Leo JPM kaonekana akilialia kuhusu mikataba ya ''kijinga na kishenzi'' iliyosainiwa na wanaCCM wenzie, ambao almost wote bado wapo hai, kicking and enjoying free oxygen mtaani. Hawagusiki. Ile siku akima Mruma wanasoma report yao ya Makinikia part2, kwa mbwembwe na jazba kubwa, JPM aliagiza wote waliotajwa wakamatwe na kuhojiwa. Mpaka leo, wapo nje wanadunda kwa raha zao.
Huyu inasemekana eti kuna jora za sare za jeshi letu tukufu zilikutwa kwenye godown anayoimiliki (sio chumbani kwake) as well as sample ya mihuri ya jeshi kukutwa ofisini. Kesi ni uhujumu uchumi!. Waliohujuma uchumi wetu mpaka sasa Bombardier ipo korokoroni nao vipi? Hao wa makinikia na hao wa mikataba ya TANESCO inayohujumu uchumi nao vipi?