Mtini
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 1,487
- 2,344
Wasalam,
Leo nimependa kushare nanyi baadhi ya mambo ya kusikitisha yanayoendelea katika mahakama za mwanzo na si kwamba yanafanywa na mahakimu wote la hasha bali wachache wenye nia ovu. Naandika haya si kuwa nimesimuliwa hapana ila ni mambo yaliyonitokea miaka ya nyuma kipindi biashara yangu imeyumba. Baada ya biashara kuyumba nikajikuta na madeni mengi yasiweza kulipika kwa wakati huo hiyvo wadeni wangu wakawa wanatumia mbinu mbalimbalia za kunibana, haya ndiyo niliyoyashuhudia.
1. Unaweza kusomewa hukumu imekaa namna hii ila siku ya kuchukua nakala ya hukumu ukakutana na kitu tofauti kabisa. Mfano unaweza kuambiwa unatakiwa kulipa laki moja ila kwenye hukumu ikaandikwa laki 6. Sasa kumbuka uliposomewa unalipa laki moja ulirelax hujujisumbua na rufaa kumbe huku kwenye makaratasi ngoma ni nyingine kabisa yaani.
2. Hakimu anaweza toa hati ya kukukamata kwa nguvu wakati unafahamika ulipo na wala si mtu wa shari l, hujaiba na kesi ni madai. Anayekudai anachonga na hakimu namna ya kukuharass anapewa hati ya kukukamata kwa nguvu anapeleka polisi msako unaanza. Ukidakwa unalala rumande wala hapo huwezi dhaminiwa polisi hadi mahakamani. Na siku ukipelekwa mahakamani hakimu husika anajifanya busy ili mradi tu ushuke magereza hapo kama unachochote lazima ujitikise.
3. Mdai anaweza kufungua kesi na usipewe summons ya kuitwa na ikaendeshwa upande mmoja. Siku moja niko mahakamani kwa kesi nyingine nikasikia jina langu linatajwa ile kuingia kule nikakuta ni kesi nyingine kabisa ambayo siijui na imeshafika mbali.
4. Inaweza kuwa ni madai ukafunguliwa jinai, japo una vielelezo au hata anayekudai akashindwa kuthibitisha jinai yake ila ukaambiwa ulipe faini au kifungo na siku ya pili ukatakiwa kulipa kiasi chote unachodaiwa.
Kiufupi ni mududu ni mengi, ndio maana kuna msemo wanasema mahakama za mwanzo hakuna sheria, serikali ijitahidi kuboresha hizi mahakama kwa kweli la sivyo haki za wengi zitakuwa zinapotea.
Leo nimependa kushare nanyi baadhi ya mambo ya kusikitisha yanayoendelea katika mahakama za mwanzo na si kwamba yanafanywa na mahakimu wote la hasha bali wachache wenye nia ovu. Naandika haya si kuwa nimesimuliwa hapana ila ni mambo yaliyonitokea miaka ya nyuma kipindi biashara yangu imeyumba. Baada ya biashara kuyumba nikajikuta na madeni mengi yasiweza kulipika kwa wakati huo hiyvo wadeni wangu wakawa wanatumia mbinu mbalimbalia za kunibana, haya ndiyo niliyoyashuhudia.
1. Unaweza kusomewa hukumu imekaa namna hii ila siku ya kuchukua nakala ya hukumu ukakutana na kitu tofauti kabisa. Mfano unaweza kuambiwa unatakiwa kulipa laki moja ila kwenye hukumu ikaandikwa laki 6. Sasa kumbuka uliposomewa unalipa laki moja ulirelax hujujisumbua na rufaa kumbe huku kwenye makaratasi ngoma ni nyingine kabisa yaani.
2. Hakimu anaweza toa hati ya kukukamata kwa nguvu wakati unafahamika ulipo na wala si mtu wa shari l, hujaiba na kesi ni madai. Anayekudai anachonga na hakimu namna ya kukuharass anapewa hati ya kukukamata kwa nguvu anapeleka polisi msako unaanza. Ukidakwa unalala rumande wala hapo huwezi dhaminiwa polisi hadi mahakamani. Na siku ukipelekwa mahakamani hakimu husika anajifanya busy ili mradi tu ushuke magereza hapo kama unachochote lazima ujitikise.
3. Mdai anaweza kufungua kesi na usipewe summons ya kuitwa na ikaendeshwa upande mmoja. Siku moja niko mahakamani kwa kesi nyingine nikasikia jina langu linatajwa ile kuingia kule nikakuta ni kesi nyingine kabisa ambayo siijui na imeshafika mbali.
4. Inaweza kuwa ni madai ukafunguliwa jinai, japo una vielelezo au hata anayekudai akashindwa kuthibitisha jinai yake ila ukaambiwa ulipe faini au kifungo na siku ya pili ukatakiwa kulipa kiasi chote unachodaiwa.
Kiufupi ni mududu ni mengi, ndio maana kuna msemo wanasema mahakama za mwanzo hakuna sheria, serikali ijitahidi kuboresha hizi mahakama kwa kweli la sivyo haki za wengi zitakuwa zinapotea.