Uzi wa Matembezi (Travel & Vacations) na Vivutio vya Utalii nchini Tanzania

Juu ya jiwe Gangilonga ,Iringa mjini...Picha ya pili ni Mtwa Mkwawa museum(makumbusho ya mkwawa ambapo kuna fuvu la mkwawa)
 

Attachments

  • IMG_20220722_114422~2.jpg
    IMG_20220722_114422~2.jpg
    2.2 MB · Views: 2
  • IMG_20220724_115328~3.jpg
    IMG_20220724_115328~3.jpg
    1.7 MB · Views: 2
Barabara ya morogoro-dodoma..Huwa ina kisehemu kina kijani kizuri sana lami nyeupe haina magari..
 

Attachments

  • PXL_20221204_102921439.jpg
    PXL_20221204_102921439.jpg
    3.4 MB · Views: 2
I wish kufika Zanzibar,Hivi ni sehemu gani ntaenjoy zaidi nikienda, bajeti ni 300k🤔 naenda ijumaa kurudi jpili je itatosha? Napenda kuona wale watu wanaojirusha kwenye maji kutokea juu Hivi.
Kwa uchache.

Zanzibar

Kuna Upande wa town, Stone town......

Hapa kuna utajiri wa kihistoria kuanzia magofu ya mji mkongwe wa stone town uliojaa mali kale za tamaduni ya bara la asia, tamaduni za wazawa na historia ya utamaduni wa "waswahili" wa pwani, vyakula (forodhani), viungo asilia (karafuu, amdalasini, hiriki), michezo na matamasha (Sarakasi, Sauti za busara, mwaka kogwa n.k)

Upande wa Shamba

Huku ndio upande wa beach nzuri na mahoteli mengi ya kitalii, snorkeling & diving sites, activities kama kuogelea na dolphin, kasa n.k hupatikana upande huu.

N.k kutembelea shamba inahitaji uwe na bajeti nzuri zaidi kuliko Stone town.
 
Lindi beach ,Lindi mjini
Sea view beach & resort (hotel) mchana na usiku..Picha yenye mtu ni ya karibu na soko la samaki(ferry) asubuhi jua linapochomoza
Mkuu apk , shukrani kwa kushare picha nzuri na mandhari ya vivutio tofauti vinavyopatikana nchini kwetu, nimependa picha za lindi....mwisho wa mwaka huu nina road drive ya kusini mwa Tz nategemea kupita moja ya maeneo haya uliyoyaweka hapa.
 
  • Thanks
Reactions: apk
....Pamoja mkuu..
Kwa lindi mjini kuna kaview kazuri kipindi bahari imerudi nyuma na kuna jua ila kipindi cha mvua panaboa hasa..
Sehemu ambayo imetulia japo ni mbali kidogo kutokea lindi mjini wanapaita kuchele ya kitunda ndani ndani nauli ya pantoni 300 +boda 7,000 kwenda na 7,000 tena kurudi Kiingilio ni sawa na bure sema tu ununue soda 1000..Kuna view nzuri ila hakuna watu sana ile beach isipokuwa siku za sikukuu(mwenyeji alinipa hiyo taarifa) ila kama ni kwenda kwa ajili ya utulivu wa akili ni sehemu nzuri+network inasumbua sana pia kule🤣 so kama umeenda na mpango wa kuzima vifaa vyote vya mawasiliano kula hakuna haja kuzima😁..Kuna ngamia wawili wa kupanda na kupiga picha,kuna kitanda cha juu cha kulala kina view nzuri kabsa ya bahari,guest ya kulala hakuna ni almost kama matent na hivyo vyumba vilivyotengenezwa na miti..Vyakula naweza nikasema ni average tu sikuona wako serious na chakula..Naambatanisha picha chini hapa mkuu.
 
Mla Bata
Huku ni kuchele ya kitunda..Nilipapenda pamepoa..Zaidi sana waliopo ni wavuvi wako bize na kazi zao..Nimekumbuka pia kuna balcony moja walikuwa wanatengeneza kipindi hicho nadhani sahivi patakua pazuri zaidi kuongezeka kwa vikorombwezo hivyo.Beach ni nzuri na ni safi ila huduma za kijamii ndio kama zimekaa kushoto kidogo.
 

Attachments

  • PXL_20230918_112912042.jpg
    PXL_20230918_112912042.jpg
    4.1 MB · Views: 2
  • PXL_20230918_131830541.jpg
    PXL_20230918_131830541.jpg
    3.9 MB · Views: 1
  • PXL_20230918_121611243_055517.jpg
    PXL_20230918_121611243_055517.jpg
    3.1 MB · Views: 1
  • PXL_20230918_131921559_055559.jpg
    PXL_20230918_131921559_055559.jpg
    4.6 MB · Views: 1
Kwa uchache.

Zanzibar

Kuna Upande wa town, Stone town......

Hapa kuna utajiri wa kihistoria kuanzia magofu ya mji mkongwe wa stone town uliojaa mali kale za tamaduni ya bara la asia, tamaduni za wazawa na historia ya utamaduni wa "waswahili" wa pwani, vyakula (forodhani), viungo asilia (karafuu, amdalasini, hiriki), michezo na matamasha (Sarakasi, Sauti za busara, mwaka kogwa n.k)

Upande wa Shamba

Huku ndio upande wa beach nzuri na mahoteli mengi ya kitalii, snorkeling & diving sites, activities kama kuogelea na dolphin, kasa n.k hupatikana upande huu.

N.k kutembelea shamba inahitaji uwe na bajeti nzuri zaidi kuliko Stone town.
Ahsante sana mkuu, kwa hako ka bajeti kangu ntatoboa kweli? Au niendelee kujipanga🙆‍♀️
 
Mla Bata
Huku ni kuchele ya kitunda..Nilipapenda pamepoa..Zaidi sana waliopo ni wavuvi wako bize na kazi zao..Nimekumbuka pia kuna balcony moja walikuwa wanatengeneza kipindi hicho nadhani sahivi patakua pazuri zaidi kuongezeka kwa vikorombwezo hivyo.Beach ni nzuri na ni safi ila huduma za kijamii ndio kama zimekaa kushoto kidogo.
Service na customer care bado ni changamoto maeneo mengi ya vivutio vya utalii mkuu.

Shukrani sana sana mkuu apk hii location naiweka kwa bucket list lazima nipite mwisho wa mwaka, mandhari nzuri sana.
 
  • Thanks
Reactions: apk
Ahsante sana mkuu, kwa hako ka bajeti kangu ntatoboa kweli? Au niendelee kujipanga🙆‍♀️
Kama sikosei umesema wastani wa siku mbili/tatu si ndio?

Hapo bajeti itakuwa kipengere mkuu, labda kwa kujibana mnoo na usitake makuu 😂😂.
Ngoja tuanze kubreak down.....300k Tsh.

  • Nauli kwenda/kurudi , 🚢 daraja la kawaida- 35k x 2 = 70k

  • Accommodation 🛌 - Hapa ndio mtiti sana, kwa zanzibar kupata malazi kwa bei nafuu ni issue hasa kipindi cha high season ambapo wageni wanakuwa ni wengi sana, nashauri kwa bajeti hiyo muda mzuri ni wa low season, kipindi hiki ni kizuri tena ni vema ukatumia applications kama airbnb, booking.com kufilter accommodation kutokana na bajeti yako. Nimeattach baadhi ya accommodation zenye bei nafuu kwa kipindi cha low season kutoka airbnb na booking.com.Hapa tuweke bajeti kuanzia 45k (Tsh) per night x 2= 90k laki ishakata hapo 😂😂

N.B: Mitandao mingine ya kupata malazi ya bei nafuu ni pamoja na agoda, homestay, hostelwords n.k hizi wenzetu wazungu wanatumia sana hasa wale solo travellers, packpackers na wasafiri wengine wa bajeti nafuu.

  • Chakula 🍲🥘🥂- Hapa nitakuachia wewe mwenyewe kutokana na ulaji wako. Ila naamini huwezi kumaliza laki kwa siku mbili/tatu.
Kama utakuwa stone town muda wa jioni utahitaji kwenda forodhani kupata misosi, gharama za usafiri ni kama bara, boda boda ya kukutoa hotelini na kukurudisha kama accommodation itakuwa mbali. Mimi mara nyingi huwa kuna chimbo langu lipo karibu na bandarini nikifika S.town lazima nilale hapo na sihitaji usafiri kufika sehemu nyingi, ni mwendo wa "andha kanoon" tu kukata mitaa ya mji mkongwe kwa miguu.

Sasa mpaka hapo tumeshaona malazi na usafiri ushagharimu karibia laki na 80, bado hujala, hujanunua zawadi kwaajili yako na uwapendao (not important though) ila kuna jambo la msingi hupaswi kulikosa uwapo S.town. si jingine bali ni....

  • Excursions- Ukiacha kutembealea maeneo kama Old slave market kwaajili ya kuona historia ya biashara ya utumwa, kukatisa mitaa ya stone town kujionea mandhari mazuri ya magofu ya kale, ngome kongwe na vivutio vingine vinavyopatikana katikati ya mji ambavyo vingi havina gharama Ni vyema ukatenga kiasi cha pesa kwa ajili ya kutembelea vivutio kadhaa ambapo utahitajika kuwa na kiasi fulani cha pesa.
  1. A day trip to (Changuu) "Prison Island" & "Nakupenda beach" -Changuu/ Prison island kisiwa kidogo kilichojitenga, utapata kujua historia yake lakini pia utaweza kujionea kobe wakubwa wenye umri mpaka miaka 200 wanaopatikana hapo, vile vile utaweza kwenda kutembelea beach nzuri ya "nakupenda" kama ni mpenzi wa snorkeling basi hapa ni mahala pake, packae huhusisha chakula (sea food plata, viazi mbatata mkaango, matunda na soft drinks) kabla hujamaaliza trip yako.
Hapa kwa mTZ si chini ya elfu 80K Tsh kama utashare usafiri (boat) na wenzako.

Mpaka hapo utakuwa umepata mwanga wa bajeti kiasi gani utapaswa kuandaa, NB: Hii ni breakdown ya kujibana sana (budget) ila ukitaka makuu ya kwenda kulala 5 star hotel, Boat First class chakula 3 courses kazi kwako😂😂 .

Nina imani nitakuwa nimekupa ABCs za kutosha kwaajili ya safari yako, kama kuna cha kuongezea basi wengine watakuja kuongezea. Elli apk Mshana Jr Depal Paula Paul RRONDO
 
Kama sikosei umesema wastani wa siku mbili/tatu si ndio?

Hapo bajeti itakuwa kipengere mkuu, labda kwa kujibana mnoo na usitake makuu 😂😂.
Ngoja tuanze kubreak down.....300k Tsh.

  • Nauli kwenda/kurudi , 🚢 daraja la kawaida- 35k x 2 = 70k

  • Accommodation 🛌 - Hapa ndio mtiti sana, kwa zanzibar kupata malazi kwa bei nafuu ni issue hasa kipindi cha high season ambapo wageni wanakuwa ni wengi sana, nashauri kwa bajeti hiyo muda mzuri ni wa low season, kipindi hiki ni kizuri tena ni vema ukatumia applications kama airbnb, booking.com kufilter accommodation kutokana na bajeti yako. Nimeattach baadhi ya accommodation zenye bei nafuu kwa kipindi cha low season kutoka airbnb na booking.com.Hapa tuweke bajeti kuanzia 45k (Tsh) per night x 2= 90k laki ishakata hapo 😂😂

N.B: Mitandao mingine ya kupata malazi ya bei nafuu ni pamoja na agoda, homestay, hostelwords n.k hizi wenzetu wazungu wanatumia sana hasa wale solo travellers, packpackers na wasafiri wengine wa bajeti nafuu.

  • Chakula 🍲🥘🥂- Hapa nitakuachia wewe mwenyewe kutokana na ulaji wako. Ila naamini huwezi kumaliza laki kwa siku mbili/tatu.
Kama utakuwa stone town muda wa jioni utahitaji kwenda forodhani kupata misosi, gharama za usafiri ni kama bara, boda boda ya kukutoa hotelini na kukurudisha kama accommodation itakuwa mbali. Mimi mara nyingi huwa kuna chimbo langu lipo karibu na bandarini nikifika S.town lazima nilale hapo na sihitaji usafiri kufika sehemu nyingi, ni mwendo wa "andha kanoon" tu kukata mitaa ya mji mkongwe kwa miguu.

Sasa mpaka hapo tumeshaona malazi na usafiri ushagharimu karibia laki na 80, bado hujala, hujanunua zawadi kwaajili yako na uwapendao (not important though) ila kuna jambo la msingi hupaswi kulikosa uwapo S.town. si jingine bali ni....

  • Excursions- Ukiacha kutembealea maeneo kama Old slave market kwaajili ya kuona historia ya biashara ya utumwa, kukatisa mitaa ya stone town kujionea mandhari mazuri ya magofu ya kale, ngome kongwe na vivutio vingine vinavyopatikana katikati ya mji ambavyo vingi havina gharama Ni vyema ukatenga kiasi cha pesa kwa ajili ya kutembelea vivutio kadhaa ambapo utahitajika kuwa na kiasi fulani cha pesa.
  1. A day trip to (Changuu) "Prison Island" & "Nakupenda beach" -Changuu/ Prison island kisiwa kidogo kilichojitenga, utapata kujua historia yake lakini pia utaweza kujionea kobe wakubwa wenye umri mpaka miaka 200 wanaopatikana hapo, vile vile utaweza kwenda kutembelea beach nzuri ya "nakupenda" kama ni mpenzi wa snorkeling basi hapa ni mahala pake, packae huhusisha chakula (sea food plata, viazi mbatata mkaango, matunda na soft drinks) kabla hujamaaliza trip yako.
Hapa kwa mTZ si chini ya elfu 80K Tsh kama utashare usafiri (boat) na wenzako.

Mpaka hapo utakuwa umepata mwanga wa bajeti kiasi gani utapaswa kuandaa, NB: Hii ni breakdown ya kujibana sana (budget) ila ukitaka makuu ya kwenda kulala 5 star hotel, Boat First class chakula 3 courses kazi kwako😂😂 .

Nina imani nitakuwa nimekupa ABCs za kutosha kwaajili ya safari yako, kama kuna cha kuongezea basi wengine watakuja kuongezea. Elli apk Mshana Jr Depal Paula Paul RRONDO
Hapa nililala February kwa 50,000 ni jengo la zamani ila si mbaya. Nashauri budget ya accomodation aweke kuanzia 50,000 ndio standard. Huku ni juu
IMG_20240126_073418.jpg
 
Back
Top Bottom