TUKANA UONE
JF-Expert Member
- Jan 3, 2018
- 1,816
- 5,151
Nitasema ukweli daima,Salamu kwangu Mwiko!
Sijajua kama wapo waganga wa Kweli kama tunavyoaminishwa ama laa!
Miaka fulani wakati najitafuta kama kijana,hali ya maisha ilikuwa ngumu sana,katika kujichanganya na wana mitaani nikakutana na mwana mmoja huko mkoani akaniaminisha ya kwamba kuna mtaalamu mmoja huyo ni noma na watu wengi wamefanikiwa kupata maisha kutoka kwake!
Ok!,nikamwambia mshikaji kama vipi anipeleke ili na mimi aweze kunitatulia changamoto zangu.
Tulipofika kwa huyo mtaalamu ukafika muda wa kupigiwa ramli chonganishi!,Mle ndani nikabaki mimi na yule mtaalamu!
Yule mtaalamu baada ya kupiga Ramli zake akaanza kuniambia eti "Bodaboda wenzio wanakuroga pale kijiweni hivyo wanataka kukuangamiza" 😂😂
Nilishangaa sana moyoni kwasababu sijawahi kuwa dereva wa Bodaboda tangu nizaliwe, kwakuwa sikutaka kumkatisha tamaa ikabidi niwe naitikia kama vile ni kweli mimi ni Bodaboda!
Baada ya hapo nilimpa hela na niliumia sana kutoa ile hela,na akanipatia dawa akawa amenielekeza namna ya kuzitumia!
Wakati tunarudi tukiwa njiani, yule mshikaji aliyenipeleka kwake akawa anamsifia sana yule mganga huku akiniuliza kama yote niliyotabiriwa ilikuwa kweli? Sikutaka kumkata jamaa asije akajisikia vibaya nikawa namwambia kila kitu nilichokuwa naambiwa kilikuwa sahihi!
Zile dawa nilipofika nilizitupilia mbali kabisa!
Tangu miaka hiyo sijawahi na sitokuja kumwamini mtu anayejiita Mganga kwasababu wote ni matapeli!
Sijajua kama wapo waganga wa Kweli kama tunavyoaminishwa ama laa!
Miaka fulani wakati najitafuta kama kijana,hali ya maisha ilikuwa ngumu sana,katika kujichanganya na wana mitaani nikakutana na mwana mmoja huko mkoani akaniaminisha ya kwamba kuna mtaalamu mmoja huyo ni noma na watu wengi wamefanikiwa kupata maisha kutoka kwake!
Ok!,nikamwambia mshikaji kama vipi anipeleke ili na mimi aweze kunitatulia changamoto zangu.
Tulipofika kwa huyo mtaalamu ukafika muda wa kupigiwa ramli chonganishi!,Mle ndani nikabaki mimi na yule mtaalamu!
Yule mtaalamu baada ya kupiga Ramli zake akaanza kuniambia eti "Bodaboda wenzio wanakuroga pale kijiweni hivyo wanataka kukuangamiza" 😂😂
Nilishangaa sana moyoni kwasababu sijawahi kuwa dereva wa Bodaboda tangu nizaliwe, kwakuwa sikutaka kumkatisha tamaa ikabidi niwe naitikia kama vile ni kweli mimi ni Bodaboda!
Baada ya hapo nilimpa hela na niliumia sana kutoa ile hela,na akanipatia dawa akawa amenielekeza namna ya kuzitumia!
Wakati tunarudi tukiwa njiani, yule mshikaji aliyenipeleka kwake akawa anamsifia sana yule mganga huku akiniuliza kama yote niliyotabiriwa ilikuwa kweli? Sikutaka kumkata jamaa asije akajisikia vibaya nikawa namwambia kila kitu nilichokuwa naambiwa kilikuwa sahihi!
Zile dawa nilipofika nilizitupilia mbali kabisa!
Tangu miaka hiyo sijawahi na sitokuja kumwamini mtu anayejiita Mganga kwasababu wote ni matapeli!