Sheikh23
JF-Expert Member
- Jul 11, 2016
- 1,128
- 1,842
Wakuu habari,pasi na shaka wengi wetu tumewahi kuhudhuria kwa mganga/waganga wa kienyeji kwa shida mbalimbali za miili yetu na maisha kwa ujumla.Nishee nanyi visa/madhira niliyowahi kuvisikia toka kwa watu wangu wa karibu ktk kutafuta uzima kwa wataalamu hawa;
1. Mzee jirani alipelekwa baharini usiku wa saa8 ili kuaguliwa,huko alikutana na watu wengi wakiwa na waganga wao,hakuna aliekuwa bize kumshangaa mwenzake,gari za kifahari zilikuwepo,kila mtu alikuwa na vifaa vyake vya kazi,mwenye mbuzi,kondoo,kuku,vyungu n.k,
Tiba ya mzee ilianza,mtaalamu alichanganya dawa kwenye chungu chenye moto,ubani na madawa ya marashi yanayopalia puani,sharti alilopewa mzee ni aingie Baharini mpaka maji yafike usawa wa shingo yake ndio atupe kile chungu kwa mbele na asigeuke nyuma.
Shida mwanaharamu,mzee alijitwisha chungu,hatua moja baada ya nyingine akielekea kwenye maji ya shingo(size),huku akipaliwa na moshi wa dawa na joto kali la mvuke kutoka kwenye chungu alichojitwisha kichwani.
Hakuna masharti mepesi kwa mganga,alipofikia maji size ya kifua chake,mawimbi yalianza kumpiga usoni na kumfanya ashindwe kupumua vizuri,hivyo alikitupa chungu kilichokua na dawa kabla ya kufikia maji ya shingo na kuharibu tiba ile. Mganga alimfokea sana na kumlaumu kwa kuharibu tiba. Ilibidi ipangwe siku nyingine kwa ajili ya kutekeleza tiba ile
2. Kisa cha pili,Mzee safari hii hakurudi kule kwa awali,ila masharti hayakuwahi kuwa mepesi,mganga wa pili alimtaka mzee akaoge barabarani,barabara ya lami kwenye pilikapilika za watu na biashara. Dawa iliandaliwa kwenye beseni ikiwa kwenye hali ya kimiminika.
Sharti likijirudia la kujitwisha(rejea mganga #1),safari hii akitokea nyumbani kwake mpk barabarani,kama ujuavyo beseni likijaa maji,ile kujitwisha beseni likamwaga maji tiba ikaharibika kwani hakutakiwa kumwaga hata tone mpk afike barabarani ambapo angetakiwa kuoga akiwa uchi wa mnyama.
Mganga alirudia kutengeneza dawa nyingine,safari hii alimtwisha mwenyewe ili tiba isiharibe,mzee alijitahidi kutembea kwa umakini na hakumwaga hata tone la maji mpk akafika barabarani.
Note:hakuna raia anaemwona ila yeye anawaona kwa jinsi alivyotengenezwa na mtaalamu kishirikina)
Kufika amefika,ishu ikawa atavuaje nguo aoge na yeye anaona kama watu wote wanamuangalia,mbaya zaidi sio mbali na nyumbani kwake,baada ya tafakuri dawa hii ilimwagwa na mzee akarudi nyumbani kupumzika
Visa ni vingi,hatuwezi kuvimaliza kwa andiko moja.
Ongezea kisa chochote ulichowahi kukutana nacho au kukisikia kwenye kutafuta tiba/uzima,mali au shida yoyote iliyokupeleka au kumpeleka jamaa yako kwa mganga wa kienyeji
................
Sheikh23
1. Mzee jirani alipelekwa baharini usiku wa saa8 ili kuaguliwa,huko alikutana na watu wengi wakiwa na waganga wao,hakuna aliekuwa bize kumshangaa mwenzake,gari za kifahari zilikuwepo,kila mtu alikuwa na vifaa vyake vya kazi,mwenye mbuzi,kondoo,kuku,vyungu n.k,
Tiba ya mzee ilianza,mtaalamu alichanganya dawa kwenye chungu chenye moto,ubani na madawa ya marashi yanayopalia puani,sharti alilopewa mzee ni aingie Baharini mpaka maji yafike usawa wa shingo yake ndio atupe kile chungu kwa mbele na asigeuke nyuma.
Shida mwanaharamu,mzee alijitwisha chungu,hatua moja baada ya nyingine akielekea kwenye maji ya shingo(size),huku akipaliwa na moshi wa dawa na joto kali la mvuke kutoka kwenye chungu alichojitwisha kichwani.
Hakuna masharti mepesi kwa mganga,alipofikia maji size ya kifua chake,mawimbi yalianza kumpiga usoni na kumfanya ashindwe kupumua vizuri,hivyo alikitupa chungu kilichokua na dawa kabla ya kufikia maji ya shingo na kuharibu tiba ile. Mganga alimfokea sana na kumlaumu kwa kuharibu tiba. Ilibidi ipangwe siku nyingine kwa ajili ya kutekeleza tiba ile
2. Kisa cha pili,Mzee safari hii hakurudi kule kwa awali,ila masharti hayakuwahi kuwa mepesi,mganga wa pili alimtaka mzee akaoge barabarani,barabara ya lami kwenye pilikapilika za watu na biashara. Dawa iliandaliwa kwenye beseni ikiwa kwenye hali ya kimiminika.
Sharti likijirudia la kujitwisha(rejea mganga #1),safari hii akitokea nyumbani kwake mpk barabarani,kama ujuavyo beseni likijaa maji,ile kujitwisha beseni likamwaga maji tiba ikaharibika kwani hakutakiwa kumwaga hata tone mpk afike barabarani ambapo angetakiwa kuoga akiwa uchi wa mnyama.
Mganga alirudia kutengeneza dawa nyingine,safari hii alimtwisha mwenyewe ili tiba isiharibe,mzee alijitahidi kutembea kwa umakini na hakumwaga hata tone la maji mpk akafika barabarani.
Note:hakuna raia anaemwona ila yeye anawaona kwa jinsi alivyotengenezwa na mtaalamu kishirikina)
Kufika amefika,ishu ikawa atavuaje nguo aoge na yeye anaona kama watu wote wanamuangalia,mbaya zaidi sio mbali na nyumbani kwake,baada ya tafakuri dawa hii ilimwagwa na mzee akarudi nyumbani kupumzika
Visa ni vingi,hatuwezi kuvimaliza kwa andiko moja.
Ongezea kisa chochote ulichowahi kukutana nacho au kukisikia kwenye kutafuta tiba/uzima,mali au shida yoyote iliyokupeleka au kumpeleka jamaa yako kwa mganga wa kienyeji
................
Sheikh23