VAT itaua makampuni mengi ya mikoani, TRA angalieni hili

Mkulima

JF-Expert Member
Feb 4, 2007
1,034
1,022
Wana JF,

Ujumbe huu uende kwa Rais Samia pamoja na TRA.

Huu mfumo mpya ambao TRA imeuanzisha katika kukusanya VAT umeleta matatizo makubwa sana hasa kwa kampuni za wilayani na mikoani.

Kawaida VAT huwa hivi. Mfanyabiashara unaauza bidhaa yako au huduma yako na kuongeza VAT juu ambayo mlaji huibeba. VAT haitakiwi kuwa mzigo kwa muuzaji bali mnunuzi wa huduma.

Sasa kinachotokea TZ hasa kwa kampuni kubwa zilizoko wilayani ni kwamba
1. Ukiwa VAT registered unaweza kuwa na ushindani na makampuni mengine ambayo sio VAT registered. Kwahiyo ukiongeza VAT kwenye bidhaa yako, inakula kwako kwasababu huduma yako itakuwa aghali zaidi. Hili linatokea sana kwa biashara kubwa huko wilayani. Kwahiyo hawaongezi VAT kwenye mauzo yao na badala yake wanatoa VAT kwenye faida zao. Mfano mauzo ya milioni 50 kwa mwezi, VAT yake ni milioni 9.

2. Inatakiwa utoe VAT ya manunuzi yote unayofanya katika kutengeneza mauzo yako. Bahati mbaya wilayani wafanyabiashara ambao ni VAT registered ni wachache sana. Kwahiyo unajikuta huna receipts kabisa za manunuzi yenye VAT. Kwenye expenses zako VAT ni zero

Huko nyuma mfanyabiashara alikuwa anaruhusiwa kuingiza VAT ya baadhi ya matumizi yake. Lakini sasa wamebana, kama huna receipt imekula kwako. Maana yake katika hayo mauzo ya milioni 50 ni kama wewe hujaweka matumizi yoyote. Yaani umezalisha milioni 50 bila ku invest hata senti tano.

Kwahiyo ikifika tarehe 20 mwezi unaofuata inabidi ulipe hiyo milioni 9 ya VAT. Na of course utakuwa hauna maana huenda hata fida tu ya biashara yako haifiki hiyo figure.

3. Unaweza kuta hao uliowauzia huduma yako hawalipi ontime. Kama sisi wengine hata sasa tunadai madeni ya October 2022. Sasa TRA wanataka VAT yao hapo hapo. Kwahiyo unatakiwa kulipa hiyo milioni 9 ambayo hujapokea malipo yake.

Matokeo ya hizo points tatu ni kufilisika. Yaakiendelea hayo mimi mimi miezi mitatu inayokuja huenda ikabidi kufunga biashara na kuondoa wafanyakazi kama 30. Kwasasa ni stress tu na kutoa pesa zangu zingine ili kulipa hizo VAT. Mwisho wa siku kila mwezi ni hasara tu.

Kwa mfano huko nyuma nilikuwa nalipa wastani wa VAT milioni moja kwa mwezi. Miezi miwili ya mwaka huu nimelipa average kwa mwezi milioni 9.

Wanavyofanya nchi zingine, mfanyabiashara anachagua kulipa VAT flat rate kwa mfano katika VAT uliyokusanya unalipa 25% na hakuna mambo ya kudai VAT ya matumizi au unadai VAT ya matumizi. Mfanyabiashara anachagua njia ambayo ni nafuu kwake.

Kwa TZ huu mfumo mpya wa kulazimisha unaenda kuua biashara zetu. Hivi hata kwa akili ndogo kweli kwenye biashara ya kama hoteli, unaweza kuzalisha mauzo ya milioni 50 bila kuwa na matumizi yoyote ya maana? Ina maana watu wanafanya manunuzi ila ni kwenye maduka ambayo sio VAT registered. Biashara kama ya hoteli faida haizidi asilimia 20. Sasa VAT pekee ikichukua asilimia 18, kuna biashara tena hapo?

Ukiwa Dar au miji mikubwa ni rahisi kununua kila kitu kutoka maduka ambayo ni VAT registered. Lakini wilaya kama kule Ngara huna luxury hiyo.

Wahusika chukueni hatua.
 
VAT ni utapeli wa wazi kabisa, halafu mfumo wa kodi wa Tanzania kwa kiasi kikubwa ni utapeli kwa mfano mimi nina mtaji wa laki moja, au milioni moja nilikopata mtaji wewe mtoza ushuru haupajui sasa kimantiki kodi ilitakiwa nifanye biashara halafu kwenye faida ninayoipata ndio wewe TRA uchukue kodi yako na mimi nibaki na faida yangu kidogo. Sasa ajabu wewe unaanza makadirio kwenye mtaji wa mtu ambapo haujui mtaji umetokea wapi?
 
Mapitio ya VAT lazima yafanyike na kuboreshwa ikiwezekana ibakie single digit, haiwezekani dunia ya ushindani VAT iwe two digit tena kwenye nchi ambayo bado biashara nyingi watu wanajikongoja taratibu kukua lakini serikali hiyo hiyo inawarudisha nyuma
 
Ndio maana watu wanakwepa kodi kwa mambo ya kipuuzi kama hiyo.

Na wangekua na kodi rafiki nakuhakikishia tax base yao ingekua kubwa na wangepata mapato ya kutosha sana lakini kwa sababu wao kodi hawaendi na uhalisia ndio hiyo unaona watu wengi hufanya biashara yenye mabilioni kwa mwaka kimya kimya na hawapo kwenye mifumo yao kabisa na wanalazimika kukwepa kwa sababu kama hizo za uonezi
 
Wana JF,

Ujumbe huu uende kwa Rais Samia pamoja na TRA.

Huu mfumo mpya ambao TRA imeuanzisha katika kukusanya VAT umeleta matatizo makubwa sana hasa kwa kampuni za wilayani na mikoani.

Kawaida VAT huwa hivi. Mfanyabiashara unaauza bidhaa yako au huduma yako na kuongeza VAT juu ambayo mlaji huibeba. VAT haitakiwi kuwa mzigo kwa muuzaji bali mnunuzi wa huduma.

Sasa kinachotokea TZ hasa kwa kampuni kubwa zilizoko wilayani ni kwamba
1. Ukiwa VAT registered unaweza kuwa na ushindani na makampuni mengine ambayo sio VAT registered. Kwahiyo ukiongeza VAT kwenye bidhaa yako, inakula kwako kwasababu huduma yako itakuwa aghali zaidi. Hili linatokea sana kwa biashara kubwa huko wilayani. Kwahiyo hawaongezi VAT kwenye mauzo yao na badala yake wanatoa VAT kwenye faida zao. Mfano mauzo ya milioni 50 kwa mwezi, VAT yake ni milioni 9.

2. Inatakiwa utoe VAT ya manunuzi yote unayofanya katika kutengeneza mauzo yako. Bahati mbaya wilayani wafanyabiashara ambao ni VAT registered ni wachache sana. Kwahiyo unajikuta huna receipts kabisa za manunuzi yenye VAT. Kwenye expenses zako VAT ni zero

Huko nyuma mfanyabiashara alikuwa anaruhusiwa kuingiza VAT ya baadhi ya matumizi yake. Lakini sasa wamebana, kama huna receipt imekula kwako. Maana yake katika hayo mauzo ya milioni 50 ni kama wewe hujaweka matumizi yoyote. Yaani umezalisha milioni 50 bila ku invest hata senti tano.

Kwahiyo ikifika tarehe 20 mwezi unaofuata inabidi ulipe hiyo milioni 9 ya VAT. Na of course utakuwa hauna maana huenda hata fida tu ya biashara yako haifiki hiyo figure.

3. Unaweza kuta hao uliowauzia huduma yako hawalipi ontime. Kama sisi wengine hata sasa tunadai madeni ya October 2022. Sasa TRA wanataka VAT yao hapo hapo. Kwahiyo unatakiwa kulipa hiyo milioni 9 ambayo hujapokea malipo yake.

Matokeo ya hizo points tatu ni kufilisika. Yaakiendelea hayo mimi mimi miezi mitatu inayokuja huenda ikabidi kufunga biashara na kuondoa wafanyakazi kama 30. Kwasasa ni stress tu na kutoa pesa zangu zingine ili kulipa hizo VAT. Mwisho wa siku kila mwezi ni hasara tu.

Kwa mfano huko nyuma nilikuwa nalipa wastani wa VAT milioni moja kwa mwezi. Miezi miwili ya mwaka huu nimelipa average kwa mwezi milioni 9.

Wanavyofanya nchi zingine, mfanyabiashara anachagua kulipa VAT flat rate kwa mfano katika VAT uliyokusanya unalipa 25% na hakuna mambo ya kudai VAT ya matumizi au unadai VAT ya matumizi. Mfanyabiashara anachagua njia ambayo ni nafuu kwake.

Kwa TZ huu mfumo mpya wa kulazimisha unaenda kuua biashara zetu. Hivi hata kwa akili ndogo kweli kwenye biashara ya kama hoteli, unaweza kuzalisha mauzo ya milioni 50 bila kuwa na matumizi yoyote ya maana? Ina maana watu wanafanya manunuzi ila ni kwenye maduka ambayo sio VAT registered. Biashara kama ya hoteli faida haizidi asilimia 20. Sasa VAT pekee ikichukua asilimia 18, kuna biashara tena hapo?

Ukiwa Dar au miji mikubwa ni rahisi kununua kila kitu kutoka maduka ambayo ni VAT registered. Lakini wilaya kama kule Ngara huna luxury hiyo.

Wahusika chukueni hatua.
Hii ni hoja ya msingi sana.
 
Hahaha, kuna watu nilikuwa nawaambia huu mfumo mpya wa kukusanya VAT muda si mrefu vilio vitaanza maana wametuweza haswa.

Mfumo wa sasa ni mzuri sana kwa serikali kwani mfanyabiashara anayenunua bila risiti imekula kwake labda na yeye auze bila risiti na pia huwezi chezesha manunuzi sababu yapo moja kwa moja kwenye mfumo.

MFUMO UNAKUAMBIA, UMENUNUA TSH KADHAA, UMEUZA TSH KADHAA. TUPE CHETU.

Kuna njia mbili tu za kupona. Usinunue bila risiti ili uweze kuclaim ukiuza au usiwe VAT. Kinyume na hapo na ww usitoe risiti udakwe.
 
Funga biashara na fungua biashara mpya hiyo VAT inataka ivyo.
Hata inapo tokea mfanya biashara anafunga, ahakikishe anapo peleka barua pale tra pia lazima ajiandikishe kwenye kitabu cha wageni ili ikija kutokea siku wanamdai kodi aseme nilisha kuja kuleta barua ya kusimamisha biashara na nilijiandikisha kwenye kitabu ya wageni (hua wanatabia ya kuficha barua)
 
Na ubaya zaidi ni pale wanapokuja kukadiria kodi kwenye biashara ambayo hata mtu hajaianza, na hajui mauzo yake yatakua yanakuaje kwa siku.
 
Wana JF,

Ujumbe huu uende kwa Rais Samia pamoja na TRA.

Huu mfumo mpya ambao TRA imeuanzisha katika kukusanya VAT umeleta matatizo makubwa sana hasa kwa kampuni za wilayani na mikoani.

Kawaida VAT huwa hivi. Mfanyabiashara unaauza bidhaa yako au huduma yako na kuongeza VAT juu ambayo mlaji huibeba. VAT haitakiwi kuwa mzigo kwa muuzaji bali mnunuzi wa huduma.

Sasa kinachotokea TZ hasa kwa kampuni kubwa zilizoko wilayani ni kwamba
1. Ukiwa VAT registered unaweza kuwa na ushindani na makampuni mengine ambayo sio VAT registered. Kwahiyo ukiongeza VAT kwenye bidhaa yako, inakula kwako kwasababu huduma yako itakuwa aghali zaidi. Hili linatokea sana kwa biashara kubwa huko wilayani. Kwahiyo hawaongezi VAT kwenye mauzo yao na badala yake wanatoa VAT kwenye faida zao. Mfano mauzo ya milioni 50 kwa mwezi, VAT yake ni milioni 9.

2. Inatakiwa utoe VAT ya manunuzi yote unayofanya katika kutengeneza mauzo yako. Bahati mbaya wilayani wafanyabiashara ambao ni VAT registered ni wachache sana. Kwahiyo unajikuta huna receipts kabisa za manunuzi yenye VAT. Kwenye expenses zako VAT ni zero

Huko nyuma mfanyabiashara alikuwa anaruhusiwa kuingiza VAT ya baadhi ya matumizi yake. Lakini sasa wamebana, kama huna receipt imekula kwako. Maana yake katika hayo mauzo ya milioni 50 ni kama wewe hujaweka matumizi yoyote. Yaani umezalisha milioni 50 bila ku invest hata senti tano.

Kwahiyo ikifika tarehe 20 mwezi unaofuata inabidi ulipe hiyo milioni 9 ya VAT. Na of course utakuwa hauna maana huenda hata fida tu ya biashara yako haifiki hiyo figure.

3. Unaweza kuta hao uliowauzia huduma yako hawalipi ontime. Kama sisi wengine hata sasa tunadai madeni ya October 2022. Sasa TRA wanataka VAT yao hapo hapo. Kwahiyo unatakiwa kulipa hiyo milioni 9 ambayo hujapokea malipo yake.

Matokeo ya hizo points tatu ni kufilisika. Yaakiendelea hayo mimi mimi miezi mitatu inayokuja huenda ikabidi kufunga biashara na kuondoa wafanyakazi kama 30. Kwasasa ni stress tu na kutoa pesa zangu zingine ili kulipa hizo VAT. Mwisho wa siku kila mwezi ni hasara tu.

Kwa mfano huko nyuma nilikuwa nalipa wastani wa VAT milioni moja kwa mwezi. Miezi miwili ya mwaka huu nimelipa average kwa mwezi milioni 9.

Wanavyofanya nchi zingine, mfanyabiashara anachagua kulipa VAT flat rate kwa mfano katika VAT uliyokusanya unalipa 25% na hakuna mambo ya kudai VAT ya matumizi au unadai VAT ya matumizi. Mfanyabiashara anachagua njia ambayo ni nafuu kwake.

Kwa TZ huu mfumo mpya wa kulazimisha unaenda kuua biashara zetu. Hivi hata kwa akili ndogo kweli kwenye biashara ya kama hoteli, unaweza kuzalisha mauzo ya milioni 50 bila kuwa na matumizi yoyote ya maana? Ina maana watu wanafanya manunuzi ila ni kwenye maduka ambayo sio VAT registered. Biashara kama ya hoteli faida haizidi asilimia 20. Sasa VAT pekee ikichukua asilimia 18, kuna biashara tena hapo?

Ukiwa Dar au miji mikubwa ni rahisi kununua kila kitu kutoka maduka ambayo ni VAT registered. Lakini wilaya kama kule Ngara huna luxury hiyo.

Wahusika chukueni hatua.
Watumishi wenyewe wengi ni akina kamlete,watasaidia nini hawajawahi ata kufanya Biashara ya genge!
 
Mkuu. Mfumo uko sawa. Tatizo hutaki kuajiri wataalam wakusaidie kwenye maswala ya uhasibu na kodi.
Tafuta
Finance Manager mwenye CPA
Pia uchumi unaruhusu ajiri mtu aliyesomea mambo ya Tax management.
Wataalam wako kibao ila ndio hampendi kuwatumia.
Wafanyabiashara wa kati wengi hawana huu uwezo wa kuajiri wataalam. Akijimwambafy sana atakuwa na bajeti ya laki na nusu kwa mwezi na mtaalam anayekubali hiyo pesa huyo si mtaalam ni mhitimu tu wa chuo, atamdanganya danganya hapo na materminology aliyokariri halafu mwishoni anajikuta ana tax finding kubwa za kujibu na huyo huyo cpa uchwara atajifanya maafisa wanataka kitu kidogo kodi ipungue kumbe na yeye ni sehemu ya tatizo na ana mgao.

Wafanyabiashara wengine wamepata shida zaidi sababu ya bajeti ndogo na kuajiri cpa/degree njaa wasio na uzoefu.

By tha way, uko tunapoelekea na hizi system zinazotoa mpaka financials, kama matumizi yote yatafanyika via tin, mhasibu kwenye hizi biashara ndogo ndogo na za kati hana kazi tena. Atafanya kazi gani iwapo system inatoa correct tax liability za aina zote? Reconcilliation na takataka zote sytem inafanya. Na huitaji degree au cpa kupost kwenye system. CPA watakaoiitajika na biashara za kati na ndogo ni auditors wenye mihuri na consultancy firms.
 
Tatizo la TRA hawajawahi kufanya biashara. Wanachofikiria ni kukamua wafanyabiashara.

Wasipotafuta solution ya hii issue ya VAT wajiandae kutengeneza mizoga mingi na watu wengi kujifunza njia za kukwepa kodi.

Seriakali sasa wameona mjia ya kupata kodi ni kupitia VAT. Lengo la VAT halikuwa hivyo na kutakuwa na madhara makubwa sana.

Wacha wengine tufunge hizo hotels hata kwa muda kadhaa.. Stress za TRA zimezidi.
 
Back
Top Bottom