VIDEO: Kafulila azomewa na kushushwa jukwaani, Kigoma

VIDEO: Kafulila azomewa na kushushwa jukwaani, Kigoma

bayumiJR

Member
Joined
Aug 28, 2015
Posts
36
Reaction score
36
DAVID ZACHARIA KAFULILA mbunge kijana wa Jimbo la Kigoma Kusini kwa tiketi ya Chama Cha NCCR- Mageuzi ambae alipata umaarufu mkubwa katika siku za hivi karibuni baada ya kufichua Ufisadi mkubwa wa Escrow na kupelekea Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji fredrick werema kung'oka na Serikali kuyumba amepata aibu ya Mwaka akiwa nyumbani kwao Kigoma.

LABDA ni kulewa Umaarufu, ama labda ni kukosa ukomavu na ujana, Mbunge huyo machachali alisimama kwenye jukwaa akihutubia na kuwaambia watu wa kigoma kuwa hawana Haja ya kuanzisha Chama Cha Siasa, kama wanahamu ya kuanzisha Chama wanaweza kuanzisha Chama Cha MAWESE na MICHIKICHI.

Baada ya Kauli hiyo ya Kafulila, Maelfu ya wananchi waliojitokeza Mkutano hapo waliona wamedharauliwa na kukejeliwa na Mbunge wao huyo na walianza kuzomea na kumwambia kuwa UKAWA hawana chao Kigoma, jambo lililomfanya kafulila kushindwa kuongea na kushuka jukwaani.

 
Last edited by a moderator:
Mchezo wa siasa ni mbaya sana. Si kama mpira wa miguu. Ukiteleza kidogo tu basi unapoteza wapiga kura wengi sana. Kafulila kujifanya mjuaji ndo kumemponza. Jeuri na kiburi kitakatisha ndoto yake ya kutetea ubunge wake
 
hii kali maskini tumbili mtoto .ukawa imekwisha kigoma ndio maana machal alikimbia mapema
 
  • Thanks
Reactions: R.B
mmmh nahao wananchi kuambiwa wasianzishe chama cha siasa ndio kudharauliwa? au watu hawaelewi lugha nibi
 
Tena kafulila mpuzi sana najua atapita hapa kuna binadam jimboni kwake tangu uchaguzi wa 2010 Hawajawai kumuona kule, anakoishia ni kwao nguruka,kazuramimba,uvinza, kusini ya mwambao wa ziwa kama hawatambui, NABADO VIJANA WANAKUSUBILIA KULE
 
Mda wa kuchimba dawa na kunywa maji kwa magamba unaisha kesho, safari iko pale pale Captain Lowasa anaongoza. Maccm mlipata kaupepo, kanafifia sasa.
 
Maajabu:Mpinga ufisadi ananadiwa na FISADI LOWASSA....
 
Hii hataei sana. kwa wanaukawa.
 
Ukiwa muongo jihadhari na video kwani hata mtoto hatosadiki ulichokiandika na kinachoonekana.Acha ushabiki wa kijinga kwani hakuna uhalisia na ulichosema.
 
yan anarekodi afu anasema tukapige chin hahaaa ccm mwaka huu mtakufa kifo cha mende
 
1441397987085.jpg 1441398020601.jpg
 
Timing tu imefanyika hapa. Inavyoonekana kuna watu ambao ni wanachama/ mashabiki wa chama kingine (labda ACT), au wapinzani wake wengine wa kisiasa, wameenda pale kwa ajili ya kumtafutia dosari na kumshusha umaarufu. Hata alichokisema binafsi sikioni kama kina ubaya wa kufanya watu wamzomee. Nadhani ni mpango tu ulikuwa unatekelezwa. Sidhani kama kauli kama hii ingesemwa na labda zitto, au mbowe au hata Lowasa, wangeweza kuzomewa hivyo.

Ila tukubali au tusikubali, Kafulila ni miongoni mwa wabunge wazuri wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kutetetea maslahi mapana ya taifa, ila kwa vile siasa za Tanzania ni za kishabiki, kutafutiana visa na kuchafuana basi mwisho wa siku tunachagua viongozi wasiokuwa na uwezo wa kufanya kile wanachotakiwa kukifanya. Wale wazuri wanatafutiwa njia za kuchafuliwa na hatimaye taifa linakosa viongozi wazuri.

Wataalamu wa uchumi wanaamini uongozi ni "factor of production" ingawa sociologists wanachukulia uongozi kama "prestige", watu wanatafuta kuheshimiwa tu. Tufanye maamuzi sahihi katika uchaguzi kwa maendeleo ya jamii zetu na taifa kwa ujumla.
 
ACT wanatetemeka,zitto bunge atalisikia tu
 
hakuna kwenye iyo video walipozomewa ao ulio wataja.umejilekodi mwenyewe ukizomea tena ata aliyekuwa anaongea sio kati ya ao ulio wataja.inshort umezomea wewe na siyo hadhira yote
 
Back
Top Bottom