Video: UHUNI WA WATU WA MIZANI

Video: UHUNI WA WATU WA MIZANI

Pole sana ndugu ktk kitu kinatusumbuwa ni hili swala la Mizani, sisi tulio kwenye hiyo sekta ya usafirishaji tunalitambua hili unalolisema na hao jamaa wamejivika utakatifu flani kwamba hawakosolewi na hata hizo number wameweka hapo ofisini kwao hazina msaada wowote. Na ukiwapeleka kwenye mamlaka nyingine utajibiwa hao ni Kitengo kinacho jitegemea hakifungamani na upande mwingine basi unaishia kuilipa faini yao huku unanungunika mwenyewe.
 
Hivi inachukua degree hawa wajinga wa mizani kutambua kwamba huo mzani una calibration error, unatakiwa uwe calibrated upya?

Ilishanitokea airport. Mie nina scales yangu nyumbani, nikapima mzigo zikawa kilo 20. Airport wakasema nimezidisha kilo 2. Nakisema haiwezekani tukaanza kubishana. Nikaweka kwenye mzani wa pili ikaonyesha kilo 20. Nikawaambia nendeni shule mkaongeze elimu ya kupima mizigo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom