PiedPiper77
Senior Member
- Jan 8, 2025
- 180
- 223
Kuna wakati Watanzania tunaanza kuamini Freeman Mbowe alizungukwa na vijana hatari sana huku yeye akila na kulala nao.
Kama wanavyojitambulisha hawa vijana wanaojiita G55 ni vijana toka team iliyojitanabaisha kuwa ni team Mbowe wakati wa Uchaguzi wa ndani ya CHADEMA mapema mwaka huu.
Kama vijana hawa au boss wao Mbowe walikuwa ni waasisi wa No Reforms No Election na leo ni hao hao wanatoka tena hadharani na kupinga "No reforms No Election" kwa kisingizio walikuwa wanatishia nyau tuu,
Nadhani hiki ni kiwango Cha Juu kabisa Cha Ujinga walichonacho hawa wanasiasa.
Hata hivyo, Hawa vijana wa G55 wanaharibu kabisa image ya Freeman Mbowe na kuwafanya Watanzania waamini kuwa Mbowe alikuwa anafanya michezo ya kuigiza mingi ili kujipatia chochote toka kwa Watawala kama hiki wanachokisema vijana wake ni Cha Kweli,