1.Mesut Ozil
Chini ya kocha Arsene Wenger, Mesut Ozil alikuwa mchezaji mwenye uhakika wa kupata nafasi katika kikosi cha Arsenal. Piga ua, asingekosekana kwenye kikosi cha wababe hao wa Emirates.
Lakini, chini ya kocha wa sasa, Unai Emery, Mjerumani huyo amekuwa akisugua benchi na kuweka benchi katika mechi zote kubwa.
Ozil wa sasa anapangwa kwenye zile mechi ambazo timu ina uhakika wa kushinda, lakini zile zenye utata, Emery hampangi kabisa kikosini na amekuwa akiona bora Aaron Ramsey au Alex Iwobi.