki ( tena naye Kifo cha kutatanisha tetesi alikuwaga judge or hakimu sikumbuki vizuri ). katika hiyo familia kuna mabinti kama 4 na mvulana mmoja.
Suku Makatta amefariki ndio ikabidi kuweka tangazo la kifo kwnye radio na gazeti, Sasa siku nime kaa nyumbani, akaja mmoja wa hao sisters akaniuliza ,kuna gazeti la leo ? nikamjibu ndio , akaniambia wametoa tangazo la Makatta naomba niletee nione, nikaingia ndani nika mletea , kipindi hcho sikumbuki kama nina jua kusoma au la , basi akaaza lisoma kwa sauti na ninakumbuka aksomasehemu ya hilo tangazo ikisema "Baada ya kuwawa kikatili ghorofani" .
Kinacho sikitisha ni kwamba bila kujua ni kwamba naye baada ya muda dada yake anakuja uwawa kwa kurushwa ghorofani wao nao wakatangaza kwenye gazeti hivyo hivyo kusema "Baada ya kuuwawa kikatili ghorofani " ,yeye aliitwa Adelide dada yake aliye uwawa aliitwa Angelica , nadhani kama ulisoma tangazo la makatta utakumbuka kwamba kuna sehemu ilisema "baada ya kuwawa kikatili ghorofani "
 
uzi safi sana.

Niliingia Dar kwa nguvu zangu. Nikaenda Ulaya kwa juhudi zangu. Lakini hainifanyi nichukie waliobahatika kuishi maisha mazuri ambayo mpaka leo wapo nostalgic. Ndo dunia ilivo……jamii ina matabaka.

kama hukuishi ushuani the best you can do, tengeneza mazingira wanao wayaishi hayo maisha. Otherwise hatuwezi kuwa Sawa.
Ubarikiwe sana aisee, well said.
 
Mada tamu. Zamani watoto wa kishua ndio walikuwa wanatingisha miji.

Now days zama zimebadilika. Watoto wa uswazi wenye vipaji ndio wanatingisha miji.

Diamond platnumz kaja ku change the game.

Kina millard ayo wanatingisha nchi kuliko watoto wa vigogo

Harusi ya nandy na billnass inafunika harusi za watoto wa matajiri wakubwa na hata watoto wa marais
Usisahau pia hao mastaa wanapata sana promo na social medias na hiyo inapromote pia kazi zao. Sasa baadhi ya wa kishua na matajiri wengine wanapenda faragha.So ni rahisi harusi ya Nandy, Zamaradi au Wolper kutrebd maana online tv kama zote mpaka mabango ya barabarani! but hao wenye hela zao utaona tu kwenye page za watu kama maMC fulan kapost na labda wanafamilia.
 
Makatta nilikuwaga nasoma tangazo la familia gazeti la Uhuru wkt wa kuadhimisha siku ya kifo chake. Walikuwa wanaweka hadi picha enzi hizo. Sasa wivu wa kuishi Oysterbay ndiyo visababishe kijana kurushwa kutoka ghorofani? Hizo siyo sababu zenye ushawishi au nguvu za kutosha za kufanya mauaji ya kinyama kama hayo.
Nirudi sasa kwnye kukuchana wewe , hebu fikiria, hapa tuu hunioni na wala hunijui , ila story zangu za Obay na ushuani zina kukera kupita kawaida , je ungenijua na ninakutanulia wakati wewe una saga jiwe, si ungeniua kabisa ?
Hilo ndio suala sasa , Vijana a Obay tulikua na ujiko sababu baba zetu waliku ana hadhi , ina wezekana mfukoni hatuna pesa , ila ile tittle ilikua sio ya mchezo, so mademu walikua na shobo na sisi , kumbuka enzi hizo haijalisi una hela mradi baba yako ni fulani na una endesha gari lake , hauna haja ya kuhonga sababu wote tulikua tuna date naa ,nao kwao wako vizuri , hivyo tulikua hatuna haja ya matanuzi ya pesa ni magari ya wazazi tuu .
Hivy mademu wa Upanga wali leta shobo , so ina semekana Vijana wa Upanga hawakupenda mademu zao na shobo zao kwetu , ndio waka attack him usiku wa kwnye hiyo party iliyo fanyika Upanga na kumuua , siamini kamwa lidhamiria kama ni wali mburuza maana story ni kwamba wali mburusa ipo pia ila kama wali mrusha badi wali dhamiria kumuua , sasa nadhani umeelewa .
 
Usisahau pia hao mastaa wanapata sana promo na social medias na hiyo inapromote pia kazi zao. Sasa baadhi ya wa kishua na matajiri wengine wanapenda faragha.So ni rahisi harusi ya Nandy, Zamaradi au Wolper kutrebd maana online tv kama zote mpaka mabango ya barabarani! but hao wenye hela zao utaona tu kwenye page za watu kama maMC fulan kapost na labda wanafamilia.
Nikweli wote hao kina Diamond haya matanuzi ni promotins za makampuni wao wenyewe hawana pesa hiyo , na hawatumii hata centi .
 
Alikua ni mama tuseme sababu alianza kazi toka wazazi wameoana akiwa msichana , hivyo akaweza nunua nyumba huko Msasani na akaolewa na kuw ana familia ingaw abado alikau ana fanua kazi home, Servant Quarter ilikuw ana vyumba viwili alikua hoseboy na kuna ndugu mwingine aliishia hapo ,
Okay nilidhani ni kama Jamaa yangu tulisoma nae, kuna siku alituambia wana mfanyakazi mzungu (Sijui hio Work Permit ya kuja kufanya kazi za ndani alipewa na Nani)...

Anyway to each their own......
 
uzi safi sana.

Niliingia Dar kwa nguvu zangu. Nikaenda Ulaya kwa juhudi zangu. Lakini hainifanyi nichukie waliobahatika kuishi maisha mazuri ambayo mpaka leo wapo nostalgic. Ndo dunia ilivo……jamii ina matabaka.

kama hukuishi ushuani the best you can do, tengeneza mazingira wanao wayaishi hayo maisha. Otherwise hatuwezi kuwa Sawa.
Sure classess zipo kila mahali duniani hata kwenye dini mtoto wa askofu mkuu au shekhe mkuu atakwa tofaut na wa vyeo vya chini kwenye hiyo dini
 
Yes ndio hapo nadhani sasa hivi kuna zile towers Uhuru Heights, unajua kisa kilikuaje? ni kweli wali mrusha au wali mchoma kisu? Hata huyo Makatta was a hasomeboy , kwenye msiba, wa mama zetu walikwenda huko kwenye msiba , walipo rudi wakawa wanashangaa wakiuliza why wasichana walivyo kua wana zimia msibani ,waka hawaelewi ni kwa nini , kumbe mademu wali kua na shobo naye kinoma.
Umesahau ajali nyingine iliyo uwa pale kaunda yaani ile pickup double cabin ilijaa vijana wametoka disco upanga kukunja kulia kuingia kaunda walikunja kubwa wakapamia kisiki nje ya nyumba ya brig. Mkisi ule upande wa kushoto ukiingia kaunda, Mmoja au wawili walizimika palepale, ili pickup waliendesha watoto wa jaji, mi nilitokea muda mfupi baada ya ajali nikakuta kundi la vijana wamechanganyikiwa.
 
Upendo pekee hautoshi mkuu. Uwezo ndiyo kila kitu. Cha msingi kwenye hoja yangu ni kwamba wengi kama siyo wote wa generation yako mliyokuwa mnaishi Masaki na Oysterbay, sana sana Baba alikuwa mwajiriwa serikalini nyadhifa za juu kabisa na ndiyo sababu mlikuwa mnaishi maeneo hayo. Sasa kusomesha watoto Ulaya na Marekani kwa mshahara wa Serikali enzi hizo (na hata sasa) inahitaji zaidi ya upendo wa Mzazi. Au tuseme inahitaji rushwa na ufisadi?
Ni kweli ila kuna wazee wengine na familia zao walitoka huko sahv ni choka sana,so sad
Wengine hawakujipanga.....

Ova
 
Mkuu,

Kwanza si watu wote waliokaa Oysterbay walikuwa wafanyakazi wa serikali.

Kuna watu kama Dr. Andrew Mziray alikuwa na practice yake, hospitali yake. By some account, he was the best gynaecologyst in Tanzania.

Pili,

Mara nyingine ni kujua mambo tu.

Mimi nimekaa na mtoto wa huyo Dr. Andrew Mziray alikuwa amerudi likizo kutoka Marekani, tena visiwa vya Hawaii, katoka chuo.

Akawa ananihadithia baba yake anavyofanya kuwapeleka watoto chuo kwa scholarships za makanisa , NGOs za Marekani, na balozi za nje, anavyonunua magari makali kwa bei nafuu kwa kujua kuongea na mashirika ya kimataifa na balozi za nje, jamaa alinifungua macho sana kujua kwamba knowlege mara nyingine ni kitu muhimu kuliko pesa.

Kwa hivyo, si watu wote wamefanikiwa kwa kufanya ufisadi serikalini. Kuna wengi wameelimika na wakazitumia vizuri elimu zao ku network kimataifa na kufanya biashara halali.

Dr. Andrew Mziray ni mfano mmoja.

RIP.
Dr Andrew wa asa Estate au

Ova
 
Usisahau pia hao mastaa wanapata sana promo na social medias na hiyo inapromote pia kazi zao. Sasa baadhi ya wa kishua na matajiri wengine wanapenda faragha.So ni rahisi harusi ya Nandy, Zamaradi au Wolper kutrebd maana online tv kama zote mpaka mabango ya barabarani! but hao wenye hela zao utaona tu kwenye page za watu kama maMC fulan kapost na labda wanafamilia.
Hao wakina nandy na wengineo wanaishi tu kwa kujiumiza

Ova
 
Alafu isichukuliwe kuwa waliopata neema ya kuishi ushuani na baba zao waliokuwa na nafasi serikalini miaka hiyo kwamba sasa hivi life imewachapa; not at all na hata kama wapo basi ni wachache sana! Wengi bado maisha ni mazuri kabisa.
Mfano sisi hatukupata bahati ya kupelekwa UK or USA, ila ile exposure tu ya kuishi kwenye ile standard ya maisha ya ushuani inakuwa kama iliweka benchmark on how life should be! Sio sifa na isiwe siri, hapahapa TZ tuliweza kujua maisha yanapaswa kuwa namna gani and life is good tena pengine zaidi ya ilivyokuwa wazazi wetu. Mfano nakumbuka mzee wangu kwa nafasi yake he had 3 cars of his own, Peugeot 504, pick up ya Peugeot 404, na Ford CortinaL nakumbuka anaitumia Saturday na Sunday tu kwa mitoko binafsi! Gari za ofisini used to be Peugeot 505 ama Landrover 109 na hizo zina dereva!

Maisha ya sasa knowing standard inatakiwa kuwa namna gani, nje hayakosekani magari kwa namna yoyote na yawe ya standard flani sio tu chombo cha usafiri.

Angalizo: bitterness sio healthy u may end up injuring your internal organs.
 
Umesahau ajali nyingine iliyo uwa pale kaunda yaani ile pickup double cabin ilijaa vijana wametoka disco upanga kukunja kulia kuingia kaunda walikunja kubwa wakapamia kisiki nje ya nyumba ya brig. Mkisi ule upande wa kushoto ukiingia kaunda, Mmoja au wawili walizimika palepale, ili pickup waliendesha watoto wa jaji, mi nilitokea muda mfupi baada ya ajali nikakuta kundi la vijana wamechanganyikiwa.
Kama nakumbuka hiyo kitu ila nadhani hakuna aliye kufa, kwasababu nakumbuka kuna mshkaji mmoja alikua ana soma Tambaza, ana kaa mta wa Hill rod , nili kwenda kwao nikamkuta ana ma bandages na mapamba kabandikwa mwili wote akaniambia walipata ajali walikua kwenye pickp wanatoka nadhani sijui ilikua 7th flour kitu kama hicho , ila sikumbuki kama kuna kijana alifariki.
 
Hivi Max ndio kina Kafipa? Au namchanganya? Ila jina la mwisho Kafipa, either Max or Anthony jamani alikuwa akipita mtaa wa Ethiopia Crescent wasichana wanakimbia hatari maana mtaa ulikuwa na mabinti wazuri kweli.
max au mac tamka meki na antony wote ni kafipa, na wao walikuwa na dada matata sana
 
Alafu isichukuliwe kuwa waliopata neema ya kuishi ushuani na baba zao waliokuwa na nafasi serikalini miaka hiyo kwamba sasa hivi life imewachapa; not at all na hata kama wapo basi ni wachache sana! Wengi bado maisha ni mazuri kabisa.
Mfano sisi hatukupata bahati ya kupelekwa UK or USA, ila ile exposure tu ya kuishi kwenye ile standard ya maisha ya ushuani inakuwa kama iliweka benchmark on how life should be! Sio sifa na isiwe siri, hapahapa TZ tuliweza kujua maisha yanapaswa kuwa namna gani and life is good tena pengine zaidi ya ilivyokuwa wazazi wetu. Mfano nakumbuka mzee wangu kwa nafasi yake he had 3 cars of his own, Peugeot 504, pick up ya Peugeot 404, na Ford CortinaL nakumbuka anaitumia Saturday na Sunday tu kwa mitoko binafsi! Gari za ofisini used to be Peugeot 505 ama Landrover 109 na hizo zina dereva!

Maisha ya sasa knowing standard inatakiwa kuwa namna gani, nje hayakosekani magari matatu kwa namna yoyote na yote ni ile ooops gari hiyo sio chombo cha usafiri.

Angalizo: bitterness sio healthy u may end up injuring your internal organs.
Natamani ni kurushie dola mia aisee , point kubwa sana
 
Miaka ya 80 wakati tuko watoto ilitokea misiba ya vifo vya utatanishi, sijui kama ni utatanishi au ni kwasababu nilikuwa mtoto hivyo sikuelewa mwisho wa hizi case .

Kifo ha kwanza kilikuwa cha kijana mmoja alijulikana kama Makatta Makatta, huyu inasemekana aliuawa kwenye party maeneo ya Upanga, kwa kurushwa ghorofani, je kisa kamili kilikuwaje?

Kifo cha pili ni dada mmoja alijulikana kama Angelica Rwechungura, huyu aliuawa kwa kurushwa ghorofani maeneo ya Hotel inaitwa Entience (sina uhakika na jina la hotel), je hili tukio lilikuwaje?

Kifo cha tatu kilikuwa cha kijana mmoja alijulikana kama Robert Cathless, yeye naye inasemekana alirusha ghorofani maeneo ya mjini, je naye hili tukio lilikuwaje?

Wote hao vijana walikuwa ni vijana wanaishi Oysterbay na wengi wetu hatujui kama watuhumiwa walikamatwa au case ziliishaje, zaidi ya wauaji wa Angelica ambao walikamatwa na case ilifanyika ila hatujui mwisho wake ulikuaje, mwenye taarifa naomba atujuze zaidi.
Ettiennes hakuna ghorofa la kurushwa mtu akafa.

Labda aliuliwa akatupwa hapo.

Nimecheza disco kwa Mgiriki hapo miaka 1970 - 73.
 
Back
Top Bottom