PostGE2025 Video: DW waachia Ushahidi mpya juu ya mauaji ya Oktoba 29, 2025

PostGE2025 Video: DW waachia Ushahidi mpya juu ya mauaji ya Oktoba 29, 2025

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections
najua maumivu yenu ila mengine ni kusahau tu yapite!,watu washachinjwa na kuzikwa kusikojulikana hatuna uwezo wa kuwarudisha tena ni kuwaombea Mungu awape pumziko salama huko waliko.
Angechinjwa mamaako,babaako au ndugu mwingine wa uzao wenu ungesahau hayo maumivu kisa huna uwezo wa kuwarudisha.Hapa hoja si kuwarudisha ila haki itendeke kwa wote waliouwawa kinyama! Wewe huna ndugu ameuwa naona au hata kuona wengne si ndugu zako wakitandikwa risasi na kufa papohapo.
 
Machafuko ya uchaguzi wa Oktoba 2025 nchini Tanzania yalifunikwa na giza zito la kuzimwa kwa intaneti, baada ya mrindimo wa bunduki kunyamaza ghafla. Sasa, ushahidi mpya unafichua kile ambacho hakikusimuliwa - vifo vya watu ambao idadi yao bado haijulikani, miili iliyotoweka, na tuhuma za ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaodaiwa kufanywa na vyombo vya usalama.

Kurunzi ya DW inamulika kilichotokea Mwanza, jiji la pili kwa ukubwa nchini Tanzania, na inakuja na undani ambao haujawahi kuwekwa hadharani.

Inasikitisha Sana.

Samuya alitukosea sana...atalipa damu za wasio na hatia aliowaua.
 
Tulishamwachia Mungu yeye atajua alipe kwa wakati gani!, kumbuka kila baya na jema atendalo mtu hulipwa kwa wakati.
Unamuachia Mungu ili iweje?tutalipa kisasi amini nakuambia ,hakuna kumuachia Mungu.huwezi kujisifu kwa kuuwa halafu utuambie unamuachia Mungu.Labda Mungu awe shemj yako sawa
 
najua maumivu yenu ila mengine ni kusahau tu yapite!,watu washachinjwa na kuzikwa kusikojulikana hatuna uwezo wa kuwarudisha tena ni kuwaombea Mungu awape pumziko salama huko waliko.
Acha zako wewe...tuzike nguo then tumuachie Mungu?tena watu ambao hata kwenye maandano hawakuwepo tena siku ya tatu baada ya uchaguzi haramu..tutalipa kisasi kaeni mkijua hivyo
 
Wale jamaa waliokutwa kwenye banda la video asee jmn walimiminiwa risasi kama magaidi
kwenye banda lile kulikuwa mtoto wa miaka 9 na yeye walipiga risasi wale mbwa .....haiwezeakani damu zipotee kirahisi hivi.hivi visasis ni vya vizazi na vizazi ...muda ni mwalimu mzuri
 
Back
Top Bottom