G-Mdadisi
Senior Member
- Feb 15, 2018
- 157
- 99
Asasi za kiraia zinazotetea haki za wanawake Zanzibar kwa pamoja zitazindua waraka wa mapendekezo ya sheria ambao una lengo la kuwawezesha wanawake wengi kupata haki ya kushika nafasi za uongozi katika ngazi za maamuzi.
Uzindizi huo utafanyika siku ya Alhamis tarehe 05 Oktoba, 2023 katika ukumbi wa Bima uliopo Madema (Mpirani ) mjini Unguja ambao utawahusisha washiriki 80 muhimu kutoka taasisi za serikali na zisizo za kiserikali pamoja na waandishi wa habari.
Asasi hizo ni pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar (TAMWA –ZNZ), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya ya Utetezi wa Kimazingira na Jinsia Pemba (PEGAO) na Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA)
Uzinduzi huu umekuja kufuatia kukamilika kwa mchakato wa kupitia sheria, sera na katiba za vyama vya siasa ambao uliwashirikisha wadau mbali mbali na kuona mapungufu mengi yakiwemo kutozingatiwa usawa wa kijinsia kwa kundi la wanawake, vijana na watu wenye ulemavu
Hali kadhalika, azimio la 1325 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililotolewa tarehe 31 Oktoba mwaka 2000 linasema. “Kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi kunakuza demokrasia ya nchi, uchumi, amani na utulivu kwa muda mrefu”.
Aidha, Mkataba wa kimataifa unaopinga aina zote za udhalilishaji dhidi ya wanawake, (CEDAW) wa mwaka 1979 katika kifungu cha 7 unasisitiza kuwa na haki sawa baina ya mwanamke na mwanamme katika uchaguzi na mchakato mzima wa upigaji kura na kuchaguliwa kushika madaraka.
Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022, Zanzibar ina idadi ya watu wapatao kubwa kuliko wanaume 1,889,773 inaonyesha kuwa idadi ya wanawake ni 974,281 ambayo ni kubwa kuliko wanaume, hata hivyo, ilibainika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kuwa jumla ya wanawake 294,237 sawa na asilimia 51 waliandikishwa kama wapiga kura ikilinganishwa na wanaume 272,115 ambao ni sawa na asilimia 49.
Imetolewa na ZAFELA, PEGAO, TAMWA-ZNZ na JUWAUZA
Uzindizi huo utafanyika siku ya Alhamis tarehe 05 Oktoba, 2023 katika ukumbi wa Bima uliopo Madema (Mpirani ) mjini Unguja ambao utawahusisha washiriki 80 muhimu kutoka taasisi za serikali na zisizo za kiserikali pamoja na waandishi wa habari.
Asasi hizo ni pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar (TAMWA –ZNZ), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya ya Utetezi wa Kimazingira na Jinsia Pemba (PEGAO) na Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA)
Uzinduzi huu umekuja kufuatia kukamilika kwa mchakato wa kupitia sheria, sera na katiba za vyama vya siasa ambao uliwashirikisha wadau mbali mbali na kuona mapungufu mengi yakiwemo kutozingatiwa usawa wa kijinsia kwa kundi la wanawake, vijana na watu wenye ulemavu
Hali kadhalika, azimio la 1325 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililotolewa tarehe 31 Oktoba mwaka 2000 linasema. “Kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi kunakuza demokrasia ya nchi, uchumi, amani na utulivu kwa muda mrefu”.
Aidha, Mkataba wa kimataifa unaopinga aina zote za udhalilishaji dhidi ya wanawake, (CEDAW) wa mwaka 1979 katika kifungu cha 7 unasisitiza kuwa na haki sawa baina ya mwanamke na mwanamme katika uchaguzi na mchakato mzima wa upigaji kura na kuchaguliwa kushika madaraka.
Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022, Zanzibar ina idadi ya watu wapatao kubwa kuliko wanaume 1,889,773 inaonyesha kuwa idadi ya wanawake ni 974,281 ambayo ni kubwa kuliko wanaume, hata hivyo, ilibainika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kuwa jumla ya wanawake 294,237 sawa na asilimia 51 waliandikishwa kama wapiga kura ikilinganishwa na wanaume 272,115 ambao ni sawa na asilimia 49.
Imetolewa na ZAFELA, PEGAO, TAMWA-ZNZ na JUWAUZA