Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,597
- 215,272
Nilikua ninaangalia documentary ya ndoa ya Charles na Diana siku nyingi kidogo. Usiku kabla ya ndoa ndiyo wa mama watu wazima walimkalisha Diana na kumwambia mume wako ana uhusiano wa kimapenzi na Camilla. Wewe utakua mke wa ndoa na ikiwezekana utakua malkia Charles akiwa mfalme. Kwa binti wa miaka 18 aliyejua anaolewa na mfalme ajaye furaha ya ndoa ilimuishia pale.
Katika kuoa watu makini huangalia anamuoa mtoto wa nani, familia ikoje, wengine hata mapenzi yanakua hayapo lakini wanaangalia kuchanganya damu. Watoto wangu watakua na nusu ya damu ya ukoo flani na mgawanyo wa mali pia.
Kuna mama katika ile documenary ambae na yeye ni mke wa tajiri mmoja wa ma Lady alisema “ Diana was naive to let the situation slide away, she was the wife and she would have been the one to be seen in public with Charles and find her self a way to make happy when Charles is with Camilla”
So sometimes married people are aware of infidelities but they just keep the blind eye and focus on rising up the kids.