Vatican yashutumiwa kuhusika mauaji ya kimbari Rwanda

Malaria 2

JF-Expert Member
Oct 17, 2023
2,831
4,221
Katika mahojiano aliyoyafanya na gazeti la "Badisches Tagblatt" la Ujerumani, jaji Wolfgang Schomburg amewanyooshea viongozi wengi kidole: Schomburg aliyekuwa sehemu ya jopo la majaji lililosimamia kesi ya mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 amewataka mapadri wa kikatoliki waliohusika katika mauaji hayo ya kinyama wafikishe mahakamani. Schomburg ameukosoa uongozi wa kanisa katoliki, Vatikan, kwa kuwalinda mapadri hao ambao wanapaswa kufikishwa mbele ya sheria.


Ni kweli kwamba vipo visa ambapo uongozi wa kanisa katoliki uliamua kuwapatia hifadhi viongozi wa kiroho ambao walihusika moja kwa moja kwenye mauaji ya kikatili.


Mmoja wao ni padri Wenceslas Munyeshyaka. Yeye mwaka 1994 alibeba bunduki kama mwanajeshi na kupanga njama na waasi wa Kihutu. Waasi hao waliwaua mamia ya watu waliokuwa wametafuta hifadhi ndani ya kanisa la padri Munyeshyaka. Padri huyo baadaye alihamia Ufaransa. Mahakama moja ya nchini Rwanda ilimhukumu adhabu ya kifungo cha maisha lakini kanisa katoliki nchini Ufaransa lilimtetea na kusema kuhukumiwa kwa Munyeshyaka kwa mauaji ya kimbari si sababu ya kumfanya asiendelee na kazi yake ya upadri.


Mapadri wafichwa Ulaya


Padri Munyeshyaka hayupo pekee yake. Mapadri na masista waliofahamika kuhusika katika mauaji ya Rwanda walipelekwa Ulaya na kupatiwa hifadhi huko. Miongoni mwao alikuwa Padri Athanase Seromba aliyeruhusu kanisa lake libomolewe likiwa na Watutsi 2,000 ndani. Wale walioponea walifyatuliwa risasi na kuuliwa. Kanisa Katoliki lilimsaidia kukimbilia Italia na hata kuhakikisha kwamba anapwea jina jipya na pasipoti mpya.
 
Katika mahojiano aliyoyafanya na gazeti la "Badisches Tagblatt" la Ujerumani, jaji Wolfgang Schomburg amewanyooshea viongozi wengi kidole: Schomburg aliyekuwa sehemu ya jopo la majaji lililosimamia kesi ya mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 amewataka mapadri wa kikatoliki waliohusika katika mauaji hayo ya kinyama wafikishe mahakamani. Schomburg ameukosoa uongozi wa kanisa katoliki, Vatikan, kwa kuwalinda mapadri hao ambao wanapaswa kufikishwa mbele ya sheria.


Ni kweli kwamba vipo visa ambapo uongozi wa kanisa katoliki uliamua kuwapatia hifadhi viongozi wa kiroho ambao walihusika moja kwa moja kwenye mauaji ya kikatili.


Mmoja wao ni padri Wenceslas Munyeshyaka. Yeye mwaka 1994 alibeba bunduki kama mwanajeshi na kupanga njama na waasi wa Kihutu. Waasi hao waliwaua mamia ya watu waliokuwa wametafuta hifadhi ndani ya kanisa la padri Munyeshyaka. Padri huyo baadaye alihamia Ufaransa. Mahakama moja ya nchini Rwanda ilimhukumu adhabu ya kifungo cha maisha lakini kanisa katoliki nchini Ufaransa lilimtetea na kusema kuhukumiwa kwa Munyeshyaka kwa mauaji ya kimbari si sababu ya kumfanya asiendelee na kazi yake ya upadri.


Mapadri wafichwa Ulaya


Padri Munyeshyaka hayupo pekee yake. Mapadri na masista waliofahamika kuhusika katika mauaji ya Rwanda walipelekwa Ulaya na kupatiwa hifadhi huko. Miongoni mwao alikuwa Padri Athanase Seromba aliyeruhusu kanisa lake libomolewe likiwa na Watutsi 2,000 ndani. Wale walioponea walifyatuliwa risasi na kuuliwa. Kanisa Katoliki lilimsaidia kukimbilia Italia na hata kuhakikisha kwamba anapwea jina jipya na pasipoti mpya.
Duuh hatari sana watu wanaugwaya uzi unao wahusu!
 
Kumpa hifadhi muhalifu/Mtuhumiwa ni sawa na kusapoti alichokifanya.
Ni kweli kabisa kama wamemkingia kifua hayo ni makosa makubwa sana hawana tofauti na hawa walioandika Aya hii

Suratul Al'anfal
12. Mola wako Mlezi alipo wafunulia Malaika: Hakika Mimi ni pamoja nanyi, basi watieni nguvu walio amini. Nitatia woga katika nyoyo za walio kufuru. Basi wapigeni juu ya shingo na wapigeni kwenye kila ncha za vidole.

Vatican na waliotunga koran ni washenzi sana, makatili mno
 
Ni kweli kabisa kama wamemkingia kifua hayo ni makosa makubwa sana hawana tofauti na hawa walioandika Aya hii

Suratul Al'anfal
12. Mola wako Mlezi alipo wafunulia Malaika: Hakika Mimi ni pamoja nanyi, basi watieni nguvu walio amini. Nitatia woga katika nyoyo za walio kufuru. Basi wapigeni juu ya shingo na wapigeni kwenye kila ncha za vidole.

Vatican na waliotunga koran ni washenzi sana, makatili mno
Huu sasa uchokozi. ๐Ÿ˜
Quran imeingiaje, hii ni dini ya amani
 
Kwamba walikimbilia kanisani akawaua yeye, au? Kwa nini wasitafutwe waasi walioua?
Baadhi ya mapadri walishiriki moja kwa moja ktk mauaji ya halaiki dhidi ya Watutsi na Wahutu wa mrengo wa kushoto (wasioafiki mauaji dhidi ya Watutsi). Baadhi ya Watawa walitoa taarifa kwa Wauaji kuhusu uwepo wa watutsi walioenda kujihifadhi ndani ya kanisa wakijua ni mahala salama na wengine washika kabisa bundiki na kuua. Wote walioshiriki wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria.
 
Katika mahojiano aliyoyafanya na gazeti la "Badisches Tagblatt" la Ujerumani, jaji Wolfgang Schomburg amewanyooshea viongozi wengi kidole: Schomburg aliyekuwa sehemu ya jopo la majaji lililosimamia kesi ya mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 amewataka mapadri wa kikatoliki waliohusika katika mauaji hayo ya kinyama wafikishe mahakamani. Schomburg ameukosoa uongozi wa kanisa katoliki, Vatikan, kwa kuwalinda mapadri hao ambao wanapaswa kufikishwa mbele ya sheria.


Ni kweli kwamba vipo visa ambapo uongozi wa kanisa katoliki uliamua kuwapatia hifadhi viongozi wa kiroho ambao walihusika moja kwa moja kwenye mauaji ya kikatili.


Mmoja wao ni padri Wenceslas Munyeshyaka. Yeye mwaka 1994 alibeba bunduki kama mwanajeshi na kupanga njama na waasi wa Kihutu. Waasi hao waliwaua mamia ya watu waliokuwa wametafuta hifadhi ndani ya kanisa la padri Munyeshyaka. Padri huyo baadaye alihamia Ufaransa. Mahakama moja ya nchini Rwanda ilimhukumu adhabu ya kifungo cha maisha lakini kanisa katoliki nchini Ufaransa lilimtetea na kusema kuhukumiwa kwa Munyeshyaka kwa mauaji ya kimbari si sababu ya kumfanya asiendelee na kazi yake ya upadri.


Mapadri wafichwa Ulaya


Padri Munyeshyaka hayupo pekee yake. Mapadri na masista waliofahamika kuhusika katika mauaji ya Rwanda walipelekwa Ulaya na kupatiwa hifadhi huko. Miongoni mwao alikuwa Padri Athanase Seromba aliyeruhusu kanisa lake libomolewe likiwa na Watutsi 2,000 ndani. Wale walioponea walifyatuliwa risasi na kuuliwa. Kanisa Katoliki lilimsaidia kukimbilia Italia na hata kuhakikisha kwamba anapwea jina jipya na pasipoti mpya.
Hii mbona inajulikana,, kama kanisa katoliki wanahusika tena moja,, ila kama ndo ingekuwa uislam lazima ungesikia habari za ugaidi..
 
Back
Top Bottom