Uzi wa kujifunza lugha ya Kiswahili

mzenjiboy

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
907
383
Nimeona katika jukwaa la lugha kuna “English learning thread” yaani uzi unaohusiana na kujifunza lugha ya English.

Nahisi itakuwa vyema wahusika wakaanzisha uzi mwengine wa kujifunza lugha ya Kiswahili kwa sababu humu JF kuna watu wengi lugha ya Kiswahili inawapiga chenga kwani tunaona maandishi yao.

Si kila mwenye kuzungumza Kiswahili huwa Mswahili. Lugha ya Kiswahili ina wenyewe.
 
Nimeona katika jukwaa la lugha kuna “English learning thread” yaani uzi unaohusiana na kujifunza lugha ya English.

Nahisi itakuwa vyema wahusika wakaanzisha uzi mwengine wa kujifunza lugha ya Kiswahili kwa sababu humu JF kuna watu wengi lugha ya Kiswahili inawapiga chenga kwani tunaona maandishi yao.

Si kila mwenye kuzungumza Kiswahili huwa Mswahili. Lugha ya Kiswahili ina wenyewe.
Kuna tofauti baina ya mjuzi na mweledi?
 
... kiwakilishi nafsi kiambata "a" kinadokeza nini?

... kwanza, kiwakilishi nafsi kiambata ni mofimu tegemezi zinazoambikwa katika neno au mzizi wa neno ili kudokeza nafsi inayohusika.

Hivyo, kiwakilishi nafsi kiambata "a" kinadokeza au kuwakilisha nafsi ya tatu umoja. Mfano, anasoma, analia, atakuja, n.k.
 
Back
Top Bottom