Video: Maajabu ya kisima kinachowaka katika ya maji

Video: Maajabu ya kisima kinachowaka katika ya maji

Fanyia kazi ya kutuambia specific place kilipo hicho kisima...maana kuna watu wako huko lkn hawakijui


Hadi sasa nimeshauliza watu wawili wakazi wa Kifanya wanasema hicho kisima hakuna au may be ni kipya/cha hivi karibuni kwa watu wa hapo hajui kipo wapi!

Pia hiyo sio gesi ni volcano hiyo
 
Kwa ushahidi wa picha khabari ni sahihi na ushahidi wa wakazi wa huko eneo si sahihi.
 
me nilisema tangia mwanzo kuwa nawaswas na eneo hilo kama lipo tz.. hilo eneo lingekua hapa tz bas ni jipy halina wiki.. magazet ya udaku yangekua yashajipatia habar ya kuuza na habar zingeenea..
kwa uelewa wangu kunauwezekano mkubwa wa eneo hilo kuwa karibu na active volcano kwa chin.. hivyo kuna clerk ambayo inafika moja kwa moja hadi hapo..
au ndo hiyo natural gases znareact na kutoa flames
 
Hadi sasa nimeshauliza watu wawili wakazi wa Kifanya wanasema hicho kisima hakuna au may be ni kipya/cha hivi karibuni kwa watu wa hapo hajui kipo wapi!

Pia hiyo sio gesi ni volcano hiyo
Mkuu hiyo ni gas% sema yawezekana imechanganyika na gas zingine ndo maana inawaka. Natural gas sometime huwa sio pure. Huwa na gas zingine ambazo zikikutana na oxygen zina explode na kuwaka.
 
Mkuu hiyo ni gas100% sema yawezekana imechanganyika na gas zingine ndo maana inawaka. Natural gas sometime huwa sio pure. Huwa na gas zingine ambazo zikikutana na oxygen zina explode na kuwaka.
 
Nahisi itakuwa mitaa ya moro vijijini hasa matombo mgeta, antonio nugaz alisharusha kwa tv vitu ka hivyo ,maji yanachemka ila majani still yapo evergreen aisee!!
 
HAPO UTAKUTA CHINI KUNA MALI NYINGI SANA SASA HUO MOTO NI ULINZI KUWA HAKUNA ATAKAYEWEZA KUFIKIA MALI HIZO MPAKA IDHINI YA WAZEE


LA SIVYO UTAKUTANA NA KAPPA


Kappa_water_imp_1836.jpg

e17ddc7a39344e595bda9191c0866653.jpg
 
Hiyo ni hot spring mkuu ni vitu natural ukiona hivyo ujue kuna ufa kuelekea earth core, hivyo usishangae siku mlima kama kilimanjaro ukatokea hapo

ebana ndo mwalimu wako wa geography alichokufundisha hicho au ulimuelewa vibaya
 
Hapo panaonekana panajulikana na wanajamii wa mji huo,Kunaonekana kuna bomba la chuma pia panatumika na watu kunufaika na kisima hicho.
 
Hapo lazima kumejaa uchawi na matambiko ya kutisha.

Naona kushoto kuna kitu kama kiti kikubwa!. usikute wabena wanaabudu hapo.

Na wewe ulikwenda huko mtoni usiku kufanya nini?

Serikali yenye akili ingeshachunguza na kufanya documentaries mbali mbali juu ya sehemu hiyo ili kujua historia na mwelekeo wa hali hiyo kwa maisha ya sasa na baadaye ye viumbe hai katika eneo hilo.

Ama ninashangaa kwa nini hiyo sehemu haijahifadhiwa vizuri kama sehemu chache za mambo tofauti ndani ya nchi.
Kwa mtu ambaye ana shule haba uchawi ni kitu asichokijua!
Kwa taarifa yako sehemu nyingi za Njombe ziko sehemu ambazo ni volcanic.
Hapo lazima kuna methane gas au flammable gas inayotoka chini ya ardhi na kuwaka moto.

Upande wa pili wa Njombe yaani milima ya Livingstone kuna mlima unsitwa Kyejo, mlima ambao unatoa gesi ya carbon monoxide na dioxide.

Gesi hiyo inavunwa na Tanzania Oxygen Ltd kutengeneza nilu.
 
Nami nimetumiwa nimeambiwa ipo Kifanya mkoani njombe, lakini kila nikiwauliza Kifanya Sehemu gani hawanipi jibu, Mlioko Kifanya ndio inabidi mukitafute hicho Kisima Kama kweli Kipo Kifanya hapo.
wenye akili tumeshahitimisha hii thread yako
 
maeneo wanayochimba gas hadi maji ya bombani ndani huwa yanaweza kuwaka moto. njia ya kuchimba wanaita fracking husababisha nyufa ndani ya ardhi na gas huchanganyikana na underground water. kifanya hawachimbi gas.
 
HAPO UTAKUTA CHINI KUNA MALI NYINGI SANA SASA HUO MOTO NI ULINZI KUWA HAKUNA ATAKAYEWEZA KUFIKIA MALI HIZO MPAKA IDHINI YA WAZEE


LA SIVYO UTAKUTANA NA KAPPA


Kappa_water_imp_1836.jpg

e17ddc7a39344e595bda9191c0866653.jpg
mkuu hyu ndo kappa au? ni nan haswa? mana km iko historical hv
 
Hiyo kitu imesha wahi tokea kifanya nadhani miaka kama 10 iliyopita pembezoni mwa mlima kifanya.... Volcano eruption
 
Nimeishi kifanya mwaka mzima ndo nasikia leo kwenye hui uzi.ni uongo uliotukuka
 
Back
Top Bottom