Nimeamua kuweka video hapa ili watanzania muweze kuamua kama kweli Mhe. Lema alihusika na mauwaji na kuchochea vurugu chuo cha uhasibu Arusha kama mkuu wa Mkoa wa Arusha (pigs kazi lema usiogope mtu)
Nimeamua kuweka video hapa ili watanzania muweze kuamua kama kweli Mhe. Lema alihusika na mauwaji na kuchochea vurugu chuo cha uhasibu Arusha kama mkuu wa Mkoa wa Arusha (Mulongo) anavyodai.
Part I
[video=youtube_share;_z-Cl4nNva0]http://youtu.be/_z-Cl4nNva0[/video]
Part II
[video=youtube_share;Y1Zy44AokSw]http://youtu.be/Y1Zy44AokSw[/video]
Wenzako wote video haifunguki wewe umeibuka na kutema kauli zako tata!! na mapovu tu humu. Au umetumwa? Mbona hueleweki? Kuwa serious ndugu acha uongo..Huku ni kwa Magreat thinker. Uongo peleka facebook sio humu..Au wewe una link yako nyumbani.?hapo umewabamba mkuu kila kitu chajieleza na wanaumbuka sasa
Mbona mi naicheki vizuri tu tena kwenye simu?Wenzako wote video haifunguki wewe umeibuka na kutema kauli zako tata!! na mapovu tu humu. Au umetumwa? Mbona hueleweki? Kuwa serious ndugu acha uongo..Huku ni kwa Magreat thinker. Uongo peleka facebook sio humu..Au wewe una link yako nyumbani.?
Usiogope. amini kuwa kila kwenye vita MUNGU yupo upande wa hakiUwiiii huyu mkuu wa mkoa amesema mmetaka kuonana na serikali na ameenda hakusema kitu, bali kurushia wanafunzi mabomu yanayotoa moshi. Uwiii ona walivyokimbia wassiumie au kufa
mapolisi, ffu wamejaa kibao utadhani kuna fujo na walikuwa wametulia wanafunzi wanasubiri kusikiliza anasema nini
jk nchi imekushinda kwa kweli hata wanafunzi,
mungu tuepushe vita nchini, naona mnataka kuua wananchi na kuwa mashujaa huyo mkuu wa mkoa ulimtoa wapi ameenda anaongea na hasira sanaaa kama anataka kupasuka.
Aibu sana serikali.
Mbona jk hasemi chochote kwa majanga ya hawa watu wake?
Sijawahi kusema maneno haya ila shame on you mkuu wa mkoa. Achia kazi haikuwezi
poleni wanafunzi. Hii ni video ya pili, nisingeangalia nisingedsema haya yote
uwiiiiii, what?????? Just like that??????
Makamanda vedio inafunguka na kusikika vizuri mno ila hakikisha una GB za kutosha. Mimi hapa natumia 5GB!
Hii video imemuumbua Lema. Kwa hakika hapa Lema hakwepi. Ni wazi kwamba alichochea vurugu, na amemdharau mkuu wa mkoa.
Kwanini yeye asingeacha hayo maneno yasemwe na mkuu wa mkoa mwenyewe? Haya bwana ameyatafuta mwenyewe. Mwanzoni alifanya vizuri sana na ameongea maneno ya msingi sana. Lakini kuanzia baada ya mkuu wa mkoa kufika, Lema hakupaswa kuendelea kuwa msemaji tena.
Kwa busara za kawaida kabisa, alipaswa amuachie mkuu wa shule na mkuu wa mkoa waseme wanayotaka, lakini kitendo cha kusimama na kuwatangazia alichokisema mkuu wa mkoa na kuwatamkia wanafunzi kwamba hawa ndiyo aina ya viongozi tulionao na nini ambacho mkuu wa mkoa alipaswa kufanya hakikuwa sawa kabisa. Kwanza alipaswa aheshimu uamuzi wa mkuu wa mkoa kufika eneo la tukio.
Katika hili sitaweza kumtetea Lema. Amelikoroga.