Video: Edward Lowassa na hali ya kisiasa nchini

Video: Edward Lowassa na hali ya kisiasa nchini

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,356
Anaongelea kuhusu Katiba mpya na Muungano. Anasema ni bora kuzungumzia kero za Muungano.

Anasema haamini kuwepo kwa serikali tatu bila kuvunjika kwa Muungano.

Anaongelea kuhusu shule za kata. Anasema japokuwa inadaiwa ni zake, hizo shule siyo zake bali alikuwa anatekeleza ilani ya CCM.

Anasizitiza elimu kwanza, siyo kilimo kwanza. Katoa mfano wa Tony Blair aliyeingia madarakani na kusizitiza elimu kwanza, elimu kwanza, elimu kwanza.

Anaonyesha masikitiko yake kuhuasiana milipuko ya mabomu Arusha. Pia anasikitika mpaka sasa waliohusika na hiyo milipo bado hawajakamatwa.

Anasema anahisi kuna watu wanatuonea "gere" kwa amani tuliyonayo, kwa utulivu wetu na kwa umoja wetu.

Kwa sababu bado haamini kama vyama vya siasa Tanzania vinaweza kuchukiana mpaka kuanza kurushiana mabomu.

[video=youtube_share;8iyJpDVHuRk]http://youtu.be/8iyJpDVHuRk[/video]
 
Hata akirekodi video kwa kumshirikisha Rose Mhando au hata Bahati Bukuku huyo kamwe sitampa kura yangu endapo CCM watampitisha kugombea Urais, mbona haongelei masuala ya Richmond na hasara ambayo tumeipata kama taifa?
 
Mzee wa mapesa

"To know the enemy is half the victory"
 
Anaposema kuwa 'walipokuwa wanafikiria kuandika Katiba ...' ana maana gani? Je ni kuwa yeye hakuhusika katika maamuzi hayo hasa akiwa kiongozi katika Chama chake?
 
Maganga Mkweli; Mkuu, hao wanapewa hela hivyo usiwalaumu.Uzuri wake ni kwamba attribution yake inaeleweka kwamba ni "Waziri mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa kampuni hewa ya Richmond Mhe Edward Lowassa..."
 
Last edited by a moderator:
Watoto wameshughulikiwa vizuri na akina mama nao wameshughulikiwa vizuri....Anaaishi nchi gani huyu hadi kutoa kauli ambayo haina ukweli wowote kuhusu watoto na wanawake!?

Mhhhh! Muungano ukivunjika watakaoumia zaidi ni watu wa chini!!!!


Mhhhh! hakumtaja Mwalimu katika Viongozi waliomuamini!!!!!
 
Hata akirekodi video kwa kumshirikisha Rose Mhando au hata Bahati Bukuku huyo kamwe sitampa kura yangu endapo CCM watampitisha kugombea Urais, mbona haongelei masuala ya Richmond na hasara ambayo tumeipata kama taifa?

hilo ni suala la kuzungumzwa na ikulu siyo yeye.....alijiuzulu ili kuinusuru serikali na chama chake..."Kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya serikali yangu, nimemwandikia rais barua ya kuachia ngazi" au umesahau maneno yake bungeni siku anauiuzulu? ... serikali wala ccm hawajawahi kukanusha matamshi yake......ccm wote wachafu tu.
 
michango anayotoa ni 'marafiki wa Lowasa' ni akina nani?

ujenzi wa shule za kata umeacha madeni ya kutupwa Halmashauri
 
hakika nakwazika sana na neno "WAZIRI MKUU MSTAAFU"
alistaafu lini na wapi..?
Huyo ni muharifu kama walivyo waharifu wengine. Alistaafishwa kwa manufaa ya umma. Alipaswa kufikishwa mahakamani kujibu utumiaji wa madaraka vibaya na ufisadi.
 
Hao marafiki zake aliowataja Mwanza kuwa ndo watampa bilion moja kwa ajili ya "bomu linalotaka kuripuka" (vijana wasio na ajira) awataje kwa majina tujue ni akina nani? Na pesa zote hizi wanatoa wapi?
 
Yaani nikisikia jina lake natamani kujinyonga Mwizi mkubwa huyu... Anajisafisha misikitini/makanisani shwaaaini...~
 
Haki ya nani nimekumbuka wimbo wa msanii mmoja wa bongoflva "SHETANI AMESHIKA MSAHAFU NA BIBLIA ANAWAIMBIA MAPAMBIO WAO WANAMPIGIA MAKOFI" Revolutionary forever!
 
Anaposema sera ya KILIMO KWANZA imeharibu ELIMU anamaanisha nini? Kuuliza sio ujinga, msaada tafadhali.
 
Anaposema sera ya KILIMO KWANZA imeharibu mfumo wa ELIMU nchini anamaanisha nini? Kuuliza sio ujinga, msaada tafadhali.
 
Hahahahaaaaa! Alikuwa anatekeleza ilani ya ccm kuongeza division O katika taifa!!!
 
Lobyist wa kutupwa! Atueleze kuna nini ikulu? Je hana mkono yeye na rostam kwenye ugonjwa wa Mwakyembe?
 
Back
Top Bottom