Katika mahojiano aliyoyafanya na gazeti la "Badisches Tagblatt" la Ujerumani, jaji Wolfgang Schomburg amewanyooshea viongozi wengi kidole: Schomburg aliyekuwa sehemu ya jopo la majaji lililosimamia kesi ya mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 amewataka mapadri wa kikatoliki waliohusika katika mauaji hayo ya kinyama wafikishe mahakamani. Schomburg ameukosoa uongozi wa kanisa katoliki, Vatikan, kwa kuwalinda mapadri hao ambao wanapaswa kufikishwa mbele ya sheria.
Ni kweli kwamba vipo visa ambapo uongozi wa kanisa katoliki uliamua kuwapatia hifadhi viongozi wa kiroho ambao walihusika moja kwa moja kwenye mauaji ya kikatili.
Mmoja wao ni padri Wenceslas Munyeshyaka. Yeye mwaka 1994 alibeba bunduki kama mwanajeshi na kupanga njama na waasi wa Kihutu. Waasi hao waliwaua mamia ya watu waliokuwa wametafuta hifadhi ndani ya kanisa la padri Munyeshyaka. Padri huyo baadaye alihamia Ufaransa. Mahakama moja ya nchini Rwanda ilimhukumu adhabu ya kifungo cha maisha lakini kanisa katoliki nchini Ufaransa lilimtetea na kusema kuhukumiwa kwa Munyeshyaka kwa mauaji ya kimbari si sababu ya kumfanya asiendelee na kazi yake ya upadri.
Mapadri wafichwa Ulaya
Padri Munyeshyaka hayupo pekee yake. Mapadri na masista waliofahamika kuhusika katika mauaji ya Rwanda walipelekwa Ulaya na kupatiwa hifadhi huko. Miongoni mwao alikuwa Padri Athanase Seromba aliyeruhusu kanisa lake libomolewe likiwa na Watutsi 2,000 ndani. Wale walioponea walifyatuliwa risasi na kuuliwa. Kanisa Katoliki lilimsaidia kukimbilia Italia na hata kuhakikisha kwamba anapwea jina jipya na pasipoti mpya.
Ni kweli kwamba vipo visa ambapo uongozi wa kanisa katoliki uliamua kuwapatia hifadhi viongozi wa kiroho ambao walihusika moja kwa moja kwenye mauaji ya kikatili.
Mmoja wao ni padri Wenceslas Munyeshyaka. Yeye mwaka 1994 alibeba bunduki kama mwanajeshi na kupanga njama na waasi wa Kihutu. Waasi hao waliwaua mamia ya watu waliokuwa wametafuta hifadhi ndani ya kanisa la padri Munyeshyaka. Padri huyo baadaye alihamia Ufaransa. Mahakama moja ya nchini Rwanda ilimhukumu adhabu ya kifungo cha maisha lakini kanisa katoliki nchini Ufaransa lilimtetea na kusema kuhukumiwa kwa Munyeshyaka kwa mauaji ya kimbari si sababu ya kumfanya asiendelee na kazi yake ya upadri.
Mapadri wafichwa Ulaya
Padri Munyeshyaka hayupo pekee yake. Mapadri na masista waliofahamika kuhusika katika mauaji ya Rwanda walipelekwa Ulaya na kupatiwa hifadhi huko. Miongoni mwao alikuwa Padri Athanase Seromba aliyeruhusu kanisa lake libomolewe likiwa na Watutsi 2,000 ndani. Wale walioponea walifyatuliwa risasi na kuuliwa. Kanisa Katoliki lilimsaidia kukimbilia Italia na hata kuhakikisha kwamba anapwea jina jipya na pasipoti mpya.