Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Hii ndio hali ya utawala wa shari, mabavu na wenye kukusudia kuchafua amani ya Tanzania tulivu hata kama ina umasikini na ujinga ila utulivu ulikua kiunganishi kwetu. Lakini cha ajabu umasikini hawajaondoa, ujinga hawajauondoa, wanapamnana kuiondoa CHADEMA kwa shari, kwa vita kwa fujo na ikibidi kuua wanaCHADEMA wote kama sio kuwafunga.
Huko Rombo mkoani Kilimanjaro kundi la vijana wa UVCCM wakiratibiwa na viongozi wao wameamua kuzipoka ofisi za CHADEMA bila woga na kupaka rangi za CCM huku kukiwa na ulinzi, kwamba asiwepo CHADEMA KUSOGEA.
Naona vile CCM wamechoshwa na amani ya nchi hii, na hata haya yanavyotendeka husikii viongozi wakuu wa kiserikali wala kiulinzi wala kichama CCM wakikemea zaidi sana wanayafukizia mafuta ya petrol na kuyaita matendo ya kizalendo.
Taifa linazidi kupasuka pasuka, hii ni hatari ya kesho kwa taifa letu. Siku zozote CCM inapaswa kubeba lawama