Wakati tunapika Sambusa za Nyama na shoga zangu, mmoja akatupa story ya Mama mmoja na Mumewe,
Basi Mume mtu alikua anachepuka na Binti mmoja akampangia nyumba na gari ya kutembelea, bibiye kusikia hayo akatuma Wahuni wamfanyie vitendo vya kudhalilisha yule binti, wahuni walimteka wakamfanyia mambo machafu huku wanamrekodi, binti aliporudi nyumbani akampigia simu Mwenza wake na kumueleza alichofanyiwa na watu hao wasiojulikana kisha akajitoa uhai,
Ilikua ni huzuni kubwa kwa Mzee yule, alichanganyikiwa, aliomba kustaafu, akawa mtu wa Pombe na kulala Bar, Bibiye nafsi ikamsuta, Roho ikamuuma, badala ya kujenga alizidi kubomoa, basi na yeye akatafuta faraja nje, akaanza kuchepuka na Kijana wa shoka, Penzi halikufika Mbali yule Kijana akamfia kifuani wakiwa Hotelin, kumbe alikua ana tatizo la Moyo,
Mnaweza kuimagine Mtu anakufa ukiwa nae chumbani, Kitandani, Uchi,
Bibiye akapata ujasiri, akavaa haraka haraka na kumfunika Marehemu kisha akatoroka na kurudi nyumbani kwake akiamini ameshinda hadi siku ya pili Polisi walipogonga kwenye mlango wao na kumwambia yupo chini ya Ulinzi kwa kosa la Mauaji,
Cameras za Hotelini zilimuumbua,
Wakati Kesi inaendelea na Mumewe alipoanza kumlaumu kwa tendo la kuchepuka hadi kuua ndipo na yeye akatoa ya Moyoni kwa kuelezea kukosa uaminifu kwa Mumewe kukasababisha yeye afanye kitendo cha Kinyama kwa Binti yule hadi kupelekea Umauti.
Nakumbuka nilibaki mdomo wazi hadi Sambusa nilizokua nachoma zikaungua

.