UZURI MBINGUNI HAKUNA MPIRA NA MPIRA NI DHAMBI

UZURI MBINGUNI HAKUNA MPIRA NA MPIRA NI DHAMBI

Funny boe

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2023
Posts
3,388
Reaction score
7,549
Kwenye mechi inayoendelea sasa kati ya Dodoma Jiji na Simba Sc ikiwa simba hatopata goli na kufuzu kwenye haya mashindano nitatangaza rasmi kuachana na masuala ya mipira ikiwa ni kufatilia matokeo wala kuangalia zikiwa mubashara.

Uzuri ni kuwa hivi karibuni nimegundua kuwa mbinguni hakuna mpira na ni dhambi kubwa sana kujihusisha na masuala ya kidunia hasa soka.

Sasa inakaribia half time na mkumbuke simba hajawahi kupata goli hata moja kipindi cha pili.

Haiwezekani miaka 6 timu kubwa kama Simba haina kombe hata moja.

Wacha nitafute kazi nyingine za kufanya hata kuwekeza kwenye kilimo cha jembe la mkono au kuuzunguka ulimwengu nikiihubiri injili ya mungu

POVU RUKSA😎😎

ngara23
 
Mashabiki wengi walishaaminishwa Simba kufanya vibaya sababu ni Yanga, kutochukua makombe sababu ni Yanga. Kum control shabiki wa mpira wa TZ ni rahisi sana. Tumakaririshwa Simba na Yanga ni kubwa bila kuwa na facts za ukubwa gani unaozungumzwa hapo.

Sisi tumekaririshwa ushabiki.
 
Mpira wa simba na yanga ama unamanisha mpira wa kinga...🫣
 
Mashabiki wengi walishaaminishwa Simba kufanya vibaya sababu ni Yanga, kutochukua makombe sababu ni Yanga. Kum control shabiki wa mpira wa TZ ni rahisi sana. Tumakaririshwa Simba na Yanga ni kubwa bila kuwa na facts za ukubwa gani unaozungumzwa hapo.

Sisi tumekaririshwa ushabiki.
Basi kuanzia muda mchache ujao nitaachana na hayo masuala tuliyokaririshwa, uzuri vitu vya kufanya ni vingi sana
 
Mpira wa simba na yanga ama unamanisha mpira wa kinga...🫣
Mpira ambao wanaume 22 wenye miguu 44 wakiwa na wasimamizi zaidi ya kumi kila upande wanaokutana kwenye sehemu ya wazi iitwayo uwanja wakihangaikia kitu fulani chenye umbo la mviriringo kukiingiza kwenye nyavu zilizofungwa kwenye mabomba kama ya chuma hivi yaliyokaa kama mstatiri

Umenielewa?
 
Mpira ambao wanaume 22 wenye miguu 44 wakiwa na wasimamizi zaidi ya kumi kila upande wanaokutana kwenye sehemu ya wazi iitwayo uwanja wakihangaikia kitu fulani chenye umbo la mviriringo kukiingiza kwenye nyavu zilizofungwa kwenye mabomba kama ya chuma hivi yaliyokaa kama mstatiri

Umenielewa?
Ndio mkuu wangu...🫡
 
Basi kuanzia muda mchache ujao nitaachana na hayo masuala tuliyokaririshwa, uzuri vitu vya kufanya ni vingi sana
Mi napenda mpira ila nilichefukwa siku timu yangu ilipotajwa kuchangia kwenye mauwaji ya halaiki. Nilijuliza sana na toka siku hiyo mi sio yule shabiki wa awali. Hizi timu zinatumika kinyume na wengi tunavyodhani na matokeo ni km wewe na mimi
 
Mi napenda mpira ila nilichefukwa siku timu yangu ilipotajwa kuchangia kwenye mauwaji ya halaiki. Nilijuliza sana na toka siku hiyo mi sio yule shabiki wa awali. Hizi timu zinatumika kinyume na wengi tunavyodhani na matokeo ni km wewe na mimi
Ulivogundua hivo ulichukua hatua gani mkuu
 
Back
Top Bottom